UKAWA Hatarini kupoteza jimbo la Namtumbo

UKAWA Hatarini kupoteza jimbo la Namtumbo

Patriote

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2011
Posts
1,718
Reaction score
1,047
Napenda kutumia fursa hii kuwataarifu wapenda mabadiliko kuwa Jimbo LA Namtumbo lipo hatarini kupotea hivyo msaada Wa haraka unahitajika ili kuokoa jimbo lisipotee. UKAWA iliwapa jimbo hili CUF ila mtandao wa cuf ni mdogo na mgombea wao hakubaliki Kwa wapiga kura walio wengi.

Mgombea Ubunge wa CUF hakuwahi kufanya siasa katika jimbo hili hivyo inamuwia vigumu kupokelewa na wapiga kura wakati huu Wa kuomba kura. Hali ya sintofaham ilitokea Jana katika Kata ya Lusewa na Msisima ambapo mgombea huyo alifukuzwa na wapigakura wakisema wao hawamtambua wanamtambua mgombea wa Chadema Wa udiwani na Ubunge.

Tuwakumbushe viongozi Wa UKAWA kuwa kura ni hiari ya MTU. Huwezi lazimisha mtu atoe kura Kwa mgombea asiyemtaka. Kuendelea kulazimisha wananchi wamchague mmgombea wasiyemkubali ni kutafuta kupoteza kura za madiwani na za rais wetu NA hatimaye kuhatarisha ushindi wetu Kama UKAWA.

Nionavyo Mimi Kama ni lazma huyu mgombea awe mbunge basi mpeni Ubunge Wa kuteuliwa. Huu Ubunge Wa kugombea ni lazma MTU aaminike NA kukubalika katika jamii ya wapiga kura.

Kuendelea kupingana NA maamuzi ya wapiga kura ni dalili kuwa mgombea Wa cuf na cuf huku Namtumbo wapo Kwa ajili ya maslahi binafsi na sio maslah ya wapiga kura ambao mgombea Ubunge anataka kuwapigania. Kama kwel UKAWA na mgombea Ubunge Wa Cuf wanawapenda wananchi Wa Namtumbo na wanataka wasiwe chini ya Ccm basi kubalini hamuwezi kuzuia mafuriko Kwa mikono. Mpeni nafasi hiyo mgombea anaye kubalika na wananchi walio wengi ili tushinde. Mgombea asiyekubalika hawezi kumwombea kura Diwani wala rais.

Wanajamvi mlio karibu na viongoz wa ukawa Tunaomba mtusaidie kufikisha ujumbe huu Kwa wahusika.
 
Naona mmeanza kuingia hadi kwenye ngome za cuf na kuanza kuaponda majimbo yote ya kusi nn i cuf wana nguvu kuliko cdm ww unakuja na hadisi za v kinafki hapa
 
Naona mmeanza kuingia hadi kwenye ngome za cuf na kuanza kuaponda majimbo yote ya kusi nn i cuf wana nguvu kuliko cdm ww unakuja na hadisi za v kinafki hapa
Wewe msisiem unaweza kuitakia mema UKAWA?? Mimi nimeongelea Namtumbo wewe unaongelea majimbo yote ya Kusini. Hapa nasemea specifically jimbo la Namtumbo. Lakini umefanya analysis yoyote Juu ya mtandao Wa Cuf vs Wa Chadema huku Namtumbo? Kama hujafanya utafiti huna haki ya kuzungumza. Haya tunakueleza wapiga kura Wa Namtumbo achana NA story za kwenye Magazeti.
 
hayo ni yenu watu hawako huko watu wanachotaka ni mabadiliko na mabadiliko ni ya chama mabadiliko sio watu wewe kama unadhani mabadiliko ni ni watu umepitwa na wakati mabadiliko ya watu ni ya ccm ila mabadiliko ya chama ndio watu wanayoyazungumzia ndio maana Lowasa amehama chama
 
hayo ni yenu watu hawako huko watu wanachotaka ni mabadiliko na mabadiliko ni ya chama mabadiliko sio watu wewe kama unadhani mabadiliko ni ni watu umepitwa na wakati mabadiliko ya watu ni ya ccm ila mabadiliko ya chama ndio watu wanayoyazungumzia ndio maana Lowasa amehama chama
Nahisi sijakuelewa. Ila ombi letu huku sio tubishane na nyie au mtutukane. Huku tunahitaji msaada ujumbe huu muufikishe Kwa viongoz Wa UKAWA mjini huko.
 
Huyu jamaa ana hoja, ila kwakuwa watu wamechanganyikiwa hawataki kusikiliza hata ushauri. Hapo kama ni lazima mgombea awe mbunge inabidi support kubwa itolewe
 
Nahisi sijakuelewa. Ila ombi letu huku sio tubishane na nyie au mtutukane. Huku tunahitaji msaada ujumbe huu muufikishe Kwa viongoz Wa UKAWA mjini huko.

Kulikuwa na makubaliano ya kuachiana majimbo, na hilo jimbo walipewa cuf sasa kama hawana nguvu ni juu yenu kuwapa nguvu, ndio maana ya ushirikiano. Mnachotaka kufanya ni ubinafsi na uasi. Inatakiwa vyama vyote ndani ya ukawa vi-support mgombea aliyewekwa kwenye jimbo husika...
 
Ni kweli dada Zamda wa cdm ndie anaekubalika Namtumbo kubali kataa
 
Kulikuwa na makubaliano ya kuachiana majimbo, na hilo jimbo walipewa cuf sasa kama hawana nguvu ni juu yenu kuwapa nguvu, ndio maana ya ushirikiano. Mnachotaka kufanya ni ubinafsi na uasi. Inatakiwa vyama vyote ndani ya ukawa vi-support mgombea aliyewekwa kwenye jimbo husika...
Mgombea hatakiwi kuwekwa, anatakiwa aevolve toka miongoni mwa wapiga kura. Kilichopo hapa Namtumbo ni kuwa mgombea ameletwa kutoka Juu na ndio maana kuna shida kwenye kukubalika kwake. Mambo ya kuletewa mgombea yamepitwa na wakati na ndio yaliyowagharimu Ccm NA sisi tunafanya hayohayo.kama Mfumo Wa maridhiano wa UKAWA na vigezo tulivyokubaliana ndan ya UKAWA vingeheshimiwa naamini hakuna jimbo ambalo lingekuwa na mgogoro. Kwa vigezo vya ukawa Namtumbo ilipawa iende chadema na maamuzi ya nani agombee yalipaswa kuhusisha wanachi au vyama vilivyounda UKAWA Kwa pamoja.




Tatizo katika baadhi ya maeneo ikiwemo Namtumbo na msasasi maslah binafsi ya m mgombea na chama badala ya wananchi yamewekwa mbele kitu ambacho si sahihi NA nikuwapuuza wananchi.
 
Mgombea hatakiwi kuwekwa, anatakiwa aevolve toka miongoni mwa wapiga kura. Kilichopo hapa Namtumbo ni kuwa mgombea ameletwa kutoka Juu na ndio maana kuna shida kwenye kukubalika kwake. Mambo ya kuletewa mgombea yamepitwa na wakati na ndio yaliyowagharimu Ccm NA sisi tunafanya hayohayo.kama Mfumo Wa maridhiano wa UKAWA na vigezo tulivyokubaliana ndan ya UKAWA vingeheshimiwa naamini hakuna jimbo ambalo lingekuwa na mgogoro. Kwa vigezo vya ukawa Namtumbo ilipawa iende chadema na maamuzi ya nani agombee yalipaswa kuhusisha wanachi au vyama vilivyounda UKAWA Kwa pamoja.

Tatizo katika baadhi ya maeneo ikiwemo Namtumbo na msasasi maslah binafsi ya m mgombea na chama badala ya wananchi yamewekwa mbele kitu ambacho si sahihi NA nikuwapuuza wananchi.

Kwa hiyo Ukawa hamheshimiani?
 
Back
Top Bottom