Ukikuyu mbioni kuja Tanzania

Ukikuyu mbioni kuja Tanzania

chikub

Senior Member
Joined
Oct 15, 2015
Posts
110
Reaction score
28
Haikuandikwa pahala popote, lakini Nyerere alijitahidi sana kuhakikisha kuwa mgombea urais nchini hatoki miongoni mwa makabila au kanda zenye watu wengi sana wanaofananafanana kitabia na kiutamaduni kama vile kanda za ziwa, nyanda za juu kusini, na mashariki mwa Tanzania.

Wachagga, wapare, wamasai, wambulu na waarusha kwa pamoja ni wengi na wana sifa sinazoshabihiana.

Wasukuma, wanyamwezi, waha, wahaya, wakerewe, wakuria, wajaluo na wagita ni wengi sana na wana tabia zinazosikilizana.

Mbeya, Iringa na Ruvuma ni wengi sana na wana tabia zinazorandana.

Hivyo, mgombea yeyote atakayetokana na makabila ya wasukuma, wanyakyusa na wachagga ana uwezekano mkubwa wa kuungwa mkono kwa wingi na watu wanaotoka makabila yao na makabila yaliyoko kwenye kanda zao na kusababisha makabila haya yawe kigezo cha kushinda uchaguzi Tanzania.

Hii inaweza kusababisha kila chama cha siasa kusimamisha mgombea wa kutoka makabila ya kisukuma, kichagga/kiarusha, au kinyakyusa ili kupata mtaji wa kura nyingi.

Hii itakuwa sawa na Kenya ambako kabila la Kikuyu na Kijaluo ndiyo yenye kura ya turufu ya kushinda uchaguzi wa urais. Tukifanya hivyo sisi Tanzania tutakuwa tunarudi nyuma kule tuliko toka.

Kila mtu anayo haki kikatiba ya kuchagua na kuchaguliwa, lakini tunajiandaaje kukabiliana na hatari ya kurejesha ukabila nchini ndio jambo la msingi linalopaswa kujadiliwa kwenye uzi huu.
 
Wewe nawe ni mkabila tu, Kwani Magu ni Msukuma?????
 
Huo ulikuwa mtazamo wake tena kwa miaka hiyo.Kubania makabila mengine kwa kisingizio cha kuogopa kutugawa kikabila nao ni ukabila tu.
 
ndiyo magu ni wasukuma kabisaaaaaaaaaa, lakini cha msingi hapa ni kwamba tunachagua rais si kwa kuangalia kabila lake bali uwezo wa kuingoza tz,
 
Wewe nawe ni mkabila tu, Kwani Magu ni Msukuma?????

Miongoni mwa mapungufu makubwa tuliyonayo watanzani,tena bila kujari viwango vya vyeti tulivyopata mashuleni na vyuoni ni kutofikiri kwa mapana na kina kabla ya kujibu/kusema tunachodhani ni sahihi.Ukanda na ukabila ktk uchaguzi huu ulikuwa ni turufu ya nini utapata ktk sanduku la kura kwa wagombea u-rais. Ni tatizo kwa mtu kulipinga hili maana zipo sms kwa watu zilizokuwa zinahimiza ukabila waziwazi.
 
Hoja mufilisi. Kwa hiyo hayo makabila ulotaja hayapaswi kutoa rais? Nasikia Tanzania hakuna ukabila, mtoa mada unautoa wapi au wewe si Tanzania?
 
Mbona hujamtaja yeye Nyerere Mzanaki, unadhani anatofauti sana na Mjita?
 
Miongoni mwa mapungufu makubwa tuliyonayo watanzani,tena bila kujari viwango vya vyeti tulivyopata mashuleni na vyuoni ni kutofikiri kwa mapana na kina kabla ya kujibu/kusema tunachodhani ni sahihi.Ukanda na ukabila ktk uchaguzi huu ulikuwa ni turufu ya nini utapata ktk sanduku la kura kwa wagombea u-rais. Ni tatizo kwa mtu kulipinga hili maana zipo sms kwa watu zilizokuwa zinahimiza ukabila waziwazi.

Na ndio mana mkishachanganyikana watu tofauti bila kuwa na muono unaofanana maendeleo ni mbinde mno. Divide and rule ndo nzuri ili kuwatawala ukabila ndo unaofanya Africa aiendelei. Ndo mana nchi zilizoendelea bila mchanganyiko wa jamii tofauti na tatizo la nchi hii level ya ignorance ni kubwa kuliko maelezo
 
Huo ulikuwa mtazamo wake tena kwa miaka hiyo.Kubania makabila mengine kwa kisingizio cha kuogopa kutugawa kikabila nao ni ukabila tu.
Kati ya vitu anavyosingiziwa Mwalimu hiki ni kimojawapo. Mwalimu hakuwa na hulka ya ukabila na hakuona kuwa kuna makabila yanayofaa kuongoza na makabila yasiyofaa. Tumhukumu Mwalimu kwa vitendo vyake na si hisia kama hizi za kiwazimu. Mbele ya Mwalimu Watanzania wote walikuwa sawa, na hili aliridhihirisha kwa vitendo na mahusiano yake.
 
Miongoni mwa mapungufu makubwa tuliyonayo watanzani,tena bila kujari viwango vya vyeti tulivyopata mashuleni na vyuoni ni kutofikiri kwa mapana na kina kabla ya kujibu/kusema tunachodhani ni sahihi.Ukanda na ukabila ktk uchaguzi huu ulikuwa ni turufu ya nini utapata ktk sanduku la kura kwa wagombea u-rais. Ni tatizo kwa mtu kulipinga hili maana zipo sms kwa watu zilizokuwa zinahimiza ukabila waziwazi.

Mi nahitaji uthibitisho wa huo ukabila maana sijaushuhudia na nilibahatika kuzunguka maeneo mengi japo sikuwa kisiasa.
 
Mleta mada nae ni wa kupuuzwa tu hebu basi atuambie yy anamtaka nani wakabila gani ashike dola ya tz????
 
Nyerere hajataka makabila ya kusini kutoa rais kutokana na ubaguzi wake wa kikabika tu.( Yeye ndio kaanzisha ukabila)
 
Na ndio mana mkishachanganyikana watu tofauti bila kuwa na muono unaofanana maendeleo ni mbinde mno. Divide and rule ndo nzuri ili kuwatawala ukabila ndo unaofanya Africa aiendelei. Ndo mana nchi zilizoendelea bila mchanganyiko wa jamii tofauti na tatizo la nchi hii level ya ignorance ni kubwa kuliko maelezo

Angalia chimbuko la maendeleo ya North America kuanzia Karne ya 18 na mchango wa diversity (mchanganyiko/tofauti ndani ya jamii) kwenye hilo.
Umeandika kutetea ukabila kiaina. Kuna watu Kuoa, kuchagua kiongozi au hata kunywa bia na mtu nje ya kabila lake ni shiiida! Ni mawazo mfu tu.
 
ukabila / ukanda na udini shida sana. mtu anaweza kuwa mzembe, mwizi /fisadi, na nk lakin watu wakampigia kura kwasababu tu ni kabila lao au anatoka kanda moja na wao au dini moja

walaaniwe mafisadi
 
Makabila madogo mlikuwa mnashabikia sana hizi mambo lakini madhara yake yanaweza kuwa cost Kwa Miaka 450 ijayo.Haya makabila hasa wasukuma wanaweza kuwa watawala WA nchi hii Kwa miaka zaidi ya 100 to come.
 
Back
Top Bottom