UKAWA wote nipeni majibu

UKAWA wote nipeni majibu

Tunaitwa nyumbu kwa sababu kila anachoongea mbowe sisi tunaunga mkono tu
 
Unazunguka mbuyu sababu mbili zinazo maanisha kitu kimoja?
 
Uliposoma katiba ya CHADEMA ukagundua kuwa kuna kifungu kinachowataka wanachama kuwaunga mkono wagombea wanaopitishwa na chama? Kwa hiyo ukaogopa kuhama kwa kuwa utakuwa unavunja katiba ya chama? Toka lini kuhama chama imekuwa ni kuvunja katiba ya chama? Inawezekana hujui unachokizungumza.

hahaaha nashukuru umenisaidia kuuliza nilichotaka kuuliza
 
Hebu kwanza tuwe wakweli, umesema "ana madoa" na hii ya kusema kwamba ana "madoa" ni hoja inayotoka CCM lakini mwisho wa siku wanaishia kusema habari ya Ritchmond. badala ya kutumia wingi muwe mnatumia umoja kwa kusema "ana doa" kwani hoja yenu imejikita kwenye Ritchmond.

Wakati fulani huko siku za nyuma tulikuwa na usemi usemao "elimu haina mwisho". Maana ya usemi huu ni kwamba hakuna mwisho wa kujielimisha kuhusu jambo fulani. Zama za kale ilikuwa inaaminiwa kuwa dunia imebebwa juu ya Pembe za mnyama mmoja mkubwa sana anayefanana na Ng'ombe, na mnyama huyo anapojitikisa ndipo yanapojitokeza matetemeko ya ardhi, mpaka leo bado tunaamini hivyo? Sayansi imetusaidia kubadili mtizamo huo wa kizamani kuhusu Dunia na ulimwengu!

UKAWA na CHADEMA wameshajielimisha sana kuhusu sakata la Ritchmond na yatokanayo, ndiyo maana Tundu Lissu alisema kampuni ya Ritchmond Mhusika wake ni Kikwete lakini cha ajabu ni kwamba nyie hamsemi kuwa hilo ni doa kwa Kikwete na Serikali yake!

Lowassa anaposema kwamba mwenye ushahidi aende mahakamani anaongea kimantiki, kwani CCM wanalifanya suala la Ritchmond ni la Kijinai kwa ivo kama ni la kijinai basi ni lazima lipelekwe mahakamani. Kama hamuelewi ni kwa nini Lowassa anasema mwenye ushahidi aende mahakamani basi tena hakuna jinsi ya kuwaelewesha.

Mitambo ya Ritchond ni haramu? si ndiyo ya DOWANS na si ndiyo inayoendelea kutumiwa na Symbion? Symbion imetoa misaada kiasi gani kwa jamii na Serikali yetu, fedha zinazotumiwa kutoa misaada hiyo si zinatokana na uzalishaji wa umeme unaofuliwa na Mashine Haramu zilizoletwa na Ritchmond? Au ndiyo mambo ya Baniani Mbaya kiatu chake dawa?

Muheshimiwa kama ukipewa nafasi ya kufundisha mjinga nina uhakika ataelewa vizur sna na asipojua milele awezi jua comment yko naomba nitumie kufundisha wengine
 
Nimekuelewa mtoa mada,wengi wanaijiita CHADEMA ni bendera fuata upepo,hawana fikra huru na ndio maana kuchambua yaendeleayo ndani ya chama au kusikiliza na hoja kinzani toka kwa Wana mabadiliko wengine imekuwa changamoto kubwa kwao.
To be honest CHADEMA imepoteza mwelekeo sasa hivi,hawaeleweki wanasimamia mini,Leo wanasema hiki halafu kesho utawaona wakifanya kitu tofauti kabisa. Wanahitahitaji kiongozi atakayerudisha self identity ya chama iliyopotea,wanatakiwa wawe na kiongozi atakayekuwa tayari ku_reshape the party's image and retool the party's message. Mbowe is completely washed up.
 
WanaJf,

Naamini uchaguzi umeisha na Magufuli ni rais, iwe kwa halali au kwa njia za panya ila ndio rais, kuna lalamikalalamika ya viongozi wetu wa CHADEMA na ukawa kiujumla, kwamba tuliibiwa kura za rais, jambo ambalo mimi siliafiki na nmekuwa nikikwaruzana na wanachama kadhaa wa CHADEMA na kuitwa msariti, mnafiki, gamba, mamluki, CCM.

Ninachopingana na wenzangu ni kwamba hatukuibiwa kura, bali tulikosea kuweka mgombea urais ambaye ana madoa na tumemuimba miaka 8, tumemwita fisadi, mwizi sugu harafu leo anagombea urais, hivi mlitegemea wananchi wangetuelewa vipi?

Sasa naomba mwana ukawa yeyote anieleze"hivi kuhusu Richmond, Lowassa amewahi kujieleza hadharani na tukamuelewa? Mimi binafsi najua akiulizwa utasikia "mwenye ushahidi aende mahakamani" sasa hapo kajibu nini?Au utasikia "hakuna nililofanya ambalo raisi alikuwa hajui", sasa hilo ndio jibu?

Naomba mtu wa UKAWA mwenzangu anipe jibu je Richmond, Lowassa amewahi kujieleza akaeleweka? Kama hapana basi hatukuibiwa kura.

atakayetoa jibu la maana nimensheni nije kulisoma

Mkuu jibu ni jepesi sana,kama umewahi kufatilia waziri/waziri mkuu akiapa anakula kiapo cha kutunza siri za baraza la mawaziri hivyo usitarajie hata siku moja kwny maisha yako kumsikia Lowassa akijisafisha kuhusu richmond hadharani labda kwa amri ya mahakama,nilishangaa hata Dr. Slaa kudai Lowassa ajisafishe hadharan zaid ya kusema sihusiki huku akijua kiapo kinambana.
 
Kweli mbowe amewashika sana vijana wa bavicha,mimi kanikosa safari hii nmeshtuka,haiwezekani mtu walituambia ni mwizi,fisadi papa,leo eti awe msafi gafra

Kwaiyo unaona bora yule aliyekwambia sio mwiz 2008 na leo anasema ni jambazi kabs ebu chumbua yupi bora mana ata upande huo unaounga mkono nao umetoa kauli mbili sasa jaribu kazi ya majaji tuone watanzania ndo tabia yetu au vilema vya waliokua kwenye system
 
Kwa hiyo serikali ya ccm iliendelea kumlipa Lowassa fedha kupitia (Richmon baadae Dowans na baadae tena Symbion Powers) baada ya yeye kujiuzulu? Kama sio yeye aliyekuwa analipwa ni nani?

Kama kweli ni yeye mahakama zote ni za ccm, kwanini hawafungui mashitaka? Kikwete alitajwa na Lowassa siku aliyokabidhiwa kadi ya CHADEMA, kwanini hakukanusha mpaka siku ya mwisho wa kampeni? Alikuwa anahofia nini kumjibu kwa muda wote wa miezi mitatu (3) mpaka aje kulizungumzia tarehe 24 ambapo anajua hakutakuwapo tena muda wa kumjibu endapo atasema uongo?

Ukiamua unaweza kutafuta majibu ila kama pia unaweza kuendelea kuwa msukule wa kufuata kila kinachosemwa na ccm yako.
 
Mwanzo hata mimi niliaminishwa kwamba lowassa anahusika kwenye richmond , lakini baada ya kujionea richmond ndiyo symbion na kwamba obama alikuja kuizindua tena wakati lowassa kishawajibika , halafu pale kati hii hii richmond ikaitwa Dowans , nikatafakari halafu nikapima mwenyewe , maana wahenga walisema , hata kama kuona huwezi basi hata kupapasa umeshindwa ?
 
WanaJf,

Naamini uchaguzi umeisha na Magufuli ni rais, iwe kwa halali au kwa njia za panya ila ndio rais, kuna lalamikalalamika ya viongozi wetu wa CHADEMA na ukawa kiujumla, kwamba tuliibiwa kura za rais, jambo ambalo mimi siliafiki na nmekuwa nikikwaruzana na wanachama kadhaa wa CHADEMA na kuitwa msariti, mnafiki, gamba, mamluki, CCM.

Ninachopingana na wenzangu ni kwamba hatukuibiwa kura, bali tulikosea kuweka mgombea urais ambaye ana madoa na tumemuimba miaka 8, tumemwita fisadi, mwizi sugu harafu leo anagombea urais, hivi mlitegemea wananchi wangetuelewa vipi?

Sasa naomba mwana ukawa yeyote anieleze"hivi kuhusu Richmond, Lowassa amewahi kujieleza hadharani na tukamuelewa? Mimi binafsi najua akiulizwa utasikia "mwenye ushahidi aende mahakamani" sasa hapo kajibu nini?Au utasikia "hakuna nililofanya ambalo raisi alikuwa hajui", sasa hilo ndio jibu?

Naomba mtu wa UKAWA mwenzangu anipe jibu je Richmond, Lowassa amewahi kujieleza akaeleweka? Kama hapana basi hatukuibiwa kura.

Ndugu hebu fikiri, kama richmond ni ya Lowasa iweje alipwe mpaka leo ilihali tayari ni mpinzani? na hiyo richmond ndio dowans na ndiyo Symbion, naona uvivu wako tu wa kufikiri
 
"kama unaushahidi nenda mahakamani kama huna shutup"ni kweli walishutup lakini waliongea kupitia ballot boxes-and now the shut up is twisted.
 
Back
Top Bottom