Nyie wote hamjui mnachokisema. Mnadhani miundombinu huwa inajiumba.
Kwa taarifa yenu hao jamaa wanajitahidi kupita maelezo. Ingekuwa wachina wenu hali ingekuwa mbaya sana.
Kumbuka hao jamaa hawajapewa provision ya kuweka njia mchepuko (diversion). yaani wajenge humo, watu wapite humo humo, magari, pikipiki..n.k. Ni kazi kubwa sana kwa sisi tunaojua.
Kama mnataka msipate usumbufu basi ilazimisheni serikali ibomoe nyumba ambazo Magufuli alipigwa stop kuzibomoa, humo ndimo mulimotakiwa kupita njia mchepuko ili kule kati kazi iendelee bila usumbufu.
Na kwa taarifa yenu, hiyo kazi inatakiwa kukabidhiwa mid 2015. Hadi sasa jamaa wamshamaliza zaidi ya 60% ya kazi na muda uliotumika ni takribani nusu ya muda wote unaotakiwa. Kwa hiyo wanafanya vizuri sana.
Tatizo la watanzania wengi ni kujifanya wataaluma wa kila kitu, na kufuata mkumbo bila kujua mambo kiundani.