Ibara ya 20(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977. Ibara hiyo inasema:
"Kila mtu anastahili kuwa huru, bila ya kuathiri sheria za nchi, kukutana na watu wengine kwa hiari yake na kwa amani, kuchanganyika na kushirikiana na watu wengine, kutoa mawazo hadharani..."
Hii ndiyo ibara inayotambuliwa kama msingi wa kikatiba wa uhuru wa kukusanyika na kuandamana kwa amani nchini Tanzania.