Ukawa wasipojiangalia watakosa mgombea

Ukawa wasipojiangalia watakosa mgombea

Naboti

Senior Member
Joined
Apr 17, 2015
Posts
188
Reaction score
48
Hivi vyama vinavyounda Umoja wa katiba wa wananchi visiposoma vizuri katiba ya nchi hii ikifika mwisho wa siku tutajikuta tunachagua magufili VS kivuli.
Hii ni kutokana na sheria ya uchaguzi inavyosema kuwa mgombea ana anapaswa kuwa mwanachama wa chama husika kwa muda usiopungua miezi mitatu kabla ya kuanza mchakato wa kuchukua form ya kugombea nafasi ya uongozi kupitia chama hicho. Mgombea wa UKAWA sidhani kama ata kuwa amekidhi vigezo hivyo ni dhahiri mwisho wa siku UKAWA wakajikuta hawana mgombea heri wamrudishe Dr. Slaa ulingoni.
Wote tunapenda mageuzi tujitahidi kulitafakari hili tuone suluhu itakuwa ni nini ili mwisho wa siku tusije kunaswa kwenye mtego wa CCM
 
Naona mmeshikilia sana kipengele hicho dhidi ya EL.

Mmeona mkimbambikiza kesi atawaumbua.

Jaribuni leteni hoja yoyote mpambane na kamanda LISSU.
 
ahahaha,katiba haina hicho kipengele,sheria za uchaguzi zote hazina hicho kipengele na hata sheria ya vyama vya siasa hazina hicho kifungu,achilia mbali katiba pendekezwa!acha kuota ww gamba!
 
Mtaweweseka sana mwaka huu ccm kwishney.mkienda kuzimu msalimie Komba
 
Wakuu tusaidiane wekeni hiyo sheria tusome na km kweli Lissu afanye haraka kuisoma ili tusipotee
 
Magamba wana akili sana isije dakika za mwisho waka leta hoja tuka chelewa kufanya maamuzi
 
nimesoma kifungu kwa kifungu nukta kwa nukta sheria ya uchaguzi na sheria Ya gharama za uchaguzi hamna kipengele kinachoongelea hio ishu so msikuze mambo someni kwanza NO RESEARCH NO RIGHT TO SPEAK.....umeyabeba tu huko fasta unakuja mbio alafu kijana aaaaaaaaaaghrrrrr
 
Uanachama wa mtu na muda wa kushiriki uchaguzi ni maamuzi ya vyama vyenyewe. Katiba za vyama ndi mwamuzi.
Tume haina mamlaka hayo kwa kuweka kipengele hicho ni kwenda kinyume na katiba zs vyama husika.
 
Sifa ni awe mwanachama wa chama cha siasa hayo mengine umeongeza ya kwako na pengine ulikuwa unasoma katiba ya chama chako
 
Hivi vyama vinavyounda Umoja wa katiba wa wananchi visiposoma vizuri katiba ya nchi hii ikifika mwisho wa siku tutajikuta tunachagua magufili VS kivuli.
Hii ni kutokana na sheria ya uchaguzi inavyosema kuwa mgombea ana anapaswa kuwa mwanachama wa chama husika kwa muda usiopungua miezi mitatu kabla ya kuanza mchakato wa kuchukua form ya kugombea nafasi ya uongozi kupitia chama hicho. Mgombea wa UKAWA sidhani kama ata kuwa amekidhi vigezo hivyo ni dhahiri mwisho wa siku UKAWA wakajikuta hawana mgombea heri wamrudishe Dr. Slaa ulingoni.
Wote tunapenda mageuzi tujitahidi kulitafakari hili tuone suluhu itakuwa ni nini ili mwisho wa siku tusije kunaswa kwenye mtego wa CCM

layman bhana mnasumbua sana,kisheria hatuongei maneno tupu(mere words),weka facts zikisupotiwa na authority(law,books,decided cases etc),
-turud kwenye hoja unaongelea sheria ya uchaguzi ipi ya mwaka gani(full citation)
-kipengele,kifungu au ibara namba ngap? je hata kama ingekuepo km general rule,hakuna exception? -- je utafsiri wake ungekuaje(liberal or literal interpretation)?
-mwisho tuangalie kwa wenzetu kama ilishatokea kesi kama hiyo waliamuaje?
 
Labda warudi tena BUNGENI na kuipitisha hiyo sheria harakaharaka kwa kusema ndiyoooo.....!

hata kama wakifanya hivo haisaidii sheria inaact retrospectively na sio atrospectively,yani huwezi tunga sheria Leo ili umbane alofanya tendo jana ambalo sheria hiyo inalitambua kama kinyume,hivo watabanwa kuanzia sheria hiyo itakapopewa makali kuanzia ilipotangazwa
 
Back
Top Bottom