Uhusiano wa Zitto Kabwe na Tundu Lissu hauna maslahi kwa Upinzani

DALA

JF-Expert Member
Aug 24, 2009
2,212
4,517
Salaam wanajukwaa,

Nimechukua muda kutafakari ukaribu uliopo kati ya Zitto Zuberi Kabwe na Tundu Lissu kwa muda sasa, kwa bahati mbaya sana labda ni kutokana na uelewa wangu finyu wa kisiasa ndo maana natilia urafiki huu mashaka.

Binafsi nilimpenda Zitto enzi zileee za 2007 nakumbuka alipotimuliwa bungeni kuhusu mkataba wa Buzwagi nilikuwa kati ya walionyeshewa wakati wa mapokezi yake Jangwani ila baada ya pale jamaa alikubali kuwa kwenye tume iliyoundwa na JK ya madini. Yaliyofuata wengi tunajua.

Baada ya pale kimsingi sikuweza tena kumuamini Zitto kutokana na siasa zake ndani ya CHADEMA ambapo alilenga sana kujijenga yeye na kujiona bora kuliko wenzane na chama kwa ujumla jambo ambalo lilipelekea yeye kutimuliwa baada ya njama zake kugundulika.

Zitto ameendelea kunishawishi kwamba siyo mtu wa kuaminiwa na upinzani kila siku hususani kwenye uchaguzi wa 2015 aliposhirikiana na CCM.

Leo hii Zitto anajaribu kujenga mahusiano na Lissu eti ni urafiki wenye manufaa kwa upinzani?!

Mimi mpaka kesho simuamini Zitto na najua Lissu akikubali tu ulaghai wa Zitto ndo mwisho wake kisiasa. Nafsi yangu inanikataza kuamini kwamba Zitto ana nia njema na upinzani.

Wakati utaongea.
 
Lissu ni makini, na usidhani hajui haya unayoongea.

Lipo wazi hilo, alaf
Lissu ni makini, na usidhani hajui haya unayoongea.
u vijan wengi sijuhi hawajuhi au wanasahau kuwa ni LISSU ndio aliyeleta na kutoa ushahidi waq Zitto kuwa msaliti na ni yeye alishahuri afukuzwe kabla hajaenda mahakamani.

vijan hawasomi na wala, hawa ulizi kumbukumbu kabisa.
 
Lipo wazi hilo, alaf

u vijan wengi sijuhi hawajuhi au wanasahau kuwa ni LISSU ndio aliyeleta na kutoa ushahidi waq Zitto kuwa msaliti na ni yeye alishahuri afukuzwe kabla hajaenda mahakamani.

vijan hawasomi na wala, hawa ulizi kumbukumbu kabisa.
Wanakurupuka tu hawa mkuu, hivyo tuwapotezee tu.
 
Salaam wanajukwaa,

Nimechukua muda kutafakari ukaribu uliopo kati ya Zitto Zuberi Kabwe na Tundu Lissu kwa muda sasa, kwa bahati mbaya sana labda ni kutokana na uelewa wangu finyu wa kisiasa ndo maana natilia urafiki huu mashaka.

Binafsi nilimpenda Zitto enzi zileee za 2007 nakumbuka alipotimuliwa bungeni kuhusu mkataba wa Buzwagi nilikuwa kati ya walionyeshewa wakati wa mapokezi yake Jangwani ila baada ya pale jamaa alikubali kuwa kwenye tume iliyoundwa na JK ya madini. Yaliyofuata wengi tunajua.

Baada ya pale kimsingi sikuweza tena kumuamini Zitto kutokana na siasa zake ndani ya CHADEMA ambapo alilenga sana kujijenga yeye na kujiona bora kuliko wenzane na chama kwa ujumla jambo ambalo lilipelekea yeye kutimuliwa baada ya njama zake kugundulika.

Zitto ameendelea kunishawishi kwamba siyo mtu wa kuaminiwa na upinzani kila siku hususani kwenye uchaguzi wa 2015 aliposhirikiana na CCM.

Leo hii Zitto anajaribu kujenga mahusiano na Lissu eti ni urafiki wenye manufaa kwa upinzani?!

Mimi mpaka kesho simuamini Zitto na najua Lissu akikubali tu ulaghai wa Zitto ndo mwisho wake kisiasa. Nafsi yangu inanikataza kuamini kwamba Zitto ana nia njema na upinzani.

Wakati utaongea.
Lisu anaenda ACT wazalendo kwa sababu kule kuna wapinzani wa kweli wasiotegemea ruzuku!
 
Zitto ni mtu wa system na baadhi ya viongozi wote wa upinzani ni watu wa system mfano dk slaa, lipumba ,lowassa ,mrema, nk na hata huyo mbowe kwa hiyo mkuu kuwa Mpore usijaji watu
 
Lipo wazi hilo, alaf

u vijan wengi sijuhi hawajuhi au wanasahau kuwa ni LISSU ndio aliyeleta na kutoa ushahidi waq Zitto kuwa msaliti na ni yeye alishahuri afukuzwe kabla hajaenda mahakamani.

vijan hawasomi na wala, hawa ulizi kumbukumbu kabisa.

Namuomba tu asiingie kwenye mtego wa Zitto
 
Zitto ni mtu wa system na baadhi ya viongozi wote wa upinzani ni watu wa system mfano dk slaa, lipumba ,lowassa ,mrema, nk na hata huyo mbowe kwa hiyo mkuu kuwa Mpore usijaji watu
Kama ni hivyo kwanini wanawaogopa watu wa sysyem wenzao? Si kitu kimoja? Kama wana hofu hata uenyekiti wa serikali za mitaa kuwapa wenzao basi hao sio wenzao.
 
Chadema hii ya Mbowe na Mashinji inamuhitaji zaid Zitto kuliko Zitto anavyoihitaji CDM.
 
CHADEMA ni wa ajabu kweli, wanamuamini Sumaye ambae maisha yake yote alikuwa CCM, lakini hawamuamini Zitto ambae maisha yake yote ni upinzani, akili za wanachadema hazina tofauti na matope
 
Namuomba tu asiingie kwenye mtego wa Zitto

Hata hao wapinzani wenyewe sio makini kwa hivyo, kama walimpokea Lowassa na kumpa nafasi ya kugombea urais akiwa na miezi miwili ndani ya upinzani, kuna jipya hapo? Kuna ajabu gani Lissu akishirikiana na huyo Zitto ambaye kabaki kwenye upinzani muda wote, kuliko huyo Lowassa ambaye hajawahi hata kuwa mpinzani?
 
Hata hao wapinzani wenyewe sio makini kwa hivyo, kama walimpokea Lowassa na kumpa nafasi ya kugombea urais akiwa na miezi miwili ndani ya upinzani, kuna jipya hapo? Kuna ajabu gani Lissu akishirikiana na huyo Zitto ambaye kabaki kwenye upinzani muda wote, kuliko huyo Lowassa ambaye hajawahi hata kuwa mpinzani?

Zitto siyo mpinzani wa kweli tena
 
Zitto siyo mpinzani wa kweli tena

Uko sahihi, je Lowassa alikuwa mpinzani wa kweli mpaka kupewa nafasi na cdm kugombea urais akiwa na chini ya mwezi tu ndani ya cdm? Lete sababu nyingine ya kutomuamini huyo Zito.
 
Back
Top Bottom