UKAWA bado hawajaidhinisha Lowassa na Duni kama wagombea

UKAWA bado hawajaidhinisha Lowassa na Duni kama wagombea

East African Eagle

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2013
Posts
3,759
Reaction score
2,209
Kikao pekee kilichompitisha mgombea uraisi ni Mkutano mkuu wa CHADEMA ulikofanyika Mlimani CITY.Baada ya kumpitisha mkutano mkuu hatua ya pili ilitakiwa Jina la Lowassa lipelekwe kwenye kikao cha UKAWA .

Baada ya kikao cha viongozi wa UKAWA kukaana kujadili na kumptisha Lowasa kuwa ndie mgombea wa UKAWA ndipo UKAWA wangempa kibali Lowassa kupendekeza jina la mgombea mwenza kutoka vyama vinavyounda UKAWA.

Hapo angepeleka maombi kwa chama husika kimruhusu mtu anayempendekeza agombee kama mgombea mwenza.

Chama anakoomba kingeitisha kikao halali cha kujadili ombi hilo na kutoa ruksa kama huyo aliyeombwa abadili chama kwa ruksa ya kikao halali cha chama.

Baada ya hapo Chama husika kingetoa ruksa ya kuhama na kuwajulisha washirika wa UKAWA kwamba kimeridhia kama chama.

Hapo CHADEMA wangetoa kadi kwa mhusika na kuitisha tena mkutano mkuu wa kuridhia uteuzi wa huyo mtu ndani ya CHADEMA

Lakini ule mkutano mkuu wa CHADEMA ukafanya yote,Ukajifanya mkutano mkuu wa CHADEMA na mkutano mkuu wa UKAWA na tawi la kugawa kadi kwa wanachama wapya na kuwatangaza wagombea wenza!

Seif sharif Hamad akakubali kitu kisichokuwepo kiutaratibu ndani ya CUF na kusema anashukuru lowasa kama raisi mgombea na mgombea mwenza kuwa duni haji akageuza mkutano mkuu wa CHADEMA kuwa mkutano mkuu wa UKAWA na Mkutano wa baraza kuu la CUF!!!!!! bila agenda wala chochote.

Kiutaratibu Lowassa bado hajaidhinishwa na mkutano wa Viongozi wa UKAWA kile kilichofanyika mlimani CIty ULIKUWA mkutano mkuu wa CHADEMA sio MKUTANO mkuu wa UKAWA.

Hivyo UKAWA bado hawajapata mgombea Urais na mgombea mwenza hadi pale kikao cha UKAWA. kitakapofanyika.
 
Usiombe maneno haya yakamfikia Askofu Gwajima, sasa hivi utakwambia umevimbiwa marahage na unabwabwaja hovyo.

Naomba uelewe yafuatayo:-
1. Hakuna chama cha siasa kinachohitwa UKAWA
2. UKAWA haina mkutano mkuu au barazaila ni viongozi wa vyama vya CUF, CHADEMA, NCCR - Mageuzi na NLD ambao viongozi wao walikuwepo au kutuma wawakilishi.
3. Mgombea wa urais anatoka CDM na UKAWA wanaunga mkono, hivyo kutano mkuu wa CDM kisheria ndo unaendorse mgombea.
4. CUF hawakuweka mgombea hivyo wameridhia chaguo la CDM.

Hivyo CDM ndio wenye kazi ya kufuata taratibu za vikao kitu ambacho wamefanya.

usiropoke siku nyingine.
 
Usiombe maneno haya yakamfikia Askofu Gwajima, sasa hivi utakwambia umevimbiwa marahage na unabwabwaja hovyo.

Naomba uelewe yafuatayo:-
1. Hakuna chama cha siasa kinachohitwa UKAWA
2. UKAWA haina mkutano mkuu au barazaila ni viongozi wa vyama vya CUF, CHADEMA, NCCR - Mageuzi na NLD ambao viongozi wao walikuwepo au kutuma wawakilishi.
3. Mgombea wa urais anatoka CDM na UKAWA wanaunga mkono, hivyo kutano mkuu wa CDM kisheria ndo unaendorse mgombea.
4. CUF hawakuweka mgombea hivyo wameridhia chaguo la CDM.

Hivyo CDM ndio wenye kazi ya kufuata taratibu za vikao kitu ambacho wamefanya.

usiropoke siku nyingine.

Sio kweli Eng...... nadhani hujamuelewa mleta tread, soma vizuri uelewe
 
UKAWA haina mkutano mkuu au barazaila ni viongozi wa vyama vya CUF, CHADEMA, NCCR - Mageuzi na NLD ambao viongozi wao walikuwepo au kutuma wawakilishi.

UKAWA wana wana vyama ambavyo mikutano mikuu yao lazima iridhie kabla ya wao kutangaza chochote.Lowasa kateuliwa na CHADEMA jina lake ilibidi lipelekwe mikutano mikuu ya vyama husika kwa ajili ya kuridhia.Mikutano hiyo mikuu ndio ingewapa Ruksa hao viongozi kuwa na sauti ya kusema CUF,NLD,au NCCR imeridhia!!!! na MGOMBEA mwenza vivyo hivyo!! ilibidi jina lake likajadiliwe baraza kuu la CUF lipate baraka na kuruhusiwa na baadaye lipate baraka toka vikao halali vya vyama vinavyounda UKAWA!!!
 
Wewe kweli mbulula toka lini UKAWA wanapokea maagizo yako?
 
Usiombe maneno haya yakamfikia Askofu Gwajima, sasa hivi utakwambia umevimbiwa marahage na unabwabwaja hovyo.

Naomba uelewe yafuatayo:-
1. Hakuna chama cha siasa kinachohitwa UKAWA
2. UKAWA haina mkutano mkuu au barazaila ni viongozi wa vyama vya CUF, CHADEMA, NCCR - Mageuzi na NLD ambao viongozi wao walikuwepo au kutuma wawakilishi.
3. Mgombea wa urais anatoka CDM na UKAWA wanaunga mkono, hivyo kutano mkuu wa CDM kisheria ndo unaendorse mgombea.
4. CUF hawakuweka mgombea hivyo wameridhia chaguo la CDM.

Hivyo CDM ndio wenye kazi ya kufuata taratibu za vikao kitu ambacho wamefanya.

usiropoke siku nyingine.

Umesema kweli, yaani kitendo cha babu Duni kuachia vyeo vyake na kuchukua kadi ya CHADEMA mbele ya Seif na wenyeviti wenza wa UKAWA haitoshi kujua hayo ndio makubaliano yao?, CDM imetoa rais na CUF itoe mwenza.

Kama kuna mtu anasubiri vyombo vya ukawa vikae atasubiri sana maana haitatokea.
 
Maalim Seif ni Mpemba, itakuwa kisha lamba zake. Cheza na fedha wewe.
 
Usiombe maneno haya yakamfikia Askofu Gwajima, sasa hivi utakwambia umevimbiwa marahage na unabwabwaja hovyo.

Naomba uelewe yafuatayo:-
1. Hakuna chama cha siasa kinachohitwa UKAWA
2. UKAWA haina mkutano mkuu au barazaila ni viongozi wa vyama vya CUF, CHADEMA, NCCR - Mageuzi na NLD ambao viongozi wao walikuwepo au kutuma wawakilishi.
3. Mgombea wa urais anatoka CDM na UKAWA wanaunga mkono, hivyo kutano mkuu wa CDM kisheria ndo unaendorse mgombea.
4. CUF hawakuweka mgombea hivyo wameridhia chaguo la CDM.

Hivyo CDM ndio wenye kazi ya kufuata taratibu za vikao kitu ambacho wamefanya.

usiropoke siku nyingine.

Mods majibu kama haya yakishatolewa kwenye uzi wa kipuuzi kama huu muwe unaufutilia mbali kwa matumizi sahihi ya server.
 
Kwani suala la Lowassa kugombea urais kwa tiketi ya CHADEMA si lilianza na makubaliano ya UKAWA kwanza, mara baada ya viongozi wa UKAWA kukubali Lowassa awe mgombea wa urais ndio taratibu nyingine zikaendelea, kwa hiyo hicho kinachofanyika ndo utatibu.
 
HAYA BASI NAMUIDHINISHA MIMI HAPA

LOWASA NDIYE MGOMBEA WETU UKAWA NA DUNI NDIYE MGOMBEA MWENZA

Kwa taarifa tu, hata UKAWA ikiidhinisha jiwe kugombea uraisi, wanayo kura yangu!!! THIS IS HOW FED UP I AM WITH NYINYIEMU
 
hayo ni mawazo yako....hakuna chama kinachoitwa UKAWA..na Mzee Duni Haji alihamia CDM kutoka CUF na sio UKAWA...kwa hiyo hakuna tatizo
 
Ukawa sio chama yaliyofanyika ni maridhiano ya vyama kwa utaratibu waliokubaliana viongozi na yale yaliyohitaji vikao tuliona vikifanyika.
 
Umesema kweli, yaani kitendo cha babu Duni kuachia vyeo vyake na kuchukua kadi ya CHADEMA mbele ya Seif na wenyeviti wenza wa UKAWA haitoshi kujua hayo ndio makubaliano yao?, CDM imetoa rais na CUF itoe mwenza.

Kama kuna mtu anasubiri vyombo vya ukawa vikae atasubiri sana maana haitatokea.

CUF gani tena imetoa mgomgea? Si mmesema babu Duni kahamia chadema na kapewa kadi? CUF hawana chao! hata kura za rais zitakazotoa wabunge wa kuteuliwa hawatakuwa wa CUF bali ni wa chadema!.elewa hivyo mkuu! CUF hawana chao.
 
HAYA BASI NAMUIDHINISHA MIMI HAPA

LOWASA NDIYE MGOMBEA WETU UKAWA NA DUNI NDIYE MGOMBEA MWENZA

Tatizo wewe ukiidhinisha wewe kama wewe mwanachama wa chama cchako aweza kukuburuza wewe na chama mahakamani kupinga maamuzi yako na huyo uliyemwidhinisha kuwa si mgombea halali wa kuungwa mkono na CHAMA kwa kuwa taratibu za kichama za kuidhinisha ikiwemo kuitisha mkutano mkuu hazikufuatwa!! Ikala kwako na mgombea wako uliyeidhinisha bila kibali cha kikao cha chama!!!
 
Back
Top Bottom