UKAWA wabuni mbinu mpya ya urais 2015

UKAWA wabuni mbinu mpya ya urais 2015

Then wakipata madaraka ndio wakae kikao cha siri wapange wataongozaje? Au kikao kimeamua wataongozaje nchi kwa pamoja?

Majaribio ya formula au proven theory?
 
Kama Kenya Raila alivosema Kibaki Tosha pia hivo hivo Tanzania Lipumba akisema Slaa tosha au Slaa akisema Lipumba tosha. Mungu ibariki Tanzania.
 
Ukawa lazima wawe makini ikiwa ni pamoja na kuwapa elimu zaidi wanachama wao. Kuna baadhi ya Wanachama wa CUF wameapa kutoipa kula UKAWA endapa watasimamisha mgombea Urais Mkristo.
 
Ukawa lazima wawe makini ikiwa ni pamoja na kuwapa elimu zaidi wanachama wao. Kuna baadhi ya Wanachama wa CUF wameapa kutoipa kula UKAWA endapa watasimamisha mgombea Urais Mkristo.

Ni KWAMBA Ukawa wasikimbilie kusimamisha mgombea wa urais tu, mawazo yasiwe uko, kuna mambo mengi sana yanatakiwa kuangaliwa,
1.Kuna tuhuma za ukabila
2.Kuna tuhuma za udini
3.Kuna tuhuma za umamluki
4.Ugomvi
Wanatakiwa watoe elimu ya kutosha kwa wanachama wao na wasiowanachama wao ukweli wa hayo yote. Lakini pia wasichagua mtu kwa maana ya kushinda urais, bali wachague mtu ambaye atakuwa tayari kuwasaidia kupata viti vingi vya ubunge kiasi ambacho hata wasipopata urais watakuwa na sauti Bungeni, Tatizo lililopo sio urais ni Bungeni.
Watu wengi wako tayari kuisaidia UKAWA kutoa eleimu mijini na vijijini, na hii ianze mapema.
Lakini pia waondoe tofauti zilizopo na kujenga chama, watu kama Zitto, Kafulila hata Ahamad Rashid ni muhimu kuelekea uchaguzi.
 
Then wakipata madaraka ndio wakae kikao cha siri wapange wataongozaje? Au kikao kimeamua wataongozaje nchi kwa pamoja?

Majaribio ya formula au proven theory?

Mkuu namna ilivyo shughuli pevu kumpata mgombea urais kupitia tiketi ya CCM, na ndivyo ilivyo kwa UKAWA. Tatizo la kizazi cha sasa si kama kile cha Nyerere, ubinafsi umetujaa badala ya kutanguliza maslahi ya Taifa. Tusubiri tuone.
 
Ukawa lazima wawe makini ikiwa ni pamoja na kuwapa elimu zaidi wanachama wao. Kuna baadhi ya Wanachama wa CUF wameapa kutoipa kula UKAWA endapa watasimamisha mgombea Urais Mkristo.
Aaaaagh!!!!!! Fikra hizo zisipewe nafasi kabisa.
 
Teh Teh hapo kumchagua muwakilishi wa Urais kupitia UKAWA Lazima zichapwe Live


Nakwambia hakiamama mafisadi a.k.a ccm safari hii hamchomki hii ikiwaacha naenda kuomba uraia kwa jirani zetu!

pumbavu zao maccm!
 
Teh Teh hapo kumchagua muwakilishi wa Urais kupitia UKAWA Lazima zichapwe Live



Hivi Ruttashobolwa sijajuaga una akili fupi kiasi hichi

Kumbe bado Best unatumika kama kondom tu.........
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/793265-wana-ukawa-tunamhitaji-prof-lipumba-lasivyo-patachimbika.htmlhttps://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/793265-wana-ukawa-tunamhitaji-prof-lipumba-lasivyo-patachimbika.html
 
Last edited by a moderator:
Muungano wa vyama vya Chadema,CUF,NCCR na UMD kuelekea uchaguzi mkuu 2015 waweza kuwa neema kwao kama watakuwa wamejipanga au maafa makubwa kama hawatajipanga mapema kukabili changamoto ambazo watakutana nazo zingine zikiwa za asili na zingine zikiwa za KUTENGENEZWA na mahasimu wao wakubwa ambao ni chama wanachokusudia kukitoa madarakani.

Sasa hivi vipo vikao vya viongozi kupanga nini wafanye katika ushirika wao huo, sio vibaya ila mimi ningeshauri sasa ni wakati wakuunda timu kabambe ambayo sio ya viongozi pekee bali ikishirikisha wataalamu wengine wa siasa, Uchumi,Ushirikiano wa kimataifa na nyanja nyingine hata za kijasusi (nieleweke vizuri hapo) ili kuweza kupata ushauri wa jinsi ya kuendesha umoja huo vyema katika miono tofauti ya vyama vyao, kujua jinsi ya kupata support ya ndani na nje ya nchi na hta muundo gani utakuwa wa serikali kama watafanikiwa kushinda badala ya kusubiri majaliwa.

Timu hiyo sio lazima kuchaguana kutoka ndani ya vyama bali hata ajira zinaweza kutolewa kwa wale watakao chaguliwa kwa weledi wao ili walipwe kulingana na kazi zao watakazo fanya.

Kuitoa CCM madarakani kwa kusubiri vikao vya viongozi pekee na kutoa matamko sidhani kama itakuwa rahisi ni lazima wawepo watu wapanga mikakati 24/7 na hivyo vichwa viwe vichwa kweli ndio malengo yatatimia, vinginevyo November watu watarudi na malalamiko tuu na CCM kwao malalamiko ni wimbo mzuri wa kutafutia usingizi.

Nawasilisha.
 
Nakubali kwamba si rahisi mafahali kukaa zizi moja na UKAWA ni zizi la mafahali. Iwapo wataweza kukubaliana na kuwa nguvu moja linalohitaji mkakati ni namna ya kuzuia wizi wa kura. Kwangu hili la pili ni muhimu kuliko hata huo ukawa.
 
Nakubali kwamba si rahisi mafahali kukaa zizi moja na UKAWA ni zizi la mafahali. Iwapo wataweza kukubaliana na kuwa nguvu moja linalohitaji mkakati ni namna ya kuzuia wizi wa kura. Kwangu hili la pili ni muhimu kuliko hata huo ukawa.

Ni muhimu sana kuwa na timu ya wataalamu kuzungumzia jinsi ya kuendesha umoja wao kuliko kutegemea wanasiasa pekee. Kwanza hao ni rahisi sana kuvurugwa.
 
Hoja yako ina mantiku ndani yake ukiisoma kwa makini, kama viongozi wetu wanapenda ushauri basi huu pia ni wakufanyia kazi pasi na shaka kabisa
 
Ni muhimu sana kuwa na timu ya wataalamu kuzungumzia jinsi ya kuendesha umoja wao kuliko kutegemea wanasiasa pekee. Kwanza hao ni rahisi sana kuvurugwa.

Mfano mdogo ni katika kumpata mgombea, kwamba kila chama kitasimamisha mgombea then mkutano mkuu wa vyama vyote vipigie jina mmoja linalofaa au litakalowapendeza itakuwaje akipita mgombea ambae kwa wananchi kuuzika kwake hata ukimpaka mafuta ya kakakuona lakini haendi itakuaje? nadhani hii pia si njia nzuri bado hata mimi naungana nawe kuunda tume ya wataalamu kuangalia swala ili na mengine kwa ujumla,
 
Back
Top Bottom