Fanfa
JF-Expert Member
- Sep 25, 2009
- 2,390
- 3,722
Nianze kwa kuwapongeza UKAWA kwa ujumla kwa mbinu na mikakati yao ambayo imeonyesha dhahiri kuipa wakati mgumu CCM. Hata hivyo jitihada zaidi zinahitajika kama mnataka kushinda uchaguzi huu la sivyo mtaisoma namba kama Rais kikwete alivyosema. Hakuishia hivo tu bali alienda mbali zaidi na kusema wanajua mbinu za kushinda na kwamba wana maarifa zaidi.
Moja ya mbinu na maarifa ya CCM ni hili hapa.
Napenda kuwakumbusha tu kuwa, Pamoja na mikakati yenu mizuri, ni wakati muafaka kwa CHADEMA/UKAWA kushinikiza utaratibu wa utangazwaji wa matokeo ya Urais katika ngazi ya vituo vya kuhesabia kura, ngazi ya kata na ngazi ya jimbo, yakatangazwa na wasimamizi wa uchaguzi ngazi husika.
Sisemi kuwa watatangaza mshindi katika ngazi hiyo bali wasema idadi ya kura alizopata kila mgombea wa Urais ngazi ya kituo, kata na Jimbo mbele ya wapiga kura badala ya kubandika tu kwenye kituo. Hii itaondoa kwa kiwango malalamiko/mivutano isiyokuwa ya lazima na kuzuia uchakachuaji wa matokeo ngazi ya Jimbo na taifa kwenye majumuisho ya matokeo. Hili ni eneo muhimu sana ambalo CCM wataweza kupiga bao la mkono kama utaratibu hautabadilishwa.
Tukumbuke kuwa tume ikishatangaza matokeo ya urais ngazi ya Taifa hakuna kuhoji. Hilo nalo ni bao la pili la mkono.
Kupiga kampeni peke yako hakutoshi bila kudhibiti kwenye mchakatowa upigaji kura.
Kumbukeni kuwa kuiba kura sio rahisi ila kuchakachua kwenye majumuisho ni rahisi sana.
Yangu ni hayo tu kwa leo.
Moja ya mbinu na maarifa ya CCM ni hili hapa.
Napenda kuwakumbusha tu kuwa, Pamoja na mikakati yenu mizuri, ni wakati muafaka kwa CHADEMA/UKAWA kushinikiza utaratibu wa utangazwaji wa matokeo ya Urais katika ngazi ya vituo vya kuhesabia kura, ngazi ya kata na ngazi ya jimbo, yakatangazwa na wasimamizi wa uchaguzi ngazi husika.
Sisemi kuwa watatangaza mshindi katika ngazi hiyo bali wasema idadi ya kura alizopata kila mgombea wa Urais ngazi ya kituo, kata na Jimbo mbele ya wapiga kura badala ya kubandika tu kwenye kituo. Hii itaondoa kwa kiwango malalamiko/mivutano isiyokuwa ya lazima na kuzuia uchakachuaji wa matokeo ngazi ya Jimbo na taifa kwenye majumuisho ya matokeo. Hili ni eneo muhimu sana ambalo CCM wataweza kupiga bao la mkono kama utaratibu hautabadilishwa.
Tukumbuke kuwa tume ikishatangaza matokeo ya urais ngazi ya Taifa hakuna kuhoji. Hilo nalo ni bao la pili la mkono.
Kupiga kampeni peke yako hakutoshi bila kudhibiti kwenye mchakatowa upigaji kura.
Kumbukeni kuwa kuiba kura sio rahisi ila kuchakachua kwenye majumuisho ni rahisi sana.
Yangu ni hayo tu kwa leo.