Ujerumani yampongeza Rais Magufuli kwa kupiga marufuku safari za nje ya Nchi. Imekuwa ikimtumia mwaliko wa kwenda Ujerumani.

Daimler

JF-Expert Member
Sep 11, 2018
556
973
IMG_8687.jpg

Balozi Waechter akina na Naibu Spika Tulia Ackson, Mjini Tukuyu, Mbeya.

Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Dk. Detlef Waechter, jana akiwa mkoani Mbeya ameahidi kushirikiana na Tanzania katika kuendeleza Sera za Uwekezaji nchini ikiwa ni pamoja na kuunga mkono juhudi za Rais Dk. John Pombe Magufuli kufanikisha Sera ya Viwanda.
Katika taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila jana baada ya kuwa na mazungumzo na Balozi Waechter ofisini kwake, alisema kuwa, Ujerumani inaunga mkono jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano na kwamba itaendelea kutoa msaada kupitia sekta mbalimbali kikiwemo kilimo. Alisema, Balozi alimwahidi kushawishi Nchi yake kuja kujenga kiwanda cha mbolea mkoani Mbeya.
Aidha, alisema kuwa, "Balozi Waechter amempongeza Rais Magufuli kwa kupiga marufuku safari za nje ya Nchi zisizokuwa na tija kwa Taifa."
Chalamila alisema kuwa, "Serikali ya Ujerumani imekuwa ikimtumia mwaliko Rais Magufuli wa kwenda nchini humo lakini amekuwa akigoma na kuwaeleza kuwa, hadi aiweke sawa Nchi yake."
Balozi Waechter amepongeza amani iliyopo nchini na kusihi kuendelea kuienzi kwani ndiyo sababu kubwa inayowashawishi kuja kuwekeza hapa nchini.

IMG_8689.jpg

Balozi wa Ujerumani akiwa na Waziri wa Mambo ya Nje, Mahiga wakati wa Uzinduzi wa Liaison Office, jijini Dodoma.

IMG_8691.JPG

Balozi akiwa na Wawekezaji wa Kijerumani, Kampuni kubwa la BASF, ambao wameanzisha Ofisi zao Tanzania.

IMG_8692.JPG
 
Huyo balazi hajui kuwa gharama ya safari za nje imehamia kwenye gharama za kurudia uchaguzi kuunga mkono juhudi?

Balozi hajui kuwa mpaka Agosti 12 mwaka huu tumetumia bilioni 15.8 kwa ajili ya kugharami hizi chaguzi (kuunga mkono juhudi)?.

Anyway, huyu ni mwanadiplomasia kwahiyo anajua anatakiwa aongee nini.

Alafu Musiba anawachafua na hatua hachukuliwa!
 
BASF kampuni kubwa sana hii,karibuni wawekezaji,tutakuja tu huko kwenu,ngojeni kwanza nchi ikae sawa...
Nalikubali sana Kampuni la BASF kwani Kampuni hilo kwa pamoja na Bayer ndiyo yameifanya Ujerumani kuwa wababe wa teknolojia ya chemikali hasa mwishoni mwa Karne ya 19 hadi ya 20.
 
Huyo balazi hajui kuwa gharama ya safari za nje imehamia kwenye gharama za kurudia uchaguzi kuunga mkono juhudi?

Balozi hajui kuwa mpaka Agosti 12 mwaka huu tumetumia bilioni 15.8 kwa ajili ya kugharami hizi chaguzi (kuunga mkono juhudi)?.

Anyway, huyu ni mwanadiplomasia kwahiyo anajua anatakiwa aongee nini
Asilimia 90% ya gharama za uchaguzi mdogo hugharimiwa na vyama vya siasa vinavyogombea nafasi hizo. Serikali hugharimia tu kuchapisha karatasi za kura, kusambaza karatasi hizo na kulipa posho za wasimamizi wa upigaji wa kura kwa siku ya kupiga kura ambayo ni sh elfu tano tu kwa kila msimamizi. Mambo mengine yote, yakiwamo ya kampeni ni juu ya vyama vya siasa. Ndiyo maana chadema imeshindwa kuzimudu hizi shughuli ambazo sasa zimefululiza kila mwezi: wamejitoa kwa visingizio vya uwongo.
 
Mna mpongeza kwa kupiga marufuku alafu mna mpa mwaliko wa kusafiri... UNAFIKI HUU... WAZUNGU SIO WATU WAZURI KWA WAAFRIKA...
 
Asilimia 90% ya gharama za uchaguzi mdogo hugharimiwa na vyama vya siasa vinavyogombea nafasi hizo. Serikali hugharimia tu kuchapisha karatasi za kura, kusambaza karatasi hizo na kulipa posho za wasimamizi wa upigaji wa kura kwa siku ya kupiga kura ambayo ni sh elfu tano tu kwa kila msimamizi. Mambo mengine yote, yakiwamo ya kampeni ni juu ya vyama vya siasa. Ndiyo maana chadema imeshindwa kuzimudu hizi shughuli ambazo sasa zimefululiza kila mwezi: wamejitoa kwa visingizio vya uwongo.
Mtumeee!
Siri imefichuka walahi!
 
Asilimia 90% ya gharama za uchaguzi mdogo hugharimiwa na vyama vya siasa vinavyogombea nafasi hizo. Serikali hugharimia tu kuchapisha karatasi za kura, kusambaza karatasi hizo na kulipa posho za wasimamizi wa upigaji wa kura kwa siku ya kupiga kura ambayo ni sh elfu tano tu kwa kila msimamizi. Mambo mengine yote, yakiwamo ya kampeni ni juu ya vyama vya siasa. Ndiyo maana chadema imeshindwa kuzimudu hizi shughuli ambazo sasa zimefululiza kila mwezi: wamejitoa kwa visingizio vya uwongo.
Kinadharia hiki ulichoandika ni kweli. Hata hivyo, ccm wanapata msaada mkubwa wa serikali kuongezea kwenye kile walichopaswa kuwa nacho kabla ya kukitumia kununua wapinzani!
 
Mna mpongeza kwa kupiga marufuku alafu mna mpa mwaliko wa kusafiri... UNAFIKI HUU... WAZUNGU SIO WATU WAZURI KWA WAAFRIKA...
No, wanafahamu kuwa, kuna Ziara nyingine hazihitaji Rais kama Mkuu wa wa Nchi kuhudhuria kwa kuwa ni za kiutendaji zaidi (Rais kama Kiongozi wa Serikali).
 
No, wanafahamu kuwa, kuna Ziara nyingine hazihitaji Rais kama Mkuu wa wa Nchi kuhudhuria kwa kuwa ni za kiutendaji zaidi (Rais kama Kiongozi wa Serikali).
Una fahamu impact ya rais?? Anapo enda sehemu??? Kwann wana mpa mialiko ya Mara kwa mara. Si yupo Possi huko ujereman!????
 
Ile ramani mliyokuwa mnalia nayo washaifuta hapo ubalozini?
Walianza fastjet kuitumia ktk vipeperushi vyao au majarida yao ktk ndege... Nao walitakiwa kuangazwa... Kuwa wameitoa wapi?? UN au Ujereman au makumbusho ya taifa
 
Huyo balozi inaonekana hajui yanayoendelea kama ya wizi wa kura, matumizi ya hovyo ya pesa za walipa kodi kama kujenga uwanja wa ndege Chato na zile trilioni 1.5 zilizopotea n.k.
 
View attachment 873027
Balozi Waechter akina na Naibu Spika Tulia Ackson, Mjini Tukuyu, Mbeya.

Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Dk. Detlef Waechter, jana akiwa mkoani Mbeya ameahidi kushirikiana na Tanzania katika kuendeleza Sera za Uwekezaji nchini ikiwa ni pamoja na kuunga mkono juhudi za Rais Dk. John Pombe Magufuli kufanikisha Sera ya Viwanda.
Katika taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila jana baada ya kuwa na mazungumzo na Balozi Waechter ofisini kwake, alisema kuwa, Ujerumani inaunga mkono jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano na kwamba itaendelea kutoa msaada kupitia sekta mbalimbali kikiwemo kilimo. Alisema, Balozi alimwahidi kushawishi Nchi yake kuja kujenga kiwanda cha mbolea mkoani Mbeya.
Aidha, alisema kuwa, "Balozi Waechter amempongeza Rais Magufuli kwa kupiga marufuku safari za nje ya Nchi zisizokuwa na tija kwa Taifa."
Chalamila alisema kuwa, "Serikali ya Ujerumani imekuwa ikimtumia mwaliko Rais Magufuli wa kwenda nchini humo lakini amekuwa akigoma na kuwaeleza kuwa, hadi aiweke sawa Nchi yake."
Balozi Waechter amepongeza amani iliyopo nchini na kusihi kuendelea kuienzi kwani ndiyo sababu kubwa inayowashawishi kuja kuwekeza hapa nchini.

View attachment 873028
Balozi wa Ujerumani akiwa na Waziri wa Mambo ya Nje, Mahiga wakati wa Uzinduzi wa Liaison Office, jijini Dodoma.

View attachment 873025
Balozi akiwa na Wawekezaji wa Kijerumani, Kampuni kubwa la BASF, ambao wameanzisha Ofisi zao Tanzania.

View attachment 873031
Tuna shida kubwa sana kuwaelewa wenzetu waliobobea katika lugha za kidiplomasia. ndio maana hata pale wanapotutukana kidiplomasia sisi tunashangilia kama mazuzu.

Hivi Kuna mtu alikuwa na kazi kubwa ya kujenga nchi hii kama alivyokuwa nayo Nyerere? maana kabla ya hapo hapakuwa na "taifa", kulilkuwa na mkusanyiko wa makabila ambayo yaliwekwa pamoja ili yatawaliwe na wakoloni. hapakuwa na wasomi, matokeo ya ukoloni, vita ya majimaji, hakuna miundombinu, hakuna chochote. Lakini Nyerere alikwenda huko na huko duniani na pia alitembelea vijijini kuhamasisha kilimo. ziara zake ndio ziliwezesha wingi wa viwanda ambavyo Mkapa alibinafsisha kwa bei chee

Tuwe wakweli tu, Mtanzania namba moja kwa sasa hajiamini akiwa huko nje. hajiamini hapa ndani kiasi kwamba lazima apige marufuku Bunge live, apige marufuku vyama vya siasa - anataka kusifiwa na kila mtu. kama hapa ndani hajiamini, nje hajiamini, matokeo yake ndiyo hayo. kule nje anaweza kupambana na waandishi wa habari? ingawa anaweza hata akaongea kisukuma, si kuna wakalimani watatafsiri tu, wasiwasi wake nini?
 
Asilimia 90% ya gharama za uchaguzi mdogo hugharimiwa na vyama vya siasa vinavyogombea nafasi hizo. Serikali hugharimia tu kuchapisha karatasi za kura, kusambaza karatasi hizo na kulipa posho za wasimamizi wa upigaji wa kura kwa siku ya kupiga kura ambayo ni sh elfu tano tu kwa kila msimamizi. Mambo mengine yote, yakiwamo ya kampeni ni juu ya vyama vya siasa. Ndiyo maana chadema imeshindwa kuzimudu hizi shughuli ambazo sasa zimefululiza kila mwezi: wamejitoa kwa visingizio vya uwongo.
Well explained
 
..ni kweli tumefuta safari za nje zenye gharama kubwa.

..lakini safari za ndani sasa hivi zinahusisha misafara mikubwa na silaha kivita na zina gharama kubwa.
 
Back
Top Bottom