Ujumbe wa kufungia mwaka 2018

Ujumbe wa kufungia mwaka 2018

Nkinga1

Member
Joined
Mar 8, 2013
Posts
42
Reaction score
17
Mwenye kutaka rafiki asiye kuwa na Dosari, basi ataishi mpweke daima.

Mwenye kutaka Mke au Mume ambaye hana mapungufu, ataishi bila ya kuoa au kuolewa mpaka siku ya kufa kwake.

Mwenye kutaka ndugu asiye kuwa na matatizo, ataishi akimtafuta milele.

Mwenye kutaka mtu wa karibu aliyekamilika, daima ataishi akiukataa udugu.

Tuvumilie matatizo ya wenzetu pamoja na changamoto zao, ili turejeshe hali ya maelewano kati yetu.

Unapotaka kuishi kwa furaha maishani, basi usitafsiri kila kitu unachokiona au kukisikia.

Wala usichunguze sana kila kitu kilichopo mbele yako.

Wala usichambue kila kitu unachokiona au kukisoma.

Hakika ya wale walioichambua Almasi sana, mwisho wa siku waliikuta ni Mkaa.

Usiwahukumu watu kutokana na mandhari (muonekano wa nje), vyo vyote vile walivyo.

Fahamu ya kuwa pamoja na yote hayo, bado ni wanadamu kama wewe (uhalisia wao).

Tuvumiliane hakuna mkamilifu isipokuwa Mwenyezi Mungu pekee.
#KARIBU MWAKA 2019
 
Mwenye kutaka rafiki asiye kuwa na Dosari, basi ataishi mpweke daima.

Mwenye kutaka Mke au Mume ambaye hana mapungufu, ataishi bila ya kuoa au kuolewa mpaka siku ya kufa kwake.

Mwenye kutaka ndugu asiye kuwa na matatizo, ataishi akimtafuta milele.

Mwenye kutaka mtu wa karibu aliyekamilika, daima ataishi akiukataa udugu.

Tuvumilie matatizo ya wenzetu pamoja na changamoto zao, ili turejeshe hali ya maelewano kati yetu.

Unapotaka kuishi kwa furaha maishani, basi usitafsiri kila kitu unachokiona au kukisikia.

Wala usichunguze sana kila kitu kilichopo mbele yako.

Wala usichambue kila kitu unachokiona au kukisoma.

Hakika ya wale walioichambua Almasi sana, mwisho wa siku waliikuta ni Mkaa.

Usiwahukumu watu kutokana na mandhari (muonekano wa nje), vyo vyote vile walivyo.

Fahamu ya kuwa pamoja na yote hayo, bado ni wanadamu kama wewe (uhalisia wao).

Tuvumiliane hakuna mkamilifu isipokuwa Mwenyezi Mungu pekee.
#KARIBU MWAKA 2019
Nimekuelewa sana, kilubwa wherever makes people happy let em do, mind ur own businesses n focus on ur journey and things that makes you happy.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom