UKAWA o muerte, Cuban Motto

UKAWA o muerte, Cuban Motto

Sikonge

JF-Expert Member
Joined
Jan 19, 2008
Posts
11,633
Reaction score
6,229
Nchi nyingi za Kilatino wamekuwa na aina nyingi za Slogan au Motto ambazo huzitumia ili kuwahamasisha Makamanda wao popote inapotokea wanapigania haki zao.

Wa-Cuba na wengine kadhaa wana msemo wao walioutumia miaka hizo wanapigania uhuru "Patria o Muerte, Venceremos" ambayo maana yake ni "Homeland or Death, We shall overcome".

Yes, ni Tanzania au KIFO, tutashinda. Huo ndiyo ukweli wenyewe ambao unatakiwa kusemwa waziwazi.

Kama kuna watu watakuja na kila aina ya vitisho, basi wajue kuwa mwisho wa siku, mshindi atakuwa Mtanzania.

Wengi walishajaribu kupigana na Wananchi wao na wakashindwa vibaya sana.

Kwa sasa hivi, mtetezi anayeweza kumuondoa MKOLONI mweusi ni UKAWA peke yake.

Msitutishe Wananchi kwa maneno ya Mbowe atajiunga CCM, Lipumba amehamia Rwanda, sijui nani kafanya kile au hiki.

Hatujali sana nani kajiunga au kajitoa UKAWA. Sisi jibu ni moja tu, UKAWA ndiyo chombo cha kumuondoa Mkoloni mweusi anayetawala Tanzania kwa miaka zaidi ya 50 huku akijimilikisha haki miliki ya nchi hii kwa vitisho vya MTAKIONA CHA MTEMA KUNI na vingine vingi huku wengine wakijeruhiwa vibaya kama Ulimboka na wengine wakipoteza maisha kama Mwangosi. Hawa wote damu yao haitamwagika bure. Kuna siku mtu atalipa.

Kwa wale wote wanaobeza Ukawa sisi tuna Motto moja tu kwa leo:

UKAWA O MUERTE ---- UKAWA AU KIFO ---- UKAWA OR DEATH.
 
Hali ilipofika sasa hivi hakuna wakuirudisha nyuma....

Hakuna dola iliyowahi kushinda umma.... dhulma....chuki....husda vina mwisho!!!!

Kwa tulipofika hata viongozi wote wa Mageuzi wakitusaliti tutasonga mbele mpaka mwisho....

Wapo waliodhani baadhi ya viongozi wa upinzani wakijitoa pengine vuguvugu litadorora kumbe moto ndo umetiwa petroli....

Upepo ni mkali utazoa kila kitu!!!
 
Sikonge mada zingine uwe unasubiri tufike home. Hapa umenitia hasara, tuko kama wanane hivi na wengine wanapiga Heinkein na baada ya kusoma post yako imebidi Nipige round mbili za haraka na kuna uwezekano zikaongezeka kwa hamasa ya post yako.
Aah haya bwana, ila nikiondoka sina kitu mfukoni nitaoendekeza upigwe ban kila siku jioni.
Kula like
 
Last edited by a moderator:
Sikonge mada zingine uwe unasubiri tufike home. Hapa umenitia hasara, tuko kama wanane hivi na wengine wanapiga Heinkein na baada ya kusoma post yako imebidi Nipige round mbili za haraka na kuna uwezekano zikaongezeka kwa hamasa ya post yako.
Aah haya bwana, ila nikiondoka sina kitu mfukoni nitaoendekeza upigwe ban kila siku jioni.
Kula like
Angalia sana! Pombe ni mbaya. Tunaikataa kabisa isitutawale hata kama inapigiwa debe na wakubwa. Kataa kutawaliwa na Pombe kabisa. Ukishindwa funga huo mdomo wako kwa Makufuli ili isikutawale! Haya shauri yako!!

 
Angalia sana! Pombe ni mbaya. Tunaikataa kabisa isitutawale hata kama inapigiwa debe na wakubwa. Kataa kutawaliwa na Pombe kabisa. Ukishindwa funga huo mdomo wako kwa Makufuli ili isikutawale! Haya shauri yako!!

kuna tofauti ya pombe ya kinywaji upo hapo! Wewe unasikia serikali haina hela na imewekeza mapato kwenye kinywaji kwa kukosa ubunifu unataka watu wasinywe ili waalimu wakose mishahara?
 
Mkuu Chakaza , taratibu tuwaeleweshe Wananchi wa Tanzania kuhusu umuhimu wa kupiga kura na wajuwe nani wampigie kura maana Mkoloni mweusi sasa hashikiki kwa kudhani nchi ya Tanzania ni mali ya familia.

Inafika wakati wanatuamulia ni nani sasa awe Rais, nani awe vile......

Nashukuru Mungu wametibuana na sasa ndiyo nimekuja kufahamu jinsi ilivyokuwa ngumu kuwaondoa.

Nyerere alishaona MIZIZI aliyootosha na akawa na uhakika kabisa, hakuna upinzani utawaondoa CCM. Kama kutakuwa na nguvu ya kuwaondoa CCM madarakani basi itatoka ndani ya CCM. Alijua mengi sana Mzee yule na hakukosea. Ila kuna upande inanisikisha kwani kwa kukandamiza upinzani, yeye pia amechangia kwa kiasi kikubwa manyanyaso yanayoendelea nchi kwetu na kibaya zaidi hata kupelekea kifo chake (kumbuka maneno ya Vincent Nyerere kwa Mkapa).

Mungu Ibariki Tanzania: UKAWA O MUERTE ---- UKAWA AU KIFO ---- UKAWA OR DEATH.

Sikonge mada zingine uwe unasubiri tufike home. Hapa umenitia hasara, tuko kama wanane hivi na wengine wanapiga Heinkein na baada ya kusoma post yako imebidi Nipige round mbili za haraka na kuna uwezekano zikaongezeka kwa hamasa ya post yako.
Aah haya bwana, ila nikiondoka sina kitu mfukoni nitaoendekeza upigwe ban kila siku jioni.
Kula like
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom