Hizi ni dhana mbili wanazotumia watu waliofilisika kimawazo na kisera (kama alivyosema Nyerere R.I.P).
Huwa hawana pa kuangukia na wanazichagua ili kupata huruma za watu kuwa unaona dini yetu haijawahi kumtoa kiongozi wa juu nichagueni au nipeni uongozi niwakomboe au kabila letu limedharauliwa sana nichagueni muone maendeleo; kabila letu ni dogo sana na hatuna sauti nipeni uongozi nilikomboe au kabila letu ni kubwa sana na sisi ndo tunatakiwa kutoa kiongozi kwa sasa. Ni dhana mufilisi na wanaziendeleza na kuzidakia bila kujua madhara yake kwenye vichwa vya watu
Maana unapopandikiza mbegu hizo kwenye vichwa vya watu ipo siku wale unaowaambia kuwa wanaonewa watanyanyuka na kusema sasa imetosha tumeonea sana wacha tujikomboe.
Kuna jeshi ambalo lipo tayari muda wowote kujitolea kufanya hayo wanayoyapandikiza vichwani mwa watu bila kutarajia