UKAWA kusambaratika Kesho

UKAWA kusambaratika Kesho

sem2708

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2010
Posts
5,817
Reaction score
4,965
Ndugu zangu wana JF, hatimaye nyundo ya kuwasambaratisha UKAWA imechongwa. Nayo ni kuingiza suala la KADHI kwenye katiba mpya. Ukawa mlikuwa na plan B? Kazi kwenu
 
CCM wanafanya hayo ili waungwe mkono, ila matokeo yake ni hatari sana sana
 
Suala hili halitasambaratisha Ukawa tu bali Taifa zima litagawanyika vipandevipande, hapo kuna wakristo upande mmoja na waislamu upande wa pili, pia wako wasio na dini. Hapo hakuna ccm wala ukawa. Jk mpaka kufikia mwakani atakuwa amelijeruhi vibaya sana taifa hili.
 
Wakiweka mahakama yakiislamu tutaweka mahakama yawakristo. Muislam akinishtaki msikitini mimi nitasubiri kuhukumiwa kanisani hataniona msikitini ng'o.
 
Ingawaje kwa Ccm lolote lawezekana ili mradi mkono kinywani.HAtari kubwa sana tena Hatari kuuuuuuuuuuuuubwa na maaafa
 
ccm sio wajinga kiasi hicho coz wanajua hii ishu ya mahakama ya kadhi itawaharibia hata wao
 
Safi jk, drshen, dr ghari, mbembe, jonimaleche, rasisi hili ndo tulikuwa tubalitaka. Kama muingereza anamkata shingo mmarekani huko irak kwa nini six asiharibu kwa vile anaona naye kakosa
 
Suala la udini ktk katiba haliwez kusambaratisha UKAWA ila litavuruga amani.. Maana ktk vita ya udini hakunaga mshindi wala mbabe
 
Kardinal Pengo toa tamko mapema baba kabla mambo hayajaenda mbele zaidi!
 
Ndugu zangu wana jf, hatimaye nyundo ya kuwasambaratisha UKAWA imechongwa.nayo ni kuingiza suala la KADHI kwenye katiba mpya. Ukawa mlikuwa na plan b? Kazi kwenu

Kwa hiyo wakristo na waislamu hawamo kwenye bunge la sasa?
 
Mbona uzi haujitoshelezi,hii ni hoja very sensitive,lakini inaletwa bila maelezo ya kina,aieleweki kama kuna ukweli nndani yake au ni porojo za kwenye vijiwe vya pweza.
Fafanua zaidi.
 
Back
Top Bottom