Hawa walimu sikuwakuta, lkn huu mpira niliucheza. Ukiloa, kasheshe; ulikuwa unaongezeka uzito. Kilimi cha bladder kikijitokeza, mchezo unasimama kwa muda ili kirudishwe ndani.
Nyie mnabahati mpira wenu ilikua inajazwa upepo, wa kwetu ni mifuko ya rambo inafungwa kwa ustadi tu lakini ndimu ilikua inakamuliwa balaa.
Nimecheka sana leo! sikujua kama kuna wa long kiasi hiki ndani ya jf!! Hinzi enzi zingerudi nchi ingetengamaa sana
Kwa kweli hii ni burudani
Ukiona hicho kitabu na hako ka mpira unakumbuka enzi zipi?? Nini kilikua cha maana sana kwako wakati huo???
Yaani kwa kweli Kitabu cha Mr and Mrs Daudi kinanikumbusha viboko nilivyochapwa na baba enzi za uhai wake akiwa mwalimu wa kiingereza.
Shule niliyokuwa nasoma ilikua ni kijijini sana kiasi kwamba suala la uniform au sare ya shule sio ishu wewe ilimradi uje na kaptula tu na juu kama utapiga tshirt, flana shati ni uwezo wako tu. Mwenye kandambili yaani hizo akirudi nyumbani anaziosha anaziweka hadi kesho shule au zitavaliwa kwenye mtoko maalum.
Enzi hizo watu wakivuna mahindi, tulikua tunapita kuokoteza baada ya wenye shamba kuvuna kisha tunaenda kuuza.
Nikawa nimepata vijisent vyangu nikaenda mnadani nikanunua pensi, shati na mkanda. Kwa bahati mimi nilikua na sare za shule (baba alikua mwal. mkuu). Ila siku hiyo si unajua nilitaka nikawaonyeshee wenzangu pamba zangu mpya? Nikaulamba pekupeku nguo zangu mpya.
Huku nikiwa nimechelewa darasani, nilikuta baba (mwalimu wa kiingereza) anafundisha, aliponiona tu na mavazi yangu na nimechelewa, alinishushia kipigo cha mbwa mwizi, kisha akaniambia nisome aya kwenye kitabu cha Mr and Mrs Daudi. Kwa kuwa nilikua na hasira huku bado nalia na nnatakiwa kusoma kwa sauti ili darasa lote wasikie nilikua najikuta naanza kulia tena na kila nikilia naongezewa dozi ya viboko.
Umenifurahisha sana mkuu.