lonyorengai
Member
- May 12, 2008
- 71
- 35
Imekuwa kero sasa hususan katika miji mikubwa kuona au kusikia zomea zomea kutoka kwa wapenzi, wanachama na mashabiki wa muungano UKAWA kwa wananchi wanaopita mitaani hali wamevaa nguo za CCM. Hili la kuzomea si sahihi kwa kuwa sio lazima wote tuwe wana UKAWA. Tuwasamehe na kuendelea kuwa wastaarabu kwa kuwa tunafanya kampeni za kistaarabu.Najua ni vigumu kuendelea kuona nguo za ccm au ccm yenyewe lakini mwisho wa yote tutaishi ndani ya Tanzania yetu tukiwa tofauti kiitikadi japokuwa ccm watakuwa wachache sana ama hakuna kabisa. Tuwaache na ubaya wao na maangamizo ndani ya mioyo yao kwa kukataa ukweli wa kukataliwa na wapenda mabadiliko. Suluba ya UKAWA inawatosha tusiwaumize zaidi.