Lee Van free
JF-Expert Member
- Aug 14, 2024
- 2,246
- 7,110
Ukisikia Vijana wa Kitanzania wanavyohamasishana,wanavyofundishana,wanavyopeana mbinu kwa ajili ya maandamano,kwa ajili ya kukabiliana na polisi waziwazi huwezi kuamini kama Tanzania yangu imefikia hapa.
Sikuwahi hata siku moja kufikiria kama Watanzania watakuja kufikia Hali hii.
Hali hii tumekua tukiisikia Kwa wenzetu TU,toka tukiwa wadogo.
Mioango hii ya mapambano tuliisikia inafanyika Palestina,south Africa, northern Ireland, Kashmir n.k.
Inauma sana Kwa kweli, Leo Hali hii inaenda kutokea kwetu.
Sababu kuu ni Viongozi waliochaguliwa na wananchi hawataki kuwasikikiza wananchi waliowachagua.
Tanzania ilikua msuluhishi mkubwa wa migogoro hapa Afrika Leo nani atatusuluhisha sisi?
Maandamano yafanikiwe ama yasifanikiwe lakini mbegu inayopandwa haitakuja kuoza milele.
Akifa hata mtu mmoja TU tayari nchi itaingia katika historia chafu ambayo haikua asili yetu.
Kiburi na dharau dhidi ya wananchi ni kunapelekea kuwachosa Askari wetu na vyombo vya usalama ,kwa sababu badala ya kuangalia vitisho kutoka nje wanajua bize bila sababu za msingi kukabiliana Watanzania wenzao ndani ya nchi Yao wenyewe.
Nguvu hii inayotumika kukabiliana na wananchi ingetumika kukabiliana na majangili na wahujumu uchumi Leo hii Tanzania ingekua kama Uswis.
Sikuwahi hata siku moja kufikiria kama Watanzania watakuja kufikia Hali hii.
Hali hii tumekua tukiisikia Kwa wenzetu TU,toka tukiwa wadogo.
Mioango hii ya mapambano tuliisikia inafanyika Palestina,south Africa, northern Ireland, Kashmir n.k.
Inauma sana Kwa kweli, Leo Hali hii inaenda kutokea kwetu.
Sababu kuu ni Viongozi waliochaguliwa na wananchi hawataki kuwasikikiza wananchi waliowachagua.
Tanzania ilikua msuluhishi mkubwa wa migogoro hapa Afrika Leo nani atatusuluhisha sisi?
Maandamano yafanikiwe ama yasifanikiwe lakini mbegu inayopandwa haitakuja kuoza milele.
Akifa hata mtu mmoja TU tayari nchi itaingia katika historia chafu ambayo haikua asili yetu.
Kiburi na dharau dhidi ya wananchi ni kunapelekea kuwachosa Askari wetu na vyombo vya usalama ,kwa sababu badala ya kuangalia vitisho kutoka nje wanajua bize bila sababu za msingi kukabiliana Watanzania wenzao ndani ya nchi Yao wenyewe.
Nguvu hii inayotumika kukabiliana na wananchi ingetumika kukabiliana na majangili na wahujumu uchumi Leo hii Tanzania ingekua kama Uswis.