Hatuwezi kukubali mafisadi..Hao kina kingunge na EL bakini nao wenyeweHuyu, Mgeja na wenzake wa aina hiyo si cho chote, na hizi wala si habari. Labda kwa mbali ingekuwa Sumaye au Kingunge. Ikitokea ikawa ni EL hapo sasa ndiyo ingekuwa HABARI, nchi ingetikisika, upinzani ungegalagala na CCM ingerukaruka! Hili sidhani kama linaweza kutokea.
Mwambie huyo na wenzake wote. Wakati ule tukiwa tunamaliza elimu ya sekondari kidato cha sita kabla ya kwenda vyuoni tulikuwa lazima tuende National Service kwa mujibu wa sheria, na huko ilikuwa lazima upewe kadi ya chama kwa maana kwanza chama kilikuwa kimoja. Jee watasema vijana wa wakati huo walikuwa wanaipenda CCM?
Ndivyo ilivyo sasa hivi na Mwapachu katudhibitishia, kwamba heri kuwa CCM ili shughuli zake na washirika wake zisikwame. Hivyo sio chama cha moyoni hata kidogo bali kuna uanachama wa maslahi.
Watu kama Mbowe, Baregu, Lissu, Mdee, Seif nk nk ambao kwa nafasi na taaluma zao wangeweza kuwa ccm na maisha yakasonga mbele lakini kila siku wanapambana na virungu na mabomu na hawaachi ni wa kuwaangalia mara mbili mbili na kuwakubali kuwa ni wazalendo halisi sio maslahi.
Hebu watuambie, mtu kama Lissu leo akisema nahamia CCM sii itakuwa sherehe na pengine yaweza kufanywa siku ya mapumziko kitaifa?
Saruti kwako kamanda umenena ukweli mtupu.Ukawa yaanza kupasuka katika hali ya kushangaza wanachama wengi wachadema waobesha hali ya kuikubali ccm, hii ni dalili tosha kabisa ya kifo cha ukawa. Week iliyoopita wanachama zaidi ya mia hamsini walikihama chadema na kurudi ccm, Leo tena mwapachu aliyeihama ccm kwa mbwebwe na kwenda ukawa arudi kwa mwenyewe ccm, na tetesi zinaonesha kesho pia SAA NNE mgeja na wenzake baadhi wanachama was chadema tegemeo watajiunga ccm ili kuudhihirishia umma was tz kuwa sasa ccm ya mwl imerudi. Hali hii imemfanya mbowe kuchanganyikiwa na sasa anatapatapa hajui afanyeje kuuzuia upepo wa magufuli unaowavuta wengi ccm. POLE SANA NYUMBU HALI TETE KIBANDA KINATEKETEA
Hatuwezi kukubali mafisadi..Hao kina kingunge na EL bakini nao wenyewe
Babu anacheza na wajukuuMzee Mwapachu hajafanya vibaya yuko sahihi.....lakini kwa Muungwana angekufa na tai yake shingoni.Kamwe asingekula matapishi.Hata hivyo umri umekwenda.
RURU KWERILeo amekuwa siyo chochote tena mbona alikuwa ndiyo ruru kwenye kampeni zenu kweli nyie viazi.
Kwenye siasa yote yanawezekana,ulijua Leo El angekua chadema Na zile kauli zake anayetaka nihame mie ahame yeye Mimi sihami ng'oooo ziliishia wapi? Uliwahi kuwaza chadema wanaweza kupokea El hata siku moja kutokana Na tambwe zao kua huyu mtu kua ni fisadi papa?Huyu, Mgeja na wenzake wa aina hiyo si cho chote, na hizi wala si habari. Labda kwa mbali ingekuwa Sumaye au Kingunge. Ikitokea ikawa ni EL hapo sasa ndiyo ingekuwa HABARI, nchi ingetikisika, upinzani ungegalagala na CCM ingerukaruka! Hili sidhani kama linaweza kutokea.
Kajifunze kutawadha kuondoa najisiSasa kaa hapo usubili ukawa kama utaisikia tena, wenye akili washastuka gemu LA ukawa linaenda doda, hali tete, katibu mwenyewe mpya hana mvuto wa kisiasa wala mmashiko kwa jamiim
Ninachoamini tunahitaji sana upinzani makini ili nchi hii isonge mbele. Wala tusidanganyike kuwa Mawazo ya upande mmoja yatajenga nchi. Mawazo mbadala ni muhimu mno katika kuongoza walio madarakani kujitafakari,kujikosoa na kuamsha fikra mpya ilikuleta mabadiliko. Hivyo ni muhimu chadema kujipanga kifikra na kimtazamo ili waweze kuja na mbinu mpya za ki upinzani zitakazo wasaidia kuleta kasi ya mabadiliko na hatimaye kushika dola kama wanahitaji.
Kwa mtu makini sio vyema kubeza upinzani, muhimu ni kujenga hoja zitakazo wa saidia waende mbele. Tunawahitaji sana kwa ajili ya maendeleo endelevu ya Tanzania
UKAWA ipo kwenye mioyo ya nyumbu, Malofa na wapumbavu TU.Kaka UKAWA iko kwenye mioyo ya WaTz kwa sababu. Hizi mbwembwe za Lumumba zitapita lakini makusudi ya ukawa yatasimama.
Magufuli hata kama ni mzuri kumbuka ni mwanadamu. Taasisi zetu bado ni kubogoyo.