Ujambazi Mkoa wa Pwani umezidi

hps300

Senior Member
Feb 20, 2016
170
152
Polisi mkoa wa Pwani ongezeni Juhudi za kupambana na majambazi. Kwani hali ni mbaya kufuatia matukio ya wizi wa kutumia silaha. Hawa jamaa ni kama Pwani ndo wamefanya makao yao kwa sasa. Wanafanya wanachotaka na muda wanaotoka na kwa staili ile ile ya kuvaa kininja.

Wiki iliyopita Maeneo ya Misugusu zaidi ya familia tisa zimevamiwa kwa usiku mmoja. Wiki moja kabla tukio kama hilo lilitokea maeneo ya viziwa ziwa. Usiku wa kuamkia leo aliyewahi kuwa mkuu wa Wilaya ya Liwale ameua baada ya kuvamiwa na majambazi ambao walimpiga risasi.

Baada ya kumua Former Liwale DC wakavamia nyumba ya jirani yake ambaye kwake wamefanikiwa kuchukua shilingi elfu 87,000 za kitanzania na kumjeruhi, kwa sasa amelazw Tumbi hospital.
Pwani hali inatisha na sijui huku tunakoelekea itakuwaje.
 
Polisi mkoa wa Pwani ongezeni Juhudi za kupambana na majambazi. Kwani hali ni mbaya kufuatia matukio ya wizi wa kutumia silaha. Hawa jamaa ni kama Pwani ndo wamefanya makao yao kwa sasa. Wanafanya wanachotaka na muda wanaotoka na kwa staili ile ile ya kuvaa kininja.

Wiki iliyopita Maeneo ya Misugusu zaidi ya familia tisa zimevamiwa kwa usiku mmoja. Wiki moja kabla tukio kama hilo lilitokea maeneo ya viziwa ziwa. Usiku wa kuamkia leo aliyewahi kuwa mkuu wa Wilaya ya Liwale ameua baada ya kuvamiwa na majambazi ambao walimpiga risasi.

Baada ya kumua Former Liwale DC wakavamia nyumba ya jirani yake ambaye kwake wamefanikiwa kuchukua shilingi elfu 87,000 za kitanzania na kumjeruhi, kwa sasa amelazw Tumbi hospital.
Pwani hali inatisha na sijui huku tunakoelekea itakuwaje.
 
R.I.P former Liwale DC ndg.Efraim Mfingi Mbaga.
Dip.Ed Morogoro TTC(1998-2000),BED University of Arusha(2007-2010)
 
Polisi mkoa wa Pwani ongezeni Juhudi za kupambana na majambazi. Kwani hali ni mbaya kufuatia matukio ya wizi wa kutumia silaha. Hawa jamaa ni kama Pwani ndo wamefanya makao yao kwa sasa. Wanafanya wanachotaka na muda wanaotoka na kwa staili ile ile ya kuvaa kininja.

Wiki iliyopita Maeneo ya Misugusu zaidi ya familia tisa zimevamiwa kwa usiku mmoja. Wiki moja kabla tukio kama hilo lilitokea maeneo ya viziwa ziwa. Usiku wa kuamkia leo aliyewahi kuwa mkuu wa Wilaya ya Liwale ameua baada ya kuvamiwa na majambazi ambao walimpiga risasi.

Baada ya kumua Former Liwale DC wakavamia nyumba ya jirani yake ambaye kwake wamefanikiwa kuchukua shilingi elfu 87,000 za kitanzania na kumjeruhi, kwa sasa amelazw Tumbi hospital.
Pwani hali inatisha na sijui huku tunakoelekea itakuwaje.
Ujambazi unastahili kuunduwa mamlaka mahususi kama ilivyo Ile ya madawa ya kulevya!?!
 
Ni kweli Polisi ifanye jitihada za makusudi kulitatua hili tatizo, Mfano hapo kata ya Kibindu Hivi karibuni mifugo imekuwa ikiibwa sana.
 
Ni kweli Polisi ifanye jitihada za makusudi kulitatua hili tatizo, Mfano hapo kata ya Kibindu Hivi karibuni mifugo imekuwa ikiibwa sana.
Polisi siyo wapiga ramli hadi wajue yote hayo, ukiona mafanikio ya polisi, jua kuna jitihada za makusudi za wasio polisi.

Uhalifu, hupangwa, huandaliwa na kisha hutekelezwa. Katika hatua hizo tatu, lazima watu wanajua kinachoendelea, haiwezi kufanyika kimya kimya na ikawa siri 100%.

Sasa kwa nini wanafanikiwa? Maoni yangu, sisi wananchi tumebariki yatekelezwe. Kivipi?

1. Mahusiano na polisi ni madogo, hatupashani habari na vyombo vya usalama polisi inclusive.

2. Hakuna jitihada mitaani kwetu, hakuna ulinzi tunajilalia tu. Mahali ambako mitaa imejiwekea utaratibu wa ulinzi, haishambuliwi kirahisi.

3. Tumewakumbatia wahalifu, nadhani ni kwa kuamini hawatofika kwetu, lkn siku tusiyojua watafika tu.

Tuuchukie uhalifu, tuwasaidia polisi na vyombo vya usalama
 
Hawa sio majambazi tena kwani ujambazi wao unachagua viongozi tu huu ni dalili za kuanza ugaidi serikāli ichukue tahadhari za haŕaka kabla mambo hayajawā mabaya zaidi.
 
Ni hatari sana na hivi hatujazoea kuwa hata na siraha utawasikia wanavunja mrango mpaka wanaingia huwezi kufanya kitu zaidi ya kutegemea huruma yao waibe bila kukudhuru...wabongo na ukatili walionao wanachukua mali na kuua...
 
Yaaa juzi walinibomolea kwangu mitaa ya Jirani na misugusugu wakaiba pikipiki na cement.nimeenda kuriport polisi kituo cha Kwa kipofu naambiwa wao hawashughuliki na kesi kama hiyo niende mlandizi,sasa sijui kituo cha Kwa kipofu kina kazi gani?
 
Hakuna kitu rahisi duniani kama kuzuia uharifu,serikali lazima itafute na kutumia maarifa ya wananchi wake ili kukabiliana na changamoto kwenye jamii.Haimaanishi kwamba walioajiriwa serikalini ndio wana akili nyingi na wana uwezo wa kutatua matatizo ya watanzania wote ila mtaani napo kuna watu wenye akili za vipaji ambavyo vinaweza kulisaidia Taifa.
 
Hakuna kitu rahisi duniani kama kuzuia uharifu,serikali lazima itafute na kutumia maarifa ya wananchi wake ili kukabiliana na changamoto kwenye jamii.Haimaanishi kwamba walioajiriwa serikalini ndio wana akili nyingi na wana uwezo wa kutatua matatizo ya watanzania wote ila mtaani napo kuna watu wenye akili za vipaji ambavyo vinaweza kulisaidia Taifa.

Ni kweli kabisa raia wanaweza saidia polisi namna ya kukabiliana na hao.majambazi. Tatizo.ni.kwamba jeshi linajaribu kuweka distance na raia kitu ambacho information nyingi ambazo wangeweza kuzipata hawatazipata tena kama inavyostahili.

Polisi jamii ni kitengo kizuri sana cha kukaa na jamii kwa karibu na kuweza kugundua maovu yote yaliyopo.
 

Similar Discussions

5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom