Mkuu Dingswayo inasikitisha sana kusema kweli, kama hali ya kupoteza imani katika jumuiya ya Kimataifa itaendelea itafikia wakati Watanzania wenye safari za kihalali nchi za nje kuzikataa safari hizo kwa kuogopa kudhalilishwa kiasi hiki.
Mkuu BAK, zamani miaka ya 80 hadi 90 nilipokuwa nikisafiri nje ya nchi, nilikuwa najivunia sana passport yangu. Chanzo cha kujivunia kilikuwa ni passport yangu, ambayo mara nyingi ilinitambulisha kama Mtanzania na kuulizwa kuhusu Rais Nyerere. Nawaonea sana huruma vijana wengi wa Kitanzania ambao nashuhudia wakisumbuliwa kwa kuwekwa pembeni ili kuhojiwa na kupekuliwa. Ile heshima tuliyopewa zamani imepotea kabisa.
La kusikitisha ni kwamba wale wanaohusika na kutusababishia kadhia, dhihaka na manyanyaso haya yote wao hupita VIP bila bughudha wala kukaguliwa.
Nikikumbuka alichofanya Mwalimu Nyerere juu ya huyu jamaa 'JK' kwa kile alichodai "hajakomaa kisiasa" nimegundua alikuwa anayajua mapungufu yake yenye madhara kwa Taifa, kweli bana leo nimeelewa!
Hakuna nchi yeyote duniani inayojiendesha bila miiko so ukipewa jukumu la kuwatumikia wananch lazma ujiheshmu haiwezekani upewe nafasi ya kuwatumikia wananch halafu unaonekana unapita barabarani na wakina mama kama hauwezi acha ukafanye uhuni wako-mwl jk nyerere