#COVID19 Ujerumani: Chanjo inaweza kuwa lazima Februari 2022

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,037
9,926
Viongozi wa kitaifa na wa kikanda wa Ujerumani wamekubali kuwazuia watu ambao hawajachanjwa kushiriki pakubwa katika maisha ya umma kwa nia ya kuzuia wimbi la nne la Covid-19.

Kansela anayemaliza muda wake Angela Merkel alielezea hatua hizo kubwa kama kitendo cha "mshikamano wa kitaifa".

th

Chanzo cha picha, AFP

Ni wale tu ambao wamechanjwa au kupona hivi majuzi kutokana na Covid ndio watakaoruhusiwa katika mikahawa, sinema, maeneo ya starehe na maduka mengi.

Chanjo zinaweza kufanywa kuwa za lazima ifikapo Februari, kansela aliongeza.

Wimbi la nne la Covid-19 la Ujerumani ndio kali zaidi hadi sasa, na vifo vingine 388 vilirekodiwa katika saa 24 zilizopita.

Pia kuna wasiwasi unaoongezeka juu ya kuenea kwa Omicron, ambayo maafisa wa afya wa EU wanaonya kuwa kunaweza kusababisha zaidi ya nusu ya kesi zote za Covid katika miezi michache ijayo.

Bi Merkel alisema hospitali zimezidiwa hadi wagonjwa kulazimika kuhamishwa hadi maeneo tofauti kwa matibabu. "Wimbi la nne lazima livunjwe na hii bado haijapatikana."

"Kutokana na hali hiyo, nadhani inafaa kupitisha sheria ya chanjo ya lazima," alisema, huku akiweka wazi kwamba hii itabidi kuidhinishwa na bunge.

BBC Swahili
 
Back
Top Bottom