Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekabidhi rasmi eneo kwaajili ya uwanja wa Ndege wa Kimataifa Kisiwani Pemba ambao utagharimu Euro Milioni 170 ili kufungua fursa za kiuchumi kisiwani Humo
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla amemwakilishi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi kwaajili ya tukio hilo kubwa la kihistoria
Hemed amesema kuanza kwa mradi huo kunaenda kufungua fursa za uchumi kupitia utalii na biashara ambao utafaidisha wananchi wa kisiwa hicho
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Uchukuzi Dkt Habiba Hassan Omar amesema mradi huo wa Ujenzi wa Uwanja wa ndege utagharimu Euro Milioni 170 ambao utakuwa na uwezo wa kuhudumia abiria 300,000 kwa mwaka na kuruhusu ndege kubwa kutua moja kwa moja
Aidha amesema Kampuni ya Propav itakua na jukumi pia la ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami yenye urefu wa kilomita 43.5 kutoka Mkoani hadi Chake Chake na kugharimu Euro Milioni 93
Amesema miradi hiyo ukiwemo wa uwanja wa ndege utatoa fursa za ajira 1000 kwa wananchi wa Pemba
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mheshimiwa Hemed Suleiman Abdulla amemwakilishi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwinyi kwaajili ya tukio hilo kubwa la kihistoria
Hemed amesema kuanza kwa mradi huo kunaenda kufungua fursa za uchumi kupitia utalii na biashara ambao utafaidisha wananchi wa kisiwa hicho
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Uchukuzi Dkt Habiba Hassan Omar amesema mradi huo wa Ujenzi wa Uwanja wa ndege utagharimu Euro Milioni 170 ambao utakuwa na uwezo wa kuhudumia abiria 300,000 kwa mwaka na kuruhusu ndege kubwa kutua moja kwa moja
Aidha amesema Kampuni ya Propav itakua na jukumi pia la ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami yenye urefu wa kilomita 43.5 kutoka Mkoani hadi Chake Chake na kugharimu Euro Milioni 93
Amesema miradi hiyo ukiwemo wa uwanja wa ndege utatoa fursa za ajira 1000 kwa wananchi wa Pemba