Mkuu kibiashara
Je marine board moja ina size gani? Bei yake ya sokoni (zikiwa mpya) ni sh. ngapi?
Taarifa hizi zitawasaidia wadau kujua wanahitaji boards ngapi na kiasi cha pesa wanachoweza kusave kwa kununua toka kwako.
Kwa mirunda, sehemu nyingi za rejareja wanauza around sh. 2,500.
Je, iwapo mdau anataka kukodisha tu, unakubaliana na option hiyo?
Asante...
Marine board nyingi ni around 8*4 in size.bei zake zinarange from 50,000 to 65,000 kutokana na unene.Namfahamu jamaa anayefanya biashara ya kukodisha Scaffolds(metal) kwa ajili ya ujenzi wa magorofa.am sure these can be reused more efficiently for those looking to venture into this type of business as they are much more flexible than wood.
Mkuu,
Asante kwa taarifa.
Je, jamaa anayekodisha bei zake zikoje?
Mimi niliwasiliana na jamaa mmoja anaitwa Mushi yupo mitaa ya Mbweni, lakini sasa huyu jamaa price yake ni 30,000 kwa Sqrm lakini kumbuka lazima utengeneze Beam zako mwenyewe na hapo lazima Marine kama 20 zilike. Kisha yeye atakupa hizo sheet metal ambazo utakaa nazo only for 4 weeks. 30,000 sqrm ni pamoja na labor. Hii nyumba ya 144 sqrm ilikuja 5 million ukijumlisha na marine nikaona bora ninunue marine zote nifanye foarmwork mwenyewe. It was expensive.
Huyo jamaa bei yake ni kubwa mno. Elfu 30 kwa square metre ni TOO MUCH. This is more expensive than kununua mbao au marine boards!!!
ndio maana nikanunua Marine mwenyewe. Formwork ilinigharimu kama million 8 hivi. Hapa kuna Marine kama 120, Mirunda nilinunua 800, misumari niliacha kuhesabu maana. Mbao zililika za kutosha zababu ya kutengeneza canopy sijui ngazi ya kumwaga jamvi na nyingine za kushikilia canopy nje. Plus 800,000 labor ya formwork.
Ila mkuu kwa nyuma ya sq. m 144 mirunda 800 huyo fundi wako aliiweka wapi?
Mimi nakushauri kama bado unajenga na huyo fundi kuwa karibu sana na materials anavyotumia. Usimpe pesa akanunue au kumuwekea materials ukaondoka. Nyumba ya sq. m 144 haitakiwi kuzidi mirunda 400.
Ukitaka kujenga hakikisha unayo pesa sio kuleta ubangaizaji ndio mwishowe ni kuuwana; vifaa chakavu vya ujenzi haviwezi kuwa na strength ileile kama vikiwa vipya sasa unapovifanyia biashara ya kuvizungusha na kuvizungusha gorofa hadi gorofa mwishowe ni misiba na kuishia jela. Kama huna pesa kapange usilete biashara kichaa kwenye uhai wa wenzio
ZeMarcopolo,
Nataka fundi mkali wa kunipaulia kaka. Nataka kuchukua likizo kabisa kama una contact zozote please share kaka.
ZeMarcopolo,
Nataka fundi mkali wa kunipaulia kaka. Nataka kuchukua likizo kabisa kama una contact zozote please share kaka.
Kama upo Dar naweza kukuunganisha na fundi wa kupaua mkali sanaa, ukitaka wa gypsum na fundi rangi mzuri pia
Dr ZeMarcopolo leo ninakupigia salute. Hakika tuweke SIHASA pembeni pia wakati mwingine tuje na issu critical kama hizi. Umenifundisha kitu hapa. Asante sana.Wana JF,
Lengo la thread hii ni kupeana maarifa ya jinsi ya kupunguza gharama za ujenzi wa SLAB ya ghorofa.
Gharama ya ujenzi wa slab "inatia uchungu" kwa vile inahusisha mahitaji ambayo ni disposable lakini ni ya gharama kubwa. Mahitaji hayo ni support ya kubeba zege (mbao, plywood au iron sheet), mirunda, vyuma na misumali. Gharama hizi zinakadiriwa kuwa asilimia 20 ya materials za slab nzima. Hii si gharam ndogo. Kwa ghorofa moja yenye slab ya mita za mraba 140 inahitajika kama shilingi milioni 3.5 - 4.
Kuhusu Mbao, plywood, iron sheet na mirunda kuna haja ya kubuni mbinu mbalimbali za kupunguza gharama kama ifuatavyo:
1. Tafuta jirani aliye kwenye hatua inayofanana na wewe kwenye ujenzi na ukubaliane naye akuuzie materials zake akimaliza au wewe umuuzie ukimaliza.
2. Ulizia iwapo kuna wakodishaji wa vifaa hivyo. Hakikisha unakubaliana bei na jinsi ya kufidia mbao na mirunda itakayokatwa.
3. Nunua materials mpya na uanzishe biashara ya kuzikodisha baada ya kutumia.
4. Fanya urafiki na watu wenye makampuni ya ujenzi. You can even get these materials FOR FREE!!!
5. Anza kukusanya materials kidogokidogo toka kwa wajenzi wasiohitaji. Kama jirani yako anataka kutupa mrunda muombe akupe, akiweka mbao jalalani chukua. Kama kichaa vile lakini inaweza kusave you a great deal of money.
6. Kuwa mkali kwa fundi asitupe na kupoteza vipisi ambavyo vingeweza kufanya kazi na more importantly "asikosee mahesabu".
7. Nunua vifaa unavyohitaji kwa wingi kwa pamoja katika maduka ya jumla. Ukiamua kufanya hivyo hakikisha una utaratibu salama wa kuvihifadhi.
Njia hizi zinaweza kupunguza gharama za materials hizi "disposable" kwa asilimia 50-90!
Katika thread hii wale wenye biashara za kukodishe mbao, plywood, iron sheer, mirunda, vyumba etc tafadhali wekeni terms za biashara zenu ili kuwapa members picha halisi ya jinsi wanavyoweza kupunguza gharama za ujenzi wa slab.
Iwapo umejenga slab na una materials zilizobaki. Tumia thread hii kuingia deal na wadau ili uwauzie au kuwakodisha.
Kwenye ujenzi tunasema "every shilling is GOOD". Save shilling yako kwa kuuza mbao ambazo zingeliwa na mchwa.
Dr ZeMarcopolo leo ninakupigia salute. Hakika tuweke SIHASA pembeni pia wakati mwingine tuje na issu critical kama hizi. Umenifundisha kitu hapa. Asante sana.
Marine plywood ina ukubwa wa 1.2*2.4 meters na unene wa 16mm. Mara ya mwisho nimeulizia(miezi mi3 iliyopita) minimum price ilikuwa 75,000
Wakuu mimi nimejenga kigorofa cha square meter 144, Juu 3 bedroom (all masters ) sebule ndogo na Patio. Marine sheet peke yake zimekula million 6, ukiweka na mbao unaweza lia machozi. Mirunda nilinunua 800 hiyo ni 2 million, sasa mbao za 13000 ndio sikumbuki maana niliacha na kuhesabu kabisa. In short nyumba ya 144 sqrm andaa sio chini ya milion 27 kupiga slab tuu.
Msingi nadhani sio bei kali kama Slab.
Ukitaka kukodisha metal sheet za formwork kutoka kwa jamaa wa mtaani wale wanakupa kwa 4 weeks wanakucharge kama 30,000 kwa sqrm, hawakupi frame za beam, hivyo bado utaingia 2 au 3 million gharama, vilevile canopy yake sio kama ya mbao.
Misumari inayolika unaweza kulia machozi. Ujenzi wetu Tanzania bado ni wa karne ya 7.
Mara nyingi washauri wa masuala ya ujenzi nchini hawako scientific. Wanatumia zaidi hisia kuliko evidence.
Hao waliokwambia udongo hauwezi kubeba ghorofa ni obvious kuwa walikudanganya kwa sababu ghorofa moja la matumizi ya residential halina tofauti kubwa na nyumba ya chini. Kwahiyo kama eneo halifai kwa ghorofa moja residential basi hata nyumba ya chini lisingefaa kujenga.
Pole, lakini zipo njia za kubadilisha nyumba ya chini kuwa ghorofa. Njia hizo zinaweza kuhitaji mabadiliko ya paa tu na si kubomoa nyumba nzima.
Natafuta marine boards za kukodisha lakini ziwe zimetumika sio zaidi mara moja.
Ukitaka kujenga hakikisha unayo pesa sio kuleta ubangaizaji ndio mwishowe ni kuuwana; vifaa chakavu vya ujenzi haviwezi kuwa na strength ileile kama vikiwa vipya sasa unapovifanyia biashara ya kuvizungusha na kuvizungusha gorofa hadi gorofa mwishowe ni misiba na kuishia jela. Kama huna pesa kapange usilete biashara kichaa kwenye uhai wa wenzio