kuna watu wamewekwa na kambi zote humu wanalipwa pesa kwa ajili hiyo, hata usiumize kichwa zana!
Ndio maana mi nilikua sielewi kiukweli
Mfano kuna mtu anasema ukawa hawajielewi na wameshawafahamu kwa upuuzi wao. Ni sawa kabisaa na ukawa wanasema tutawashikisha adabu,
Swali je! Utamshikisha adabu ukiwa nje?
Haya kambi ya ccm nayo haioni jinsi wabunge wa CCM wanavyotunyima raha wanainchi wameligeuza bunge kama kikao cha kitchen party, kama imefikia hatua mtu anachangia kwa kutaja ratiba ya familia yaje na kujipongeza kupata mtoto na jina atakalompa, hilo balo watu wanashangilia na kupiga makofi anashindwa jua kua wanainchi wao wakoje?? Mtu wa CCM atakwambia tunawakomesha UKAWA
Hizi kambi mbili zimetukosesha uelekeo kiukweli japo kila pande inasema nyingibe haijiewi na wanainchi huku wanadai hawaelewi sio CCM sio UKAWA.
Kwa mwendo huu taifa leti maendeleo yake yatabaki majukwaani na kwenye dayare za wagombea.
Mtugawe wakayi wa kampeni sasa mnatugawa mpaka nyakati za utendaji??
Hapa tunahitaji maombi ya pande zote tatu kwa waislam, wakristo na wapagani.
Kama kutipoteza kwa maslahi yenu kiukweli mmefanikiwa, lakini naamini machozi yetu Mungu anayaona na mtayalipa mwisho wa siku.
Wewe unayejiita mwana UKAWA unaishiia kuutetea ukawa wako ukasahau mawazo na matatizo ya wanainchi yaliyoshindwa kutekelezeka kwa wawakilishi wao kutoyawakilisha na wewe unatetea kwa maslahi yako ki ukweli hiyo dhambi itakutafuna wewe na vizazi vyako.
Wewe unayejiita mwana CCM unayetetea kila upuuzi pale unapoambiwa na aliyekulushia kifurushi cha internet ukakubali kuuficha ukweli wa mamilioni ya watanzania na kuamua kuunga mkono kila wazo ili mradi tu kalito mwana ccm yako, walahi nakuapia machozi ya wanyonge wanaishi hata kwa chini ya mlo mmoja yatakutafuna na utayalipa.
Kwa nyoote mliovibarua vya ukawa na ccm mjue mmesomeshwa na wazazi wenu wengi historia zenu mnazifahamu wenyewe ili mzikwamue familia zenu na kutengeneza taifa bora kwa kutumia ujuzi wenu kulijenga taifa kwa nguvu na akili mlizopewa, sasa mnazitumia akili na ujuzi wenu kwa kutetea vyama vyenu mnachangia kuligawa taifa lenye umoja kwa vyama vyenu walahi tukibaki nyuma kimaendeleo kwa Mungu mtawajibika
OMBI
Kwa wale ambao hatupo kambi yoyote tunaogemea kwenye ukweli, tuzidi kulipgania taifa hili mi naamini ipo siku tutafika mbali kuliko kukalia majungu