Dumbuya
JF-Expert Member
- Jan 23, 2014
- 596
- 881
Salaam wanaJF,
Nimekuwa nikifuatilia kwa karibu mchakato kuelekea uchaguzi na pamoja nakuunga mkono juhudi nyingi za upinzani kupitia Ukawa na Chadema kuna baadhi ya vitu ambavyo nimekuwa nikishangaa kwa nini havifuatiliwi.
Kuna kauli ambazo Chama Cha Mapinduzi imekuwa ikizitoa kupitia kwa viongozi wake hasa Katibu Uenezi na Itikadi Nape Nnauye.Kauli ya 'Goli la Mkono' ikiwa kubwa na nyingine nyingi ikiwemo ya Mwenyekiti wao pia akisema wana 'ujuzi,maarifa na uzoefu' wa kushinda uchaguzi hivyo ni lazima washinde ikifika oktoba.Sasa nimekuwa nikijiuliza wakati CCM ikitumia propaganda na kauli za kibabe kama hizi ofisi ya uenezi Chadema ipo wapi??
Ni nani anahusika na propaganda huku Chadema na Ukawa??Pamoja na kubishana kwa hoja na Sera napenda kuwakumbusha viongozi wa Ukawa kuwa bado kuna kundi kubwa la watanzania ambao hawana uelewa thabiti hasa wa vijijini hivyo huishia kuamini na kushabikia propaganda hizi za CCm.
Yaani maneno ya kuwa Lowassa fisadi na Chadema imenunuliwa na hela ya Richmond na mengine mengi yanahitaji ofisi madhubuti ya propaganda kuzijibu na siyo hotuba tu.Nasema tena Hoja na Sera hazisikilizwi na wote na huu umekuwa ukweli ambao CCm imekuwa ikiutumia kubaki madarakani.
Tunataka kuwepo hiki kitengo..yaani wakisema Chadema Richmond na nyie mjibu mbona Raisi na mwenyekiti wenu alimnyanyua mkono 2010 na kumpigia debe kuwa msafi??mbona kinana alifanya hivyo pia??kwa hiyo walikuwa wanatudanganya,wanafiki au akiwa CCm ndo msafi??
Mbona alikuwepo miaka 8 hajaguswa??yaani haya mambo yasipojibiwa Ukawa na Chadema watafungwa magoli hata kabla ya mechi kuanza..tena hat trick kabisaa.
Kukaa kimya kwa kitengo/ofisi hii kutaigharimu sana Ukawa na Chadema..
Itikadi na Uenezi/Propaganda Ukawa na Chadema amkenii..Hamtashinda kwa hoja na Sera tu au kurundika wajumbe na mabango,watanzania wengi wanakuwa brainwashed na propaganda za CCm huku mitaani.Tumieni ujuzi wenu wa hizo digrii za political science basi..
Asahnteni.
Nimekuwa nikifuatilia kwa karibu mchakato kuelekea uchaguzi na pamoja nakuunga mkono juhudi nyingi za upinzani kupitia Ukawa na Chadema kuna baadhi ya vitu ambavyo nimekuwa nikishangaa kwa nini havifuatiliwi.
Kuna kauli ambazo Chama Cha Mapinduzi imekuwa ikizitoa kupitia kwa viongozi wake hasa Katibu Uenezi na Itikadi Nape Nnauye.Kauli ya 'Goli la Mkono' ikiwa kubwa na nyingine nyingi ikiwemo ya Mwenyekiti wao pia akisema wana 'ujuzi,maarifa na uzoefu' wa kushinda uchaguzi hivyo ni lazima washinde ikifika oktoba.Sasa nimekuwa nikijiuliza wakati CCM ikitumia propaganda na kauli za kibabe kama hizi ofisi ya uenezi Chadema ipo wapi??
Ni nani anahusika na propaganda huku Chadema na Ukawa??Pamoja na kubishana kwa hoja na Sera napenda kuwakumbusha viongozi wa Ukawa kuwa bado kuna kundi kubwa la watanzania ambao hawana uelewa thabiti hasa wa vijijini hivyo huishia kuamini na kushabikia propaganda hizi za CCm.
Yaani maneno ya kuwa Lowassa fisadi na Chadema imenunuliwa na hela ya Richmond na mengine mengi yanahitaji ofisi madhubuti ya propaganda kuzijibu na siyo hotuba tu.Nasema tena Hoja na Sera hazisikilizwi na wote na huu umekuwa ukweli ambao CCm imekuwa ikiutumia kubaki madarakani.
Tunataka kuwepo hiki kitengo..yaani wakisema Chadema Richmond na nyie mjibu mbona Raisi na mwenyekiti wenu alimnyanyua mkono 2010 na kumpigia debe kuwa msafi??mbona kinana alifanya hivyo pia??kwa hiyo walikuwa wanatudanganya,wanafiki au akiwa CCm ndo msafi??
Mbona alikuwepo miaka 8 hajaguswa??yaani haya mambo yasipojibiwa Ukawa na Chadema watafungwa magoli hata kabla ya mechi kuanza..tena hat trick kabisaa.
Kukaa kimya kwa kitengo/ofisi hii kutaigharimu sana Ukawa na Chadema..
Itikadi na Uenezi/Propaganda Ukawa na Chadema amkenii..Hamtashinda kwa hoja na Sera tu au kurundika wajumbe na mabango,watanzania wengi wanakuwa brainwashed na propaganda za CCm huku mitaani.Tumieni ujuzi wenu wa hizo digrii za political science basi..
Asahnteni.