VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Lile lengo lenu la kusimamisha wagombea wa pamoja anzieni kwenye chaguzi za Serikali za Mitaa. Chaguzi hizo zitakazofanyika mwaka huu si za kuzipuuza.Ni muhimu sana. Zinatoa dira na kuonesha hila za kupambana nazo mwakani. Sisi CCM tumeshamaliza maandalizi.Tumeshaandikisha tunavyovitaka na kwa idadi tuitakayo. Baada ya Rasimu unafuata msimu adimu na muhimu.
UKAWA, mkichelewa mtakuta mtoto si wenu. Nawashauri tu kama wapinzani wetu wa jadi bila kadi maridadi. Sikieni na muufanyie kazi ushauri wangu huu tu: chaguzi za Serikali za Mitaa ni muhimu kidira na kisera. Mkishangaa tutapita bila kupingwa na kibingwa bila kufungwa.Kumbukueni kuwa hata mbuyu huanza kama mchicha!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
UKAWA, mkichelewa mtakuta mtoto si wenu. Nawashauri tu kama wapinzani wetu wa jadi bila kadi maridadi. Sikieni na muufanyie kazi ushauri wangu huu tu: chaguzi za Serikali za Mitaa ni muhimu kidira na kisera. Mkishangaa tutapita bila kupingwa na kibingwa bila kufungwa.Kumbukueni kuwa hata mbuyu huanza kama mchicha!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam