Ben Saanane
JF-Expert Member
- Jan 18, 2007
- 14,581
- 18,124
kama ni simple jibu mwenyewe sisi tunajibu maswali magumu na kufanya maamuzi magumu.
I like this........
kama ni simple jibu mwenyewe sisi tunajibu maswali magumu na kufanya maamuzi magumu.
Huyu fisadi mnampa sifa na nafasi kubwa sana ambazo hastahili kwa vigezo vya uadilifu, upendo na uzalendo.
Lakini Watanzania ni wagumu kujifunza kutokana na makosa yao au ya wengine. Kikwete mlimpa urais kwa sababu ya "mvuto", EL mnataka kumpa kwa sababu ni tycoon na mfalme wa siasa uchwara za CCM, sio?
Anahusika vipi? Mbona yeye tulikuwa naye hapa mnazi mmoja kwenye vikoba, rushwa imetolewa huko Dom. Where is connection between suspects and EL?
-Lowasa ndiye aliyetumia kiburi kulazimisha mradi wa maji ya ziwa Victoria kwa kukiuka matakwa ya wamisri mapak leo wamisri wana mmind
-Lowasa ndiye aliyewalazimisha wizara ya elimu enzi hizo kuongeza boom la wanafunzi wa chuo toka sh 2500 enzi hizo na mpaka leo wizara ya elimu hawataki kumsahau
-Lowasa ndiye aliyewachimba mkwara wamalawi juu ya mgogoro wa mpaka mpaka leo hawataki kumsikia
-Lowasa ndiye aliyelazimisha mchakato wa kuleta umeme jimboni kwangu na mpaka nguzo zikasimikwa ila alivyoondoka tu wajanja wakazing'oa na hakuna kinachoendelea
-Lowassa ndiye aliye kiongozi mwenye maamuzi magumu na risk taker kuliko kiongozi yeyote mkubwa wa taifa hili ukiachilia mbali JK NYERERE
Kwanini nimchukie LOWASSA??una hoja yoyote ya msingi??
-Hujataja mvua za Thailand
-Hujataja shule za kata
-Hujataja jinsi alivyokua na ujasiri wa kusimamia RICHMOND
Hivi kama ana akili kiasi hiki ni kitu gani kilimzuia kuzungumzia kashfa za EPA na kupambana na wezi kama alivyopiganiq mradi wa ziwa victoria(utadhani yeye ndiye alikua Rais au waziri wa mambo ya nje)
-Kama ana ujasiri wa kupambana na wamisri maadui wa nje,ujasiri wake kukemea rushwa ndani ya chama chake na serikali uko wapi?au na yeye ni mmoja wao?
-Aliwatisha wamalawi kama nani?kwanza alionyesha immaturity kwa kuwa kauli ya waziri wa mambo ya nje ilikua very professional,ilitosha pamoja na kauli ya the acting leader of the goernment business in the house by then Hon.Samwel Sitta
Actually hautakiwi kumchukia mtu yeyote,hata shetani na uovu wake hustahili kumchukia ila unatakiwa kuchukia matendo na vishawishi vyake wicked!
taratibu za CCM za kukemeana zinafahamika haitakiwi kukemeana majukwaani , sasa iweje uhoji kutokukemea majukwaani na sio vikaoni??
tutafanya maamuzi magumu kwa kutegemea tetesi kuwa LOWASSA ni mtoa rushwa??
Kuhusu suala la RICHMOND ile ngoma ilikua ni ya bwana mkubwa na hilo linafahamika kujiuzulu waziri mkuu badala ya Rais kwa maslahi ya serikali ni moja ya technique za mchezo wa kisiasa...
sijaona maovu ya Lowasa zaidi ya hear says.......
kwa hiyo unataka kuniaminisha kuwa LOWASSA ni fisadi ???
kwa hoja zipi mpaka nikakubaliana na mawazo yako??
unachokifanya wewe ni kama kumtaka shoga akemee ushoga! Unapozungumza suala la rushwa ni kama kumuita Lowassa kwa jina. Ni aibu ambayo itaendelea kumuandama kwa maisha yake yote japo tunajua kwamba wale wanaopaza sauti za kulisemea hili ndiyo watakuwa wa kwanza kunyongwa na kuteswa akishaapishwa kushika hatamu za utawala wa nchi hii, japo mimi nimekuwa nikisisitiza kwamba huyu bwana urais wa nchi hii atausikia kwenye bomba. Kila alipojisifu kwamba mtu wake ameshinda, matumizi ya fedha yamekuwa ni ya kutisha na bila aibu watu wake wanachekelea kununua ushindi.