Ngwananzengo
JF-Expert Member
- Jul 28, 2012
- 1,911
- 1,320
Wahenga hawakukosea waliposema kua uyaone. Rafiki yangu mmoja ambae tupo wote katika shughuli za kusaka tonge, alikuwa na tabia yenye kutia ukakasi. Kwa umri ana miaka 30 na kidogo na bado hajaoa. Katika mahusiano amekuwa akitoka na wake za watu. Tabia hii kwa kiasi imenifanya niwe nikimsisitiza kwa nini wake za watu? Yeye amekuwa akijibu mosi amekuwa na bahati na wake za watu kwani kila akitupa ndoano mambo huenda sawia.Pili anatafuta uzoefu kwa nini wake za watu wanaasi kiapo chao. Mimi ni nani nimhukumu jamaa yangu huyu. Kama ni uovu imesemwa siku ya kiama "kila mmoja ataubeba msalaba wake."Katika utafutaji kuna "sometimes Yes , sometimes No". Mwaka jana jamaa alianza kupata matatizo. Kila pesa ikiingia matatizo ndiyo yanaongezeka. Mwisho wa siku akasema Hapana lazima kuna kitu. Akajifikiria aende kwake yeye yule jana leo na hata milele akapige magoti. Katika kutafuta ushauri akaamua aende kwa "fundi". Alipofika akaambiwa ni kweli ana Tatizo la pesa kutokutulia na akapewa "dawa" za kutibu. Sharti alilopewa ni marufuku kutembea na wake za watu. Kwa kuwa alikuwa na nia ya kuondokana na Tatizo lake aliamua kufyeka michepuko yake na kurudi kuwa mwongofu. Tatizo limeisha na kile anachokipata walau kinatulia. Ama kweli sayansi zingine ni ngumu kuzielewa. Na kumbe laana zipo za Aina nyingi. Waliosema na wanaoamini mke wa mtu Sumu hawakukosea. Tukumbushane ule msemo wa wahenga waliposema, "Cha mtu m.a.v.I" na "mwenye chake muungwana".