Ujenzi: Nimefanya uchunguzi kwanini watu wengi wanashindwa au kuchelewa kuwa na kwao

Reagan Carima

Member
May 20, 2015
44
194
Kwa wakazi wengi wa mjini kuna jambo moja ambalo limekuwa kizungumkuti sana kwa watu wengi hasa sisi wa uchumi mdogo.

Hakuna mtu anayependa kuishi kwenye Nyumba za kupanga hivyo kila mtu anapenda kujenga awe na kwake, mahala ambapo atakuwa huru kufanya anavyotaka yeye.

Nimefanya uchunguzi ni kwanini watu wengi wanashindwa au kuchelewa kuwa na kwao.

1. Watu wengi wanaogopa kujenga, yaani mtu anakuwa anasubiri awe na pesa nyingi ndio aanze ujenzi.
Mara nyingi kadiri mtu umri unavyoongezeka na majukumu nayo huongezeka hivyo kipato hakitaruhusu uwe na pesa nyingi

2. Watu wanatamani vitu ambavyo hawana uwezo navyo. Jirani yangu kuna mama alipata pesa yake kiasi akaamua kwenda kuanza ujenzi kwenye kiwanja chake, pasipo kufanya tathmini ya uchumi wake alianzisha msingi wa jumba kubwa kiasi kwamba pesa aliyokuwa nayo yote iliishia kwenye msingi.

Mpaka sasa anajikongoja lakini kutokana na ukubwa wa nyumba basi imesogea mpaka kwenye madirisha ndani ya miaka kama mitano sasa. Lakini ukipiga hesabu vizuri ni kwamba pesa aliyokwisha tumia angeweza kujenga nyumba ndogo angalau ya vyumba viwili na sebule na leo angekuwa anaishi kwake.

So tukadirie haya mambo
 
Kuna ile dhana umepata kiwanja kizuriii unasema kwa kuwa hichi kiwanja ni kuzuri najenga eneo hili sitaki nije bomoa tena nataka nijenge kitu cha moja kwa moja vyumba vya kutosha mfano vinne, hapo ndipo wengi wanapo anguka, unajenga vyumba vinne matokeo yake humalizi kwa wakati na bila malengo na kuendelea kukuongezea gharama, wakati ungejenga vyumba vitatu ingefaa tu na kumaliza na kuhamia kwa haraka
 
Kuna ile dhana umepata kiwanja kizuriii unasema kwa kuwa hichi kiwanja ni kuzuri najenga eneo hili sitaki nije bomoa tena nataka nijenge kitu cha moja kwa moja vyumba vya kutosha mfano vinne, hapo ndipo wengi wanapo anguka, unajenga vyumba vinne matokeo yake humalizi kwa wakati na bila malengo na kuendelea kukuongezea gharama, wakati ungejenga vyumba vitatu ingefaa tu na kumaliza na kuhamia kwa haraka
Haswaaa na asilimi kubwa watu wanaanguka hapo
 
Haya unayosema kiongozi ni sahihi ,mimi nimejenga nyumba ya ndoto yangu ila kidogo kidogo ,..

Nilichofanya ni kuwa na ramani ya nyumba nayoitaka, kisha nikaanza kuinyanyuwa vyumba viwili ambavyo master na nashukuru haikuchukua muda sana, japo nayo imenigharimu kulingana na aina ya ujenzi niliotaka.

Maana nilitaka nijenge nyumba ambayo zitakuja kujutia baadae au kuja kujenga tena, kwa hiyo nilijitahidi kujenga kila kitu katika kiwango bora ila kama ningetaka nimalize ramani yote nahisi mpaka yesu angerudi angenikuta nipo kwenye msingi ama linta na sijapauwa sijui napauwa lini.
 
Mpe mbongo bilioni 10 atajenga mijumba akitegemea kurejesha mapesa yake baada ya miaka 10 hadi 20.

Mpe msomali bilioni 10 atafungua maduka makubwa, ata import na kukuza biashara zake kwa eneo husika.

Mpe Muhindi bilioni 10 ataanzisha kiwanda kitakua kikubwa na atapiga pesa kwa muda mrefu.

Ujumbe tusifikirie kujenga sana tuache dhana ya uoga 😂😂😂😂😂
 
Kwa mfano unakuta mtu ana hela sana prondo lakini bado anakaa nyumba ya kupanga hii tunasemaje ni maamuzi au hajawa na mpango mkakati, mimi na hisi mada ipo wazi imejielezea vizuri sana, kuwa ukitaka kujenga una kiasi chako nini cha kuzingatia.
Hii ni kujisahau. Unapata hela unaweza kulipa Kodi popote unaona huna umuhimu wa kujenga 'nje' ya mji. Siku unashtukia mrija wa pesa umeziba ndio unaanza kujuta.
 
Umekuja na uzi mzuri, watu wapite hapa wapate uzoefu
Nilikuwa nawaza sana suala la ujenzi. Nikishaenda kwa architecture akanichorea ramani moja tamu sana ila nilipopiga hesabu nikagundua ile nyumba ili niikamilisha basi itanipasa kupambana na kuitesekea sio chini ya miaka 10.

Basi nikaona isiwe kesi nikamchukua fundi tukaenda site last week tukapima nikamwambia aniwekee kijumba changu cha room 2 na sebule tu.

Leo hii nafunga lenta na wala haijaniumiza sana kiasi hata cha kuathiri biashara zangu. Na finishing pia sioni hata dalili ya kuja kunitesa na nina uhakika Mungu akipenda basi nitaikamilisha hata ndani ya mwaka huu
 
Kwa mfano unakuta mtu ana hela sana prondo lakini bado anakaa nyumba ya kupanga hii tunasemaje ni maamuzi au hajawa na mpango mkakati, mimi na hisi mada ipo wazi imejielezea vizuri sana, kuwa ukitaka kujenga una kiasi chako nini cha kuzingatia.
Pana dada mmoja ukiangalia kodi anayolipa hapo anapokaa kama angeamuwa kupanga nyumba ya uswahilini bei nafuu basi angekuwa ameshaanza ujenzi
na pili anataka kujenga nyumba kubwa wakati uwezo hana namwambia jenga kwanza ya wastani ili kujihifadhi ,hasikii
 
Back
Top Bottom