Uhusiano na nafasi za kuzaliwa

Uhusiano na nafasi za kuzaliwa

20PROFF

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2013
Posts
8,217
Reaction score
7,261
Habari zenu wanajamvi,

Uhusiano wa kawaida ambao unajengwa na jinsi mbili KE na ME, Umekuwa na changamoto kadhaa kwa watu kushindwa kujua jinsi ya ku deal na wenzao wao, kujua nani ni perfect match wake.

Tuangalie kwa ufupi jinsi nafasi zetu za kuzaliwa katika familia, hapa nitagawanya katika makundi yafuatayo.
1.First born (watoto wa kwanza), 2. Watoto wa kati (hawa ni ambao si wa kwanza wala wa mwisho), 3. Watoto wa mwisho (Last born), 4.One and only (ambao wamezaliwa peke yao kwao). Ngoja tucheki tabia zao kwa ufupi tukizihusianisha na mahusiano.

FIRST BORN, hawa wamekuwa katika nafasi za viongozi, wamekuwa wakipewa majukumu ya kuongoza wadogo zao na kuwalea pia sometimes kipindi ambacho wazazi hawapo. Hutegemewa kufanya maamuzi binafsi na huandaliwa kwa hilo ili kuweza kuwaweka walio chini yake katika mwelekeo sahihi. Wanakuwa na maamuzi ninafsi, hupenda kutoa hoja na kusikilizwa, hawapendi kupelekeshwa. Watu ambao wanajua sana kupenda na kudekeza.

LAST BORN, Hawa wamekuwa katika nafasi ya kuto wajibika sana katika familia, wamekuwa ni watu wakudeka kusubiri kufanyiwa na kupewa solution ya nin kifanyike. so ukikuta mtu kila kitu hawezi simama mwenyew na kuamua bila kusuasua hadi hapate ushauri au sapoti ya mtu, mara nyingi ni watu wa kundi hili, sio risk takers na ni wasikilizaji na wanaofanya wanayo ambiwa.

WAKATI KATI,Hawa hawatabiriki, wanakuwa wapo kati, wanaweza jisimamia, wanawez kupenda na kurudisha upendo pia, wadekaji wapo. Hawa wapo kati kama jina lao lilivyo.

One and only, hawa watoto wa pekee, hawanaga tofauti sana na wa kati kati, wanauwezo wa kucheza pande zote, wanapenda sana kupendwa hawapendi kusumbuliwa kutokana na jinsi walivyo kuzwa kwao

Sasa unachotakiwa kufanya ni kucheki nafasi yako na ya mpenzi wako then ujue jinsi ya kuishi nae, unaeza kuta una KE wako ni first born kwao so usione kama anakupanda kichwani akiwa ana pinga hoja zako, huyo anataka muende hoja kwa hoja na si kuperekeshana, kinyume na hapo hamto dumu. Au unakuta ME wako ni mzito kufanya maamuzi,kumbe ni last born na ni wagumu kutake risk, wew msome na jua jinsi ya kuashi nae.

IKIWA HIVI ITAPENDEZA ZAID

ME ni first born, mpenzi wake akawa last born ni perfect zaid, hata akiwa mwingine kwenye kundi hilo aina noma ila asiwa KE ambaye ni first born itakuwa daily majibizano.

KE first born, ajitafutie ka last born kake akapelembe, wataishi poa kabsa na kuenjoy uhusiao. Tena hapa ndo ukute KE kamzidi umri ME

ONE AND ONLY
, Akikutana na wa type yake itakuwa shida kidgo, vema akapata wa kundi jingine.

KATIKATI, hawa wanaweza match na yeyote yule
 
Mmmh....
Kuna malastborn wana majukumu mpaka utaogopa

Maana mafirstborn wamesepa wanajifanya majukumu hawayajui....
 
KE first born, ajitafutie ka last born kake
akapelembe, wataishi poa kabsa na kuenjoy
uhusiao. Tena hapa ndo ukute KE kamzidi umri
ME...mkuu umenena sana na hili jambo lazma nilifanyie kazi.
 
Mmmh....
Kuna malastborn wana majukumu mpaka utaogopa

Maana mafirstborn wamesepa wanajifanya majukumu hawayajui....

hapo nimeongelea kwa hali kawaida...hizo zingine ni excpetional
 
watu hata hawatabiriki japo najua mafirst born wana majukumu sana na wanakuaga wamekomaa kiakili baadhi yao ila kuna first born mmoja anadeka huyo utadhan ndo last hadi anakuwa mtoto wa mama...watu wa hivi hapana ni pasua kichwa kila kitu anashtaki kwa mama hata ukimnyima anapiga simu kwa mama...
 
watu hata hawatabiriki japo najua mafirst born wana majukumu sana na wanakuaga wamekomaa kiakili baadhi yao ila kuna first born mmoja anadeka huyo utadhan ndo last hadi anakuwa mtoto wa mama...watu wa hivi hapana ni pasua kichwa kila kitu anashtaki kwa mama hata ukimnyima anapiga simu kwa mama...
anawalakini huyo,aisee
 
Nimependa ulivyojenga "logic", kuna kaukweli hapa. Umeanzisha uzi mzuri ambao unaweza kuwapa baadhi ya watu (wale wanaopenda tafiti) kitu cha kutafiti kwa kina. Kwa kweli kula gwala kwa huu uzi.

Inawezekana ndiyo kuna "First-born" wadekaji au "Last-born" wenye majukumu, Dunia ndivyo ilivyo; haikosi upekee. Lakini kiuhalisia tunategemea maisha yao yawe kama ulivyoyaelezea mleta uzi. Ndiyo maana nakupa gwala.
 
watu hata hawatabiriki japo najua mafirst born wana majukumu sana na wanakuaga wamekomaa kiakili baadhi yao ila kuna first born mmoja anadeka huyo utadhan ndo last hadi anakuwa mtoto wa mama...watu wa hivi hapana ni pasua kichwa kila kitu anashtaki kwa mama hata ukimnyima anapiga simu kwa mama...

You have made my day.
 
watu hata hawatabiriki japo najua mafirst born wana majukumu sana na wanakuaga wamekomaa kiakili baadhi yao ila kuna first born mmoja anadeka huyo utadhan ndo last hadi anakuwa mtoto wa mama...watu wa hivi hapana ni pasua kichwa kila kitu anashtaki kwa mama hata ukimnyima anapiga simu kwa mama...
sijaelewa hio first au last borns anasemea jinsia gani. binafsi nilivyoshuhudia katika maisha yangu, binti yangu sitapendelea aolewe na mtu ambaye ni first born, labda kama mpango wa Mungu sitapinga. mwanaume first born, anakuwa mtoto wa mama kuliko mwanaume last born. kuna ndugu yangu mmoja, ameolewa na first born, huwezi amini, yeye ana uwezo biashara na viusafiri kadhaa, lakini jinsi ya kuendesha maisha lazima akashirikishe mama yake na baba yake, baba yake na mama yake ndio wanaocontrol familia na mkewe ni pambo tu pale. yeye walimsomesha ndiyo, akafanikiwa sasa its like wanataka wamfaidi mtoto wao kuliko mkewe kumfaidi matunda ya mafanikio. jambo hili mara nyingi nimeliona likitokea kwa mtoto wa kwanza kwasababu wazazi wanakuwa na expectations nyingiii kwa mtoto wa kwanza hasa kama ni wa kiume kuliko wale wanaomfuata, na mara nyingi huwa wanampenda sanaa kuliko...jambo hili huwa linavunja hata ndoa.

however, inasemekana watoto wa kwanza ndio huwa watafutaji kuliko. nimeongelea experience niliyoiona kwa dada yangu, ambayo naamini doesn't apply to every man.

mimi binafsi vilevile, ni mtoto mwisho, lakini kutokana na kwamba kwetu peke yangu ndio nimefanikiwa zaidi kimaisha, rundo loote toka juu waliotangulia kuzaliwa wananiangalia mimi jambo ambalo sikumbuki lini niliwahi kudeka....labda nilipokuwa primary school, lakini sijakaa na wazazi tangu nilipomaliza primary nikiwa 14yrs, nikaanza kutafuta pesa hata kwa kutumikishwa kazi ngumu na za kinyonyaji hadi nilipokuja kusimama na kufanikiwa, nikaoa na kuwa na maisha mazuri. , jambo linalonifanya nipinge kwamba sio watoto wote wa mwisho wanadeka na hawafanikiwi, katika kila general rule huwa kuna kuwa na exceptions.
 
Haya uliyoaandika yapo dhahiri...si jambo jipya
 
Back
Top Bottom