Uingereza yaishambulia tena IS nchini Syria

Uingereza yaishambulia tena IS nchini Syria

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
43,037
Reaction score
34,741
Eneo ambapo moja ya bomu limelipuliwa. Kiongozi wa Ulinzi na Usalama, Michael Fallon akiongea na Ofisa wa Jeshi alipowasili RAF Akrotiri Kusini mwa Cyprus.
Moja kati ya ndege za kivita zilizoshambulia Syria usiku wa kuamkia leo.
Fallon akiongea na maofisa wa jeshi. Moja ya ndege hizo ikiondoka. ?.akiamuru ndege kuruka. Fallon akielezea kilichotokea usiku wa kuamkia leo. Ndege aina ya Typhon ikiondoka.
NDEGE za kivita za Uingereza zimefanya shambulio kwa mara ya pili kwenye ngome za kundi la wapiganaji wa Islamic State usiku wa kuamkia leo nchini Syria tangu kuidhinishwa na bunge kwa operesheni hiyo.Wabunge waliidhinisha mashambulizi dhidi ya IS Jumatano na muda mfupi baadaye ndege za jeshi la anga la nchini hiyo zikaangusha mabomu kwenye ngome za kundi la IS.Ripoti zinasema ndege hizo kwa mara nyingine zimeshambulia visima vya mafuta, na kwamba ndege mbili aina ya Tornado zilifanya shambulio kwa mara ya kwanza na kulipua visima saba vya mafuta wakati leo ndege mbili aina ya Typhoon na Tornado mbili zimefanya shambulio kwenye ngome ya IS.Mapema Alhamisi, ndege nne aina ya Tornado ziliangusha mabomu katika visima vya mafuta vya Omar vilivyopo Mashariki mwa Syria.Ndege hizo zinatumia kambi ya RAF iliyoko Akrotiri nchini Cyprus na hakuna vifo wala majeruhi walioripotiwa kutokana na shambulio hilo.Ijumaa, Bunge la Ujerumani nalo liliidhinisha kutolewa kwa usaidizi wa kijeshi kwa vikosi vinavyopambana na wapiganaji hao nchini Syria.Juhudi za mataifa ya Magharibi dhidi ya kundi hilo zimezidishwa tangu kuuawa kwa watu 127 kwenye mashambulio kadhaa mjini Paris, Ufaransa mwezi uliopita.
 
Teh teh teh

Eti Islamic state.Muslims ndugu zenu wanateketea kila sekunde halafu nyie mpo kimya

Mataifa ya magharibi yanatumia mwamvuli wa terrorism kuwapuputisha mpaka mpungue.

Mzungu mzungu tu..!
 
Teh teh teh

Eti Islamic state.Muslims ndugu zenu wanateketea kila sekunde halafu nyie mpo kimya

Mataifa ya magharibi yanatumia mwamvuli wa terrorism kuwapuputisha mpaka mpungue.

Mzungu mzungu tu..!

Hao wakipukutika 'siyo issue' sana. Ukitaka uone nguvu yetu thubutu kutukataza tusiende kuishi ulaya na Marekani.
 
Vita inayoendelea sasa ni nani atamiliki visima vya mafuta.. Russia au nato. Kama utakumbuka wiki iliyopita assad alilaumu mashambulizi ya uingereza kuwa sio ya kibinadamu ni ya kinyama.. tujiulize kwa nani assad aongee hivyo.....
 
syria has become a testing gournd of weapons for all major super powers..... all new tiny war toys are now being tested in syria
 
Vipi zile S-400 bado hazijawa activated kutungua ndege za NATO zinazoingia Syria bila ya idhini ya Urusi?
 
Hivi mmeshawahi kujiuliza hivi vikundi vinatoa wapi silaha? na hakuna hata nchi moja kubwa ilishawahi kusema au kuishutumu nchi yeyote kuwauzia silaha. Fikiri usiendeshwe na mihemko
 
syria has become a testing gournd of weapons for all major super powers..... all new tiny war toys are now being tested in syria

I second you Bro.
The so called Super power nations are nothing More than International thieves..After all,their central target is Oil
They spread rumors all around the Globe so as to support their Evil plan.
Shiiit.white are Demonic bloodline
 
Back
Top Bottom