Ukatili wa Shirika la Bima la Taifa (NIC)

Ukatili wa Shirika la Bima la Taifa (NIC)

chibasi

JF-Expert Member
Joined
Dec 19, 2013
Posts
203
Reaction score
26
Nilikuwa mwanachama wa bima ya matumaini katika SHIRIKA LA BIMA YA TAIFA(NIC) tawi la MWANZA kwa kuchangia michango yangu kwa miaka9. Bima yangu iliiva tangu mwezi Machi 30,20013 lakini hadi leo hii zijalipwa bali danadana kutoka kwa wafanyakazi wa hapa Mwanza. Nimewasilisha malalamiko yangu haya kwa mkurungezi wa taifa kwa njia ya email lakini bado kimya. Naomba waziri husika uingilie kati ili niweze kulipwa haki yangu hii. Pia wadau naomba michango yenu.
Chanzo: Mimi mwenyewe muathirika wa ukatili huo.
 
Pole sana. Mimi ni mwanachama tangu 2008 ila sasa nataka nijitoe sitaki usumbufu baadae maana Wamekaa kitapeli sana!
 
Pole sana. Mimi ni mwanachama tangu 2008 ila sasa nataka nijitoe sitaki usumbufu baadae maana Wamekaa kitapeli sana!

fanya fast jamaa ni tapeli kwelikweli.
 
kwani shirika hilo la nic bado lipo...
 
wale ni vibaka tu kama wengine wa mitaani, mm nilijaribu kujitoa lakini imeshindikana mpaka leo wanaendelea kukata pesa kwnye mshahara.
 
fanya fast jamaa ni tapeli kwelikweli.

nimeanza process za kutoka ila ndo hivyo itakula kwangu. Nimejaribu kuelezea pia ishu yako, wakaomba niwape "Policy No" yako ili wawasiliane na huko, waone ni nini kimekwamisha! Kama vp niPM hiyo P No, kesho naamkia pale makao!
 
wale ni vibaka tu kama wengine wa mitaani, mm nilijaribu kujitoa lakini imeshindikana mpaka leo wanaendelea kukata pesa kwnye mshahara.

Hawa jamaa wanabembeleza sana uingie, ila kutoka ni ngumu sana hadi uwe na roho ya paka!! Pole sana
 
wale ni vibaka tu kama wengine wa mitaani, mm nilijaribu kujitoa lakini imeshindikana mpaka leo wanaendelea kukata pesa kwnye mshahara.

ni zaidi ya ujambazi hawana tofauti vikundi vya kijangili vinavyopatikana duniani.
 
nimeanza process za kutoka ila ndo hivyo itakula kwangu. Nimejaribu kuelezea pia ishu yako, wakaomba niwape "Policy No" yako ili wawasiliane na huko, waone ni nini kimekwamisha! Kama vp niPM hiyo P No, kesho naamkia pale makao!

sawa mkuu, huko maeneo nikutumie muda huu?
 
Lipo mkuu! Sema hapo kati liliyumba sana hadi kufanyiwa 'restructuring'... Limeanza kunyanyuka tena kdg sema ndo hvyo haya mashirika yanafilisiwa na serikali yenyewe-ccm!

nasikia wanakinga ya kutoshitakiwa, ni kweli?
 
Amante umeelezea vema. Ni kweli Shirika lipo under restructuring kwa sasa na madeni mengi yamekwishalipwa yote ya huko Nyuma kabla ya restructuring. Tatizo lililopo ni kwamba Serikali ambaye ni 100% shareholder hajaonesha nia ya dhati ya kulinyanyua Shirika lao. Biashara nyingi za bima zinapelekwa kwenye makampuni binafsi ambapo huko ndipo vigogo wengi wamewekeza na ndio sababu hasa inayofanya wasuesue. Nchi zote za nje zenye mashirika Yake ya Bima hawaruhusu kupeleka biashara nje ya kampuni zao za bima. Hii inasaidia sana kunyanyua mashirika hayo. Ila kinachofanyika hapa Tz ni kichekesho kwa Serikali ambayo ndiyo shareholder kwenye hilo Shirika ambayo haioneshi jitihada zozote za kulinyanyua.
chibasi, nadhani hujafatilia vizuri ishu yako. Hawawezi kukaa nayo kimya kwa sababu kwa sasa wanajitahidi sana kubadilisha taswira ya Shirika. Isitoshe hakuna kinga youote dhidi ya mashitaka. Kesi wanazo Kama mashirika mengine yote na fidia wanalipa Kama kawaida.
Pole kwa matatizo yaliyokupata.

Mi binafsi ni mpenzi sana wa mashirika yetu ya umma isipokuwa uongozi tulionao hauna jitihada za dhati za kunyanyua mashirika yetu ya umma nadhani sababu mpaka sasa utakuwa unajua Jibu la hiyo sababu
 
Last edited by a moderator:
wale ni vibaka tu kama wengine wa mitaani, mm nilijaribu kujitoa lakini imeshindikana mpaka leo wanaendelea kukata pesa kwnye mshahara.

Ungekuwa una nia ya dhati ya kujitoa nadhani ungekwishafanya michakato.
 
hili ni moja ya mashirika ninayoya laaani sana hapa tz mwaka 1999 nilitaabika sana kufuatilia madai yangu lakini mwishowe nikakata tamaa leo ni miaka 16 imepita nafikiria kuanzisha tena utaratibu wa kufuatilia ,huu nu uuwaji,
 
Bi Mkubwa naye bima yake iliiva toka November 30/2013 baada ya kuwachangia jamaa kwa miaka 22 lakini mpaka Leo hii bila bila.

Hawa jamaa wase-scorpion Sana.
 
nimeanza process za kutoka ila ndo hivyo itakula kwangu. Nimejaribu kuelezea pia ishu yako, wakaomba niwape "Policy No" yako ili wawasiliane na huko, waone ni nini kimekwamisha! Kama vp niPM hiyo P No, kesho naamkia pale makao!

Mkuu,how far have you gone with that issue?
 
Mm nilisaini nao mkataba last month nksomba waanze kunikata mwez October.
Kwa Hays mnayoniambia roho inaniuma cjui nifanyaje ili niweze kujitoa kabla ya makato yao kuanza
Naombeni msaada tafadhali

Mpe anae kupa
 
Mm nilisaini nao mkataba last month nksomba waanze kunikata mwez October.
Kwa Hays mnayoniambia roho inaniuma cjui nifanyaje ili niweze kujitoa kabla ya makato yao kuanza
Naombeni msaada tafadhali

Mpe anae kupa
Sikushauri ujiunge. Utajuta. Mimi ni mhanga wa hao jamaa. Nilijitoa katikati, sasa nafuatilia changu ni mwaka wa 4, nineamua kuwaachia tu. Nenda fasta ofisin kwao pia kwa Afisa Utumishi wako, waambie umebadili nia!!
 
Hata simu hawapokei wala kujibu email,mwenye no.yao anitumie hasa tawi la mwanza
 
Back
Top Bottom