Wandugu kunatetesi kuwa UKAWA wameingia hasara kubwa sana katika zharambee iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita.
Waalikwa waliojitokeza kwa kuchangia Harambee husika walikuwa wachache sana na inasemejana ilipatikana milioni ishirini tu!
Gharama za ukumbi peke yake pale !limani City ni milioni 30, na chakula cha waalikwa ilikuwa kama milioni 20.
Kina
TAMKO ,
chakii ,
TeamLowassa ,
kbosho ,
japanese ,
Watu8 , [MENTION]Mzee kabwela[/MENTION]na wengine wengi hawakujitokeza kuchangia.
Hivyo UKAWA imebugi na kuingia hasara kubwa, na hilo ni trailer ya 25 October 2015.
Watalijua Jiji.
Ndugu yangu masopakyindi umefanya watu wapaniki.
Hakuna haja ya kupaniki. Ni lugha ya kifasihi tu inayotumika kuwaonyesha kuwa watu wamepigwa changa la macho na kubadilishiwa gia angani na kamanda wa anga. Usihamaki tafadhali nitaeleza kidogo.
1. Mleta mada anadai kumepatikana hasara; kama kumepatikana hasara kuna atakayehoji matumizi ya michango? HAKUNA!
2. Wote waliopaniki na kuhamaki hakuna hata mmoja anayejua ile harambee ilichangisha shilingi ngapi na hivyo kushindwa kujibu hoja ya mleta mada na kuishia kumwaga matusi.
3. Ni jambo la ajabu kwa harambee iliyotangazwa vila na watu kuchangia kwa njia za kidigitali jumla ya michago isiwekwe wazi na shukrani za dhati isitolewe mpaka sasa. Tafakari na chukua hatua..kama hesabu za kidigitali zinachukua muda mrefu hivi si hesabu za kura ukiwapa hawa watu itachukua miaka miwili?????
4. Fuatilia harambee na michango ya M4C ya Mpesa na Tigo pesa huwa haitangazwi. Kuna tuhuma tu za ndani kwa ndani kuwa wanene wanazipiga na kudai wamejikopesha au wamejilipa..
Vyovyote iwavyo michango ya wanachama inapaswa kutangazwa na kuwekwa wazi.
5. Lowassa ni bingwa wa harambee. Kazifanya nyingi na hata taasisi nyingi za kidini zimemtumia sana kwenye harambee. Matokeo ya harambee hutangazwa mara 1. Hakuna harambee ya Lowassa ambayo makusanyo hayajulikani.
Leo nashangaaa kaingia chadema, kafanya harambee ya kuuomba umma uchangie kampeni zake. Na maombi ya michango yametumia picha yake na yeye ndo alikuwa lengo mahususi la michango hiyo lakni hadi leo, hakuna jumla ya harambee iliyowekwa wazi kwa umma. Sijaona popote. Aliyeona atujuze tafadhali.
Harambee ya Lowassa imekuwa kama ile ya michango ya Mbowe.
6. Mleta mada anacheka kimoyo moyo kuwa waliochanga wamepigwa, tena wamepigwa kwa ule mlalo maarufu wa Lipumba ...yaani malalo wa mende.
Msinipige mawe, mimi sio mweka hazina wa harambee ya Lowassa.