MakinikiA
JF-Expert Member
- Jun 7, 2017
- 5,551
- 7,596
Serikali ya Uingereza imeondoa baadhi ya vikwazo dhidi ya mafuta ya Urusi,huku bei ya mafuta ikipanda nchini humo.
Agizo hilo limeanza kutekelezwa hii leo, na inaashiria hofu inayoongezeka kuhusu upatikanaji wa mafuta kutokana na kuzuizi kilichowekwa katika Mlango bahari wa Hormuz tangu kuanza kwa vita kati ya Marekani na Israel dhidi ya Iran.
Vikwazo dhidi usafirishaji wa gesi ya asili ya Urusi iliyoyeyushwa (LNG) pia vimeondolewa.
Hatua kama hiyo iliyochukuliwa na Marekani hivi majuzi ilikosolewa vikali.
Bei za mafuta ya ndege barani Ulaya zimeongezeka mara mbili Zaidi baada ya vita kuanza, huku bei ya mafuta katika vituo za mafuta zikipanda.
Mashirika kadhaa ya ndege nchini Uingereza na duniani kote yamehairisha safari zake na kuongeza bei za tiketi kutokana na kupanda kwa bei mafuta ya ndege.