Ukimya wake unaniumiza

Ukimya wake unaniumiza

Kwanza ulifanya vizuri kuuliza future ya uhusiano wenu....mwaka mmoja unatosha kabisa kwa yeye kujua kama wewe ni chaguo lake ama vipi. lakini pia, hata wewe kujua, japo kwa maelezo yako unaonekana kuwa tayari yeye kufanya proposal ya kukuoa.

Sasa ni wakati wako kufanya maamuzi magumu, otherwise utajiweka kwake na baada ya miaka mingine miwili, ukajikuta unapigwa chini na anaolewa mwingine.

Ushauri: Ni bora ukawa singo, kuliko kuwa na mtu ambaye mmeishi mwaka mmoja na ana malengo lakini katika hayo malengo wewe sio sehemu yake.....Kwani huwezi kukituliza kwa mda, jaribu kukaa singo kwa mda..!
 
Kwa jinsi navyowafahamu wanaume hapo hamna kitu...

Anza upya mamii utapata wa kwako!
Na bora umeuliza mapema
 
Au alikuwa field kwako so muda umeisha? Lol
 
Huyo Ni Mbabe Wako Na Sio Mpz Wako.Chunguza majibu ya kukatisha tamaa anayokupa ameshagundua wewe umekufa kwake na hufurukuti so usipoangalia utakuwa mtumwa kwake na raha ya penz hutoiona.So jipe siku za kukaa kimya kusikilizia then toa maamuzi magumu.
 
msaidie kutimiza ndoto zake, nadhani hiyo ni moja ya njia kupata unacho kitaka.

toa na wewe upate
 
Mapenzi ya siku hizi ni shidaaa full stress kudadadeki
 
Habarini za asubuhi
wana Jamiiforums

Nombeni ushauri wenu, nina mpenzi . Jana nikauliza naomba kujua msimamo
wako juu ya mahusiano yetu. Akajibu binafsi nina malengo na ndoto zangu
kama unaona nakuchelewesha nakuruhusu nenda kwa mwingine atayekuoa
haraka.

Sikumiibu chcochote na mawasiliano yakaishia pale. Kila mmoja yupo
kimya, ukweli mimi naumia maana ninampenda,
sasa wadau nishaurini nianze tu mimi kumtafuta? Au niendelee kukaa kimya
au nifanyeje?

Ushauri tafadhali- mahusiano yetu yana mwaka sasa.

kimiya kimya usimtafte, kama anakupenda atakutafta.wanaume wa siku izi majanga anakufanyia vituko ili umuulize chochote apate pa kuanzia. plz usimtafte,
 
Sawa, pole sana...

Kwani yeye na wewe ni kama nani? wachumba au wapenzi wa kawaida TU?

Mliahidiana nini kwa muda gani? huo muda umisha pita au bado?

Ok, ni vizuri kujua mapema ili kuona mustakabali wako baadae..

subiri kama siku 3 usimtafute uone kama atakutafuta au lah!!

Moja ya makosa makubwa yanayofanywa na watu walioko kwenye mahusiano ni hili la kusema msubiri akutafute yeye. Mahusiano msingi wake mkubwa ni mazungumzo, kujaliana na kuthaminiana. Hivyo basi ukiona mmoja anaanza kuwa na mawazo ya kwa nini hajanitafuta au nani amuanze mwenzie hapo tayari kuna shia. Umpendae kitu cha kwanza ukiamka lazima utamani kumjulia khali (hata kama mnaishi wote). Sasa kama ninyi hamuongei kwa jambo dogo kiasi hiko inaonesha au mahusiano yenu yamegubikwa na unafki aidha kuna mmoja kati yenu anamtumia mwenzie. Ongea nae tena usisubiri akutafute, na la msingi lazima ujue kama mna ndoto za kuwa wote ni muhimu pia ukajua maswala yake ya muhimu (nikiamini na wewe ni mmoja wa hayo) pia ni vema mkaanza kushiriki katika kila mnalolifanya kwa heri.
 
Kujua muafaka ni muhimu lakini sa kamind nini, ndoto zinaweza kutimia hata baada ya miaka mia, pole mtafute tu huna haja ya kuendelea kujiumiza!!!!

Evelyn salt dada wa hekima...

Ni Moja kati ya majibu mazuri kutolewa kwenye post hii....

kuumia si kuzuri chamsingi we mtafute fanya kama hujui unajua wakati mwingine nyie dada zetu mnaona kuolewa ni kazi rahisi sana lakini mnasahau kuwa mzigo mkubwa katika maandalizi ya ndoa unakuwa upande wetu wakaka..Hivyo kama umegundua anakupenda upepee upendo wako usichoke mjali mkumbuke hata kwa msg..mchukulie kama zaidi ya rafiki fanya majukumu yale ambayo mtoto wa kike aliyempenda mvulana si kwa pesa zake, uzuri wake, umbile lake, dini au kabila lake BALI Kwa Moyo wake.

HIVYO

Mtafute tu utaona matokeo yake..yamkini ukaupdate hata mawazo yake akakushirikisha kwa nini mpaka sasa bado hajanza michakato ya kukuona pia ukahusika hata kumpa ushauri nini kifanyike..
N.B
Usiigize Upendo hayo yatokee moyoni kabisaa.



Nimeandika kwa haraka bila mpangilio lakini kwa sehemu naamini utachukua kitu na kitakusaidia.


kila la kheri!!
 
Last edited by a moderator:
Huyo Ni Mbabe Wako Na Sio Mpz Wako.Chunguza majibu ya kukatisha tamaa anayokupa ameshagundua wewe umekufa kwake na hufurukuti so usipoangalia utakuwa mtumwa kwake na raha ya penz hutoiona.So jipe siku za kukaa kimya kusikilizia then toa maamuzi magumu.

mmmmhhhhhh
 
una ushauri mzuri

Asante mwaya, ukishapata matatizo ndio unajua kuyakabili, mapenzi ni kizunguzungu yakikataa yanauma mno ila inabidi usonge mbele hakuna linaloshindikana ukidhamiria.
 
Habarini za asubuhi wana Jamiiforums

Nombeni ushauri wenu, nina mpenzi . Jana nikauliza naomba kujua msimamo wako juu ya mahusiano yetu. Akajibu binafsi nina malengo na ndoto zangu kama unaona nakuchelewesha nakuruhusu nenda kwa mwingine atayekuoa haraka.

Sikumiibu chcochote na mawasiliano yakaishia pale. Kila mmoja yupo kimya, ukweli mimi naumia maana ninampenda,
sasa wadau nishaurini nianze tu mimi kumtafuta? Au niendelee kukaa kimya au nifanyeje?

Ushauri tafadhali- mahusiano yetu yana mwaka sasa.

Pole dear.... tatizo sie binadamu huwa tunapenda kusikia yale ambayo masikio yetu yanapenda/yanataka kusikia.

Amekujibu kwa swali ulilomuuliza. Unataka nn tena? Kumlazimisha aukuoe au?
 
Huyo Ni Mbabe Wako Na Sio Mpz Wako.Chunguza majibu ya kukatisha tamaa anayokupa ameshagundua wewe umekufa kwake na hufurukuti so usipoangalia utakuwa mtumwa kwake na raha ya penz hutoiona.So jipe siku za kukaa kimya kusikilizia then toa maamuzi magumu.

Nakubaliana na ulichokiandika ......:bounce:
 
Asee umeshajibiwa kama unaona utacheleweshwa na kumsubiria tafta mwingine, hapo akili kumkichwa. unaweza kua na malengo na maisha yako ndio, ila wewe amekupa nafas gan ndani ya nafsi yake?? Anayathamin maisha yake vizur, je wewe upoje moyoni mwake??? Vunja ukimya ujue hatma yako kwake halafu ukimsubir je atakua wako bado????? Sijaelewa kwa nin kakaa kimya either kuna kitu nyuma ya pazia kua muwazi

Mbona mkuu mamaafacebook umemaliza meneno yote ...kazi kwake kufanyia kazi USHAURI ulio mpa.
 
Back
Top Bottom