Ukimya wa Lowassa kuzungumzia rushwa katika chaguzi za CCM -- kulikoni?

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234
Jamani hii haikai sawa hasa kwa huyu mjamaa (EL) ambaye anadaiwa kuutaka urais kwa udi na uvumba, na anayeripotiwa yuko katika mkakakti kabambe wa kupanga safu yake katika chama chake kujihakikishia uteuzi wa kugombea kwenda Ikulu mwaka 2015.

Rushwa katika chaguzi zinazoendelea katika CCM si suala la siri tena -- liko nje nje kabisa. Takriban vyombo vyote vya habari hususan magazeti vimekuwa vikiripoti rushwa ikitembea katika chaguzui hizo, tena mara nyingine waziwazi.

Isitoshe hata mwenyekiti wa chama hicho (JK) amelizungumzia suala hilo kwa masikitiko makubwa.

Lakini kwa nini huyu mgombea mtarajiwa (EL) hata siku moja hatujamsikia akizungumzia rushwa kama ni kitu kinachomkera? kulikoni?

Naomba majibu jamani, na msianze kuzungusha zungusha (spinning) katika swali hili ambalo ni simpo kabisa,

Nawasilisha.
 
Swali lako limekaa kiuchokozi chakozi zaidi ingawa ni la msingi. Ni kweli EL hajazungumzia rushwa katika chaguzi katika chama chake na bila shaka yeye binafsi katumia sana rushwa kufanikisha kupanga safu yake ya kumpeleka Ikulu.

Kwa kifupi Watz wajiulize kwa makini iwapo mtu wa namna hii anafaa kuwa Ikulu. Hata hivyo naamini kuna watu humu JF wataanza kuzungusha mambo kama unavyosema -- na hasa iwapo uzi wako utadumu.
 
Yeye kakaririshwa slogan ya "Ajira is a time bomb" huku midomo inamtetemeka kama anadegedege.Huwa najichanganya nakuanza kuhisi labda alizaliwa kwa rushwa sasa nikijiuliza alitoaje rushwa wakati alikuwa kachanga ndo nagundua ninakosea.
 
Yaani haoni hata aibu kukaa kimya katika suala kubwa kama hilo linalokiangamiza chama chake na taifa kwa ujumla? Akiingia Ikulu tutarajia miaka kumi mingine ya danadana katika vita ya kupigana na rushwa. Yaana kwa ujumla itakuwa miaka 20 wasted, miaka ambayo nchi itazidi kudidimia na kukaribisha machafuko makubwa!
 
Ujajua huyu mtu anapelekwa sana na sifa yake ya utendaji wake wa kufuatilia maagizo kwa watendaji wakuu katika serikali -- kama vile tulivyoona katika kipindi chake cha U-PM kuhusu ujenzi wa sekondari za kata na kuhakikisha wanafunzi wengi waliomaliza darasa la 7 wanapata nafasi za sekondari.

Kwa hilo alipata sifa kubwa -- lakini suala la ufisadi kusimamia kwake ni NIL kabisa. Na hili ndilo linalochangia kuzorota kwa elimu na uduni wa shule hizo za kata kwani fedha nyingi za serikali hutafunwa kifisadi, badala ya kuziboresha shule hizo. Matokeo ni shule hizo kukosa walimu, madawati na maabara nk.
 
mkuu sijui hii mada umeiibua wapi maana ni ya msingi sana.
Kuongelea masuala ya ajira za vijana na kusahau kuwa Pesa Tz zipo, TRA na taasisi nyingine zinakusanya zaidi ya 600b kwa mwezi lakini kinachofanyika hakionekani sababu ya hiyo rushwa.
hii hoja ndio inaweza kuwa kipimo chake kizuri na sidhani kama anaweza kujinasua as he can't fool tz'an all the time
 
Duh swali kali...........................

Rushwa ni adui wa haki, haki ikikosekana hakuna amani bila amani hakuna maisha bora.
 
Rushwa ni adui wa haki kila sehemu ipo na ndiyo maana ikawekewa sheria, Lowassa unataka aseme kama nani wakati hayupo serikalini.
 
Yeye kakaririshwa slogan ya "Ajira is a time bomb" huku midomo inamtetemeka kama anadegedege.Huwa najichanganya nakuanza kuhisi labda alizaliwa kwa rushwa sasa nikijiuliza alitoaje rushwa wakati alikuwa kachanga ndo nagundua ninakosea.

Hapo kwenye red ndo nimepapenda kwelikweli, huyu jamaa kwa rushwa hafai. Ndo maana Nyerere alimshitukia mapema akampiga chini laivu. Tatizo jamaa kashawashika ccm, hawana namna ya kumuondoa. Isitoshe ccm yenyewe hii ya sasa ni uozo mtupu. ccm = rushwa.
 
Mkuu Counterpunch huyu jamaa hawezi kabisa kulizungumzia hili maana yeye ameamua kutumia rushwa ili kuhakikisha anaibuka kama mgombea wa magamba 2015. DHAIFU naye anamuhofia maana anajua uchafu wote walioufanya 2005 wa kugawa rushwa za mabilioni ili kuhakikisha DHAIFU anakuwa mgombea wa magamba. Sasa hivi fisadi Lowassa anajua wanasema kiwogawoga tu hakuna atakayethubutu kumgusa huyu.

Mimi naamini kabisa bila rushwa basi fisadi Lowassa kamwe hawezi kupata nafasi ya kuwa mgombea wa magamba lakini ndio hivyo ndani ya magamba ukitaka kugombea nafasi yoyote ile basi rushwa ni mbele kwa mbele.


Jamani hii haikai sawa hasa kwa huyu mjamaa (EL) ambaye anadaiwa kuutaka urais kwa udi na uvumba, na anayeripotiwa yuko katika mkakakti kabambe wa kupanga safu yake katika chama chake kujihakikishia uteuzi wa kugombea kwenda Ikulu mwaka 2015.

Rushwa katika chaguzi zinazoendelea katika CCM si suala la siri tena -- liko nje nje kabisa. Takriban vyombo vyote vya habari hususan magazeti vimekuwa vikiripoti rushwa ikitembea katika chaguzui hizo, tena mara nyingine waziwazi.

Isitoshe hata mwenyekiti wa chama hicho (JK) amelizungumzia suala hilo kwa masikitiko makubwa.

Lakini kwa nini huyu mgombea mtarajiwa (EL) hata siku moja hatujamsikia akizungumzia rushwa kama ni kitu kinachomkera? kulikoni?

Naomba majibu jamani, na msianze kuzungusha zungusha (spinning) katika swali hili ambalo ni simpo kabisa,

Nawasilisha.
 
Last edited by a moderator:
"(EL) ambaye anadaiwa kuutaka urais kwa udi na uvumba," Atazungumziaje, wakati mwenye umekiri kwamba anautaka kwa udi na uvumba?

Uwanja ni wa CCM kama kuingia ikulu ni kwa manemane, udi na uvumba.
 
Jamani hii haikai sawa hasa kwa huyu mjamaa (EL) ambaye anadaiwa kuutaka urais kwa udi na uvumba, na anayeripotiwa yuko katika mkakakti kabambe wa kupanga safu yake katika chama chake kujihakikishia uteuzi wa kugombea kwenda Ikulu mwaka 2015.

Rushwa katika chaguzi zinazoendelea katika CCM si suala la siri tena -- liko nje nje kabisa. Takriban vyombo vyote vya habari hususan magazeti vimekuwa vikiripoti rushwa ikitembea katika chaguzui hizo, tena mara nyingine waziwazi.

Isitoshe hata mwenyekiti wa chama hicho (JK) amelizungumzia suala hilo kwa masikitiko makubwa.

Lakini kwa nini huyu mgombea mtarajiwa (EL) hata siku moja hatujamsikia akizungumzia rushwa kama ni kitu kinachomkera? kulikoni?

Naomba majibu jamani, na msianze kuzungusha zungusha (spinning) katika swali hili ambalo ni simpo kabisa,

Nawasilisha.

unachokifanya wewe ni kama kumtaka shoga akemee ushoga! Unapozungumza suala la rushwa ni kama kumuita Lowassa kwa jina. Ni aibu ambayo itaendelea kumuandama kwa maisha yake yote japo tunajua kwamba wale wanaopaza sauti za kulisemea hili ndiyo watakuwa wa kwanza kunyongwa na kuteswa akishaapishwa kushika hatamu za utawala wa nchi hii, japo mimi nimekuwa nikisisitiza kwamba huyu bwana urais wa nchi hii atausikia kwenye bomba. Kila alipojisifu kwamba mtu wake ameshinda, matumizi ya fedha yamekuwa ni ya kutisha na bila aibu watu wake wanachekelea kununua ushindi.
 
Yeye ndo mtuhumiwa namba moja na Fredy mtuhumiwa namba mbili. Unategemea atasema nini. Yeye ndo kinara wa Rushwa ambaye anatumia umaskini wetu kuutaka sana urais. Shame on You Eddy.
 
EL hawezi kukemea rushwa kwa sababu huo ni mkakati wake aloupanga wa kumpeleka magogoni.
 
Jamani hii haikai sawa hasa kwa huyu mjamaa (EL) ambaye anadaiwa kuutaka urais kwa udi na uvumba, na anayeripotiwa yuko katika mkakakti kabambe wa kupanga safu yake katika chama chake kujihakikishia uteuzi wa kugombea kwenda Ikulu mwaka 2015.

Rushwa katika chaguzi zinazoendelea katika CCM si suala la siri tena -- liko nje nje kabisa. Takriban vyombo vyote vya habari hususan magazeti vimekuwa vikiripoti rushwa ikitembea katika chaguzui hizo, tena mara nyingine waziwazi.

Isitoshe hata mwenyekiti wa chama hicho (JK) amelizungumzia suala hilo kwa masikitiko makubwa.

Lakini kwa nini huyu mgombea mtarajiwa (EL) hata siku moja hatujamsikia akizungumzia rushwa kama ni kitu kinachomkera? kulikoni?

Naomba majibu jamani, na msianze kuzungusha zungusha (spinning) katika swali hili ambalo ni simpo kabisa,

Nawasilisha.

Yeye mweyewe ni rushwa, sasa ajiongelee mwenyewe!!
 
Kwa hili la kukaa kimya nampongeza Lowasa. Hakuna ushahidi wa moja kwa moja kwamba watu wanatoa rushwa. Tuliwahi kuwa na sheria ya TAKRIMA hapa. Ilifutwa? Lazima pia tutofautishe kati ya kutoa rushwa na kununua kura
 
Back
Top Bottom