Uhusiano wa wanasiasa na viongozi wa dini Tanzania; Ndege iliyobeba wakuu wa nchi kadhaa duniani

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
1574151626701.png
‘Viongozi wa nchi kadhaa duniani wanatembelea eneo fulani kwa kutumia ndege moja. Dakika chache baada ya ndege kuruka, unaibuka mjadala kati ya viongozi kutoka nchi za mashariki na wale wa nchi za magharibi. Mjadala unahama kidogo kidogo na kuchukua sura ya mvutano. Rubani anasikia kelele anahofia usalama wa ndege. Anatoka kwenye chumba cha kuongoza ndege na kwenda kuwatuliza abiria wake. Ikumbukwe kuwa rubani anapokuwa ndani ya ndege, yeye ndio mwenye uamuzi wa mwisho na nguvu kushinda mtu yoyote licha ya kwamba ndege inapotua amepoteza nguvu zake zote.

Rubani anawafikia abiria, badala ya kutuliza mvutano na kuweka mazingira ya wahusika kuzungumza kwa kusikilizana, anaamua kuungana na upande mmojawapo. Bila kujali upande alioungana nao uko sahihi kiasi gani; anajikuta amekuwa sehemu ya mvutano. Dakika kadhaa baadae, ndege inaanza kuyumba, anataka arudi kwenye chumba cha kuongozea ndege lakini kila akitaka kuondoka hawezi. Upande mmoja umemshika kulia mwingine kushoto na kila mmoja anavuta kwa nguvu zake zote. Fikiria ni nini kitaenda kutokea?'

Katika mfano wa hapo juu, haimaanishi kuwa hao wanaomvuta rubani hawana akili, au sio watu muhimu, au wamechoka maisha au wanavutiwa na kitakacho wapata, la! Inakuwa ni ‘confusion’ kuna mazingira mivutano ikiachwa ikifikia hatua fulani, wahusika wanaweza kushindwa kurudi kwenye hali ya kawaida hata kama wanatamani kurudi, wanashindwa kwa sababu ya ‘confusion’.

Viongozi wa dini angalau ndio watu wanaoweza kuwaunganisha wanasiasa wanaoshindwa kuelewana kwenye mambo kadhaa ya msingi ambayo maelewano ni muhimu. Viongozi wa dini wanaweza kuwaita na kuwaunganisha viongozi wa siasa ambao hawawezi kukutana wenyewe na kuzungumza kwa sababu mbalimbali.Hii ni kwa sababu katika eneo la imani, wao ndio wenye nguvu zaidi na wanaweza kusikilizwa.

Ni vyema yanapotokea mambo yenye utata viongozi wa dini wachukue nafasi ya upatanishi ‘Mediation’ ambapo moja ya nguzo kufanikiwa katika ‘mediation’, ni kuwa mtu wa kiasi na haki ili kuaminiwa na pande zote. Hatari ya kuchagua upande ni uwezekano wa kupoteza kuaminika na kushindwa kuziunganisha pande zinazohusika pale inapohitajika kufanya hivyo.

Vile vile tunawashauri viongozi wa kisiasa wasiwashawishi viongozi wa dini kuwa upande wao bali wawaache wawe ‘mediators’ pale inapobidi. Kwa jicho la haraka unaweza kudhani kwamba kuwashawishi kuwa upande wako ni jambo jema lakini ukweli ni kwamba ijapokuwa inaweza kukupa furaha ya muda lakini ni hatari kweli. Kuwashawishi kuwa upande wako ni sawa na kumshawishi rubani kwenye ndege awe upande wako wakati unavutana na abiria wenzako kwenye ndege (bila kujali uko sahihi au la!). Kama akikubali, janga litakalokuja kutokea hata wewe halitakucha.

Kama kuna atakayekereka na hoja hii basi anisamehe kwani sijalenga kumkwaaza. Nawashukuru sana kwa jinsi ambavyo mmeelewa.
 
Ukitaka kuelewa vizuri Zaidi jinsi jambo dogo linavyoweza kusababisha shida kubwa kwa sababu ya watu kutokuwa tayari kuzungumza au kutokuwa na miundombinu ya kuwaunganisha ili wazungumze na kukubaliana kwenye mambo ya msingi. Jiulize ni sababu gani zilisababisha mkasa wa Franz Frednand kupelekea vita ya dunia,? au Japani kuvamia Manchuria miaka ya 1938 na mkasa wa daraja la Marcopolo. Kimsingi mpaka sasa hakuna sababu za msingi zinazoweza kuelezeka ya watu kutozungumza.

Katika mazingira ambayo watu hawazungumzi na wanaishi pamoja, kikombe tu kilichowekwa juu ya kiti kinaweza kuleta balaa kubwa kila mtu akidhani kategeshewa na mwenzake, kumbe kaweka mtoto
 
Mnataka mpatanishwe kwa kutofautiana nini? Mkimaliza “kupatinishwa” muanze kumzodoa Rais kama mlivyokuwa mnafanya kwa JK ? Mmejaa chuki na mnajaribu kwa njia zote muisambaze hiyo chuki kwa wananchi ila mmeshindwa, hamna support kutoka kundi lolote la jamii.

Ni mwezi tu uliopita mlikuwa mnashangilia na kufurahia uzushi wenu kuwa JPM amefariki, Leo mnataka mpatanishwe , kwa ajili ya nini wanafiki wakubwa nyie, acha tuendelee na mdundo huu huu mwisho wa siku kila mtu ataheshimu sehemu yake.
 
Naomba utuambie kwa sasa Rubani ameungana na upande upi Nyakati zile za WARAKA Rubani alikuwa upande upi.
 
Mna….! unakusudia nini?

Halafu inapendeza ukawa unasoma mada ukaelewa kabla ya kuchangia
Umewakilisha kundi na sio mtu, hivyo ni mna....
Ukweli huko pale pale, imewauma kuona viongozi wa dini hawashangilii ujinga wenu, endelee na kamanda Askofu Shoo na kamanda Askofu Munga ambao wameshaonyesha chuki zao na mahaba yao kwa CDM.
 
Naomba utuambie kwa sasa Rubani ameungana na upande upi Nyakati zile za WARAKA Rubani alikuwa upande upi.
Mantiki sio sangapi rubani anaungana na upande upi, suala hapa ni rubani kutuliza mivutano nani ya ndege 'kidipomasia' kwa ajili ya usalama wa ndege na waliomo na ili hilo liwezekane rubani lazima awe na kiasi, na awe makini kujua ni kipi muhimu kwa wakati upi.
 
Kwa hapa tz naona viongozi wa dini wengi wamechagua upande wa wanyonyaji!!!wameacha misingi ya imani na kutetea ustawi wa waumini wao!wamekalia kimya utekaji na ukiukwaji wa haki za bina adamu!!!hadi mzee machinga wa mtwara katekwa ni siku ya nne hajapatikana!!!DIWANI ATHUMANI MKURUGENZI MPYA WA USALAMA UKO WAPI?TEKA TEKA INAENDELEA TENA KIMYA KIMYA SANA!WATEKAJI WANAKUJA USIKU WA MANANE !!!!!hadi jiwe aondoke atakuwa ameua na kutesa wengi!!!!NATOA WITO KWA VIONGOZI WA DINI WASOME ALBADIR NA KUSALI NOVENA ILI KUKOMESHA TEKA TEKA!NA WALE WALIOPOTEA WARUDI!!!TUOMBE PAMOJA!!!
 
Kuna kitu watu hamkielewi. Kususa ni hatua ya mwisho kwa wakristu. Kabla ya hapo kuna hatua lazima zifuatwe. Kwa ufupi, ni kuwa ukihisi ndugu yako amekukosea, wewe uliyekosewa ndo unawajibu wa kumfuata yule unayedhani amekukosea na kuanza harakati za usuluhishi. Akikusikia, umempata ndugu yako, akikataa unatafuta msuluhishi, akikataa na hapo ruksa kumsusia. Sasa watu mnatunga hadithi ndefu kumfundisha mbobezi wa mafundisho ya kimungu. Yuko sahihi kwa mafundisho ya kiimani.
 
Mtu anaweza kusema hakuna haja ya mazungumzo kwenye vitu vidogo vidogo, jambo la msingi kukumbuka ni kuwa mivutano yoyote mikubwa huwa inaanza na vitu vidogo vidogo. Baadae mazungumzo hayafanyiki au yana feli na kitu kidogo hukua.

Kutofautiana katika Maisha ni kitu cha kawaida ila katika mazingira ambayo watu hawazungumzi; jambo dogo tu liweza kuleta shida kubwa. Hii ni kwa sababu pande zinazotofautina zikiwa hazizungumzi, kila upande unakuwa una 'Exaggerate' tatizo.

Hata hivyo wakati Fulani 'Mediation' ni muhimu na kwa mazingira ya Tanzania, viongozi wa dini wangweza ku fit zaidi kucheza sehemu hiyo zaidi ya sehemu nyingine yoyote
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom