Uhamiaji na Wavaa kaptula na Jeans

Uhamiaji na Wavaa kaptula na Jeans

Mr Bean.

Senior Member
Joined
Jan 25, 2015
Posts
185
Reaction score
133
Wadau nipo hapa uhamiaji nimezuiwa na walinzi wa getini kwamba siwezi ingia nikiwa nimevaa kaptula al maarufu pensi. Nikiwa nimekaa hapo nje ya geti natafakari nikawaona mzungu mmoja na mkewe nimesema mkewe kwasababu kwajinsi walivyokuwa wamekaribiana japo wenzetu ni ngumu kutofautisha mtu na bintie.

Sasa kilichonishangaza ni hao wazungu wa kuruhusiwa kuingia tena bora ya huyo wa kiume huyo wa kike naweza sema alivaa kichupi. Wakati bado naendelea kutafakari nikaambiwa kwamba hata ukija umevaa jeans huruhusiwi kuingia uhamiaji.

Wadau hii imekaaje?.
 
labda walinzi walijua wewe ni afisa uhamiaji. si unajua ukilewa ukaingia bungeni, unatumbuliwa?
 
hahaha kuna mambo ukifikiria sana unaweza kuichukia nchi yako. Nakumbuka niliendaga Zanzibar tukawa tunapiga picha bustani ya forodhani wakatokea weusi wenzetu wakasema haituhusiwi kupiga picha bila kibali.
 
Sasa unaweza kwenda huko kwao hao wakoloni/wazungu ulaya na wewe ukifika vaa kama wao utembee unavoweza, nahisi utainekana kituko, maana siyo culture yako.

Wao wanavaa hivo kutokana na mazingira na hali ya hewa ilivyo.
 
Kuna muandishi mmoja anaitwa Frantz Fanon aliandika ktabu kinaitwa wretched of the earth ,tafsiri yake ni ''viumbe waliolaaniwa''.Yeye alitanabaisha kuwa waafrika tunalaumu Wazungu kuwa wanatubagua,lakini ukweli ni kuwa ni sisi ndio tunaojibagua na kutoa mwanya kwao waendelee kutubagua.Mwisho wa kunukuu
 
kaka hii inanikumbusha kuna wakati natoka nairobi na ndege ya jioni kwenda zanzibar,na nilifika zanzibar kama saa 3 za usiku, wakati nafika pale nilishangaa mie ilibidi niitwe pembeni nifungue kila kitu kilichokuwa kwenye begi langu wapekue na wazungu walikuwa wanapita tu hata hawaulizwi, nikawauliza mbona wale wana mabegi makubwa kuliko langu hamuwakagui na hamuwaulizi, nikapewa jibu kuwa usitufundishe kazi, hilo jibu lilinikera sana nikaanza kuwa mkali na mie mpaka bosi wao akaja nikaambiwa niende zangu manake hao wazungu walikuwa washaanza shangaa kulikoni, ni kweli ubaguzi tunao sisi kwa sisi wala sio kulaumu wazungu
 
Acha bana sio kwa wote mbona mimi nimeongia apo mara nyingi tu nikiwa na kaptala or jeans labda wamekuhisi vibaya bt si kweli kua kuna mavazi maalumu yakuingia apo
 
Siku hizi ofisi za umma ili uhudumie au uruhusiwe kuingia ndani lazima uwe umevaa mavazi ya staha ambayo wameyabandika kwenye mbao za matangazo. Wameonyesha mavazi yanayofaa na yasio faa. Ila ilibidi itumike kwa watu wote sio kibaguzi kama alivyofanyiwa mleta mada
 
hahaha kuna mambo ukifikiria sana unaweza kuichukia nchi yako. Nakumbuka niliendaga Zanzibar tukawa tunapiga picha bustani ya forodhani wakatokea weusi wenzetu wakasema haituhusiwi kupiga picha bila kibali.

Mi nikisikia mtu anaenda Zanzibar huwa namuonea huruma. Nimeenda mara moja nikabaguliwa, siendi tena.
 
Siku hizi ofisi za umma ili uhudumie au uruhusiwe kuingia ndani lazima uwe umevaa mavazi ya staha ambayo wameyabandika kwenye mbao za matangazo. Wameonyesha mavazi yanayofaa na yasio faa. Ila ilibidi itumike kwa watu wote sio kibaguzi kama alivyofanyiwa mleta mada

Ni sawa tu, sisi sio utamaduni wetu na wao ni sawa kwao kwani hawana tofauti na wanyama.
 
Ni kweli uhamiaji wanakataza mi nilienda pale MWAKA jana nimevaa suruali nikazuiliwa kuigwa wakasema kama nataka mlinzi wa pale getini alikuwa mdada angeniazima kanga nijifunge ndio niingiie uzuri nilikuwa na mume Wangu na tulikuwa tunahitaji forms tu. Ikabidi mi nibaki ye ndo aende kuzichukua. Na kuhusu ubaguzi hii tabia jamani imekithiri Sana na saa nyingine mtu anakuangalia kama una mwonekano wa hela then asipouona tayari anaanza kukuletea dharau.
 
Zamani nilikuwa naona watu wanaenda ubalozi ni kuomba visa na suit eti kama hukuvaa suit Balozi atakuona masikini unaenda kutafuta maisha, sikukubaliana nalo, siku nilio kwenda wakati nahitaji hio visa, nilienda na pans tu, mbona sikukataliwa!

Kama mtu wa kawaida unaenda sehemu as customer u naweza kuvaa vyovyote as long sio uchi, huwendi kuomba kazi boss
 
Zamani nilikuwa naona watu wanaenda ubalozi ni kuomba visa na suit eti kama hukuvaa suit Balozi atakuona masikini unaenda kutafuta maisha, sikukubaliana nalo, siku nilio kwenda wakati nahitaji hio visa, nilienda na pans tu, mbona sikukataliwa!

Kama mtu wa kawaida unaenda sehemu as customer u naweza kuvaa vyovyote as long sio uchi, huwendi kuomba kazi boss
Ndugu unajua TOFAUTI ya uhamiaji na ubalozi (kuomba viza?) ama na wewe ulisoma chuo cha ushirika Moshi?
 
Ndugu unajua TOFAUTI ya uhamiaji na ubalozi (kuomba viza?) ama na wewe ulisoma chuo cha ushirika Moshi?
Mkuu ubalozi una tofauti gani na uhamiaji! Kazi zao ni similar, ,halafu, mbona huku zanzibar uhamiaji tunaingia na pakacha za tungule na pans ?
 
Mkuu ubalozi una tofauti gani na uhamiaji! Kazi zao ni similar, ,halafu, mbona huku zanzibar uhamiaji tunaingia na pakacha za tungule na pans ?
Ndugu inaelekea elimu yako ya kuunga unga huenda hata ndo umeanza FOUNDATION course kwenye chuo pale BWEJUU au KIBANDAMAITI.
 
Back
Top Bottom