UKAWA sisi ni Wenzenu: Rudini Bungeni

UKAWA sisi ni Wenzenu: Rudini Bungeni

Yawezekana hunijui...........ninachokwambia ni kwamba hata UKAWA Wasiporudi bungeni.........bunge litaendelea tu.
Ukawa wameshasema hawarudi, sasa kitu gani kinawazuia kuendelea.
Na ni bora ukawa wawepo wateteee maslahi mengine ya mtanzania na sio muundo wa muungano tuuu.
Muundo wa serikali ni paramount. Ndio itatupa dira ya wapi tunapotaka kufika.
Wote hakuna aliyejibu swali la msingi...umaskini wetu chanzo ni muungano?
Ndio, ubadhirifu mkubwa unafanyika kwa kivuli cha Muungano. Hakuna wa kuwajibika wala wa kuwajibishwa kwani yapo mambo hayana wenyewe.
Mie nilidhaniu una uelewa kidogo. Umaskini wetu ni muuundo wa muungano?
Okay, wewe mwenye uelewa mkubwa, nini chanzo cha umasikini wetu?
Hapo tu ndo akili yako imeenda left.
Hii ndiyo aina ya mipasho iliyosheheni ndani ya hilo Bunge. UKAWA cant be a party to this stupidity.
 
Katiba mpya ya Watanzania itapatikana kwa ridhaa yetu wananchi na si ukawa maana hatua ya mwisho rasimu hiyo italetwa kwetu kwa ajili ya kuipigia kura.

Kama mlielewa katiba italetwa kwenu kuridhiwa hata bila ukawa kushiriki kwanini mnaendelea kutafuta maridhiano na ukawa? Ni kama alivyojigamba Lukuvi kwenye mdahalo wa leo 3/8/'14 kuwa theluthi mbili za bara na visiwani wanazo na kwamba itapatikana katiba kasoro haitakuwa imeshiba sana kwa kukosekana ukawa bungeni.Ujue kupata theluthi mbili za zanzibar ni lazima wapatikane wajumbe 16 kati ya waliosusia bunge maalumu la katiba kutoka visiwani. Nani anaejua kilichokwisha fanyika hivyo kuwa na uhakika huo?Wengi tumemsikia Oluochi ambae nae ni mjumbe wa bunge hilo na muumini wa serikali tatu tena kwa kutumwa na waalimu anaowawakilisha. Katika kipindi kilichorushwa na star tv leo asubuhi tar.3/8 amesema ili bunge hilo liweze kuipitisha katiba hiyo lazima lifanye political porching kuwapata wabunge 16 kati ya waliosusia bunge hilo toka visiwani. Huenda hilo limeshafanyika na ndio maana wanadai bunge litaendelea na kazi yake tar.5/8 hata bila ukawa mbali na rai nyingi za kuliahirisha hadi baada ya uchaguzi mkuu ila kuvifanyia marekesho baadhi ya vifungu kwenye katiba iliyopo tuingie uchaguzi.Tumesikia toka ukawa kuna vifungu vilivyopitishwa na wote ila vimechakachuliwa baada ya wao kuondoka. Sasa endapo watarudi bungeni na kutaka virejeshwe kabla hawajaendelea na hatua yoyote huoni huo ni mvutano mwingine utakaopelekea kutoka tena bungeni? Wengi hawaelewi kuwa watakaporudi hiyo tar.5 wanaenda kupitisha sura ya kwanza na ya sita na sio kujadili tena ndio maana ukawa hawataki kuwa sehemu ya waliopitisha serikali mbili badala ya tatu zilizotakiwa na wananchi.Pia ieleweke kwenu kuwa sura zote 15 zilizobaki kujadiliwa zina mahusiano makubwa sana au zinazungumzia zaidi serikali tatu na sio mbili. Hofu ya ukawa wakishiriki tu watakuwa wamejimaliza wenyewe kwani itaonekana wameyakubali yote hata yale yaliyopitishwa wakiwa nje ya bunge.Busara na hekima itumike kuahirisha mchakato na uundwaji wa bunge la katiba ufanyiwe marekebisho kwa upunguza idadi ya wabunge na nafasi zao zichukuliwe na wananchi.
 
lee jibu swali walau...................main argument ya ukawa ni Muundo wa Muungano.....nakuuliza tena umaskini wetu ni Sababu ya Muundo wa Muungano?

Ta Muga sina uhakika kama main argument ya UKAWA ni muundo wa muungano pekeekwa sababu muundo wa muungano ndio ilikua sehemu ya kwanza au aya ya kwanza kujadiliwa katika rasimu nzima iliyopendekezwa na wananchi kupitia tume ya Warioba.UKAWA waliona kuwa wengi (CCM) Bungeni hawaijadili kama ilivyo na kwenda kinyume na maoni ya wananchi ambao ndio wanaunda nchi na ambao ndio wanapenda watawaliwe vipi, ndipo UKAWA wakaonani kinyume na matakwa ya wenye nchi yaani wananchi. na kuamua kutorudi bungeni.hilo lilikua ni kubwa .Ila mambo madogomamdogo ambayo yanapandisha hasira na huenda yanaweza yakasababbisaha mpasuko mkubwa na pengine kuisambaratisha nchi ni lugha za dharau,kejeli matusi,na za kibaguzi.hili hasa lilielekezwa zaidi kwa wapinzani hususani kwa Wapemba.( unafahamu zilianzaje conflicts za wahutu na watusi ,sudani kusini na sudani kaskazini n.k) .Hata hivyo mkuu Ta Muga inawezekana pengine kama UKAWA wangekubali hilo la muundo wa muungano lipite kama wajumbe wengi kwa maaana ya kubali yaishe, pengine wangeweza kuja kutokubaliana kwa mambo mengine ambayo hayakuwa yamefikiwa katika majadiliano,kwa sababu hayajafikiwa ndio maana nimesema sina uhakika kwa kuwa mjadala wa BMK ulikua ndio kwanza umeanza.Swali lako la pili je umasikini wetu ni sababu ya muundo wa muungano,nakujibu hivi.Muundo wa muungano ni moja kati ya matatizo yanayowakabili watanzania.Kwangu mimi Tanzania ina matatizo ya kisiasa na matatizo ya kiuchumi. matatizo ya kisiasa yanasumbua sana viongozi na matatizo ya kiuchumi yanasumbua sana wananchi. Sasa kwa sababu kuna fursa ya kuya solv yote kwa pamoja ni bora yakawa solved kwa pamoja.Manung'uniko ya muungano ni makubwa mno kuliko unavyofikiria,ni heri tutengane kwa amani kuliko kutengana baada ya kupigana.ZNZ imeomba sarafu yake,bendera yake,wimbo wa taifa wake,benki yake,itambulike nje ki vyake,n.k.ZNZ ikipewa hivyo vyote kuna MUUNGANO HAPO? naomba na mimi nikuulize vijiswali; kwa nini CCM au wengi bungeni hawataki swala la muundo wa muungano lijadiliwe au liguswe? au kwa nini hawataki serikari tatu? na je kwa nini swala la muundo wa muungano hasa wa serikali tatu litokee kila tume? TUME za Nyalali,Kisanga,na sasa Warioba? hizo tume mbili za mwanzo UKAWA hawakuwepo.
 
Back
Top Bottom