Uhalisia wa Zuio la Bomoabomoa Dhidi ya Serikali

Uhalisia wa Zuio la Bomoabomoa Dhidi ya Serikali

Dragoon

JF-Expert Member
Joined
Nov 24, 2013
Posts
7,012
Reaction score
8,146
UHALISIA WA ZUIO LA BOMOABOMOA DHIDI YA SERIKALI

Hivi karibuni baadhi ya maeneo katika jiji la Dar es Salaam (hasa maeneo ya Kimara) kumekuwa na ubomoaji unaofanywa na serikali kupitia wakala wa barabara TANROADS dhidi ya makazi ya wananchi na kuibua manung’uniko na lawama za hapa na pale, wengine wakidai kuwa kuna kesi mahakamani na mahakama ilikwishatoa amri ya kuzuia ubomoaji huo. Kumeibuka kauli mbalimbali, wengine wakisema kuwa serikali imeingilia uhuru wa mahakama na kukiuka amri iliyotolewa na mahakama. Ifuatayo ni makala fupi kuhusiana na ni nini hasa inapaswa kutambulika kuwa amri yamahakama kuzui bomoabomoa mahali popote pale.

Wapo wanaodai kuna zuio na walioonesha karatazi zilizoandikwa Stop Order wakisema kuwa ndio amri halali ya Mahakama. Nitatoa ufafanuzi wa hivi vitu viweli, Stop Order na Amri ya Zuio.

Stop Order

Mwandishi Bryan A. Garner Katika kamusi ya misamiati ya kisheria Black’ law Dictionary, 8th edition anatoa maana ya neno Stop order:

“Order that suspends a registration statement containing false, incomplete, or misleading information…. A bank customer’s order instructing the bank not to honor one of the customers’ checks – also termed stop payment order. …An order to buy or sell when the security’s price reaches a specified level (the stop price) on the market…”

Msamiati Stop order umetajwa katika baadhi ya sheria za Tanzania. Msamiati huu unajitokeza katika sura na. 323 ya sheria za Tanzania (The Forest Act) na hauhusiani vyovyote na kesi za madai na ubomoaji kupisha miradi ya serikali. Pia msamiati Stop Order unajitokeza katika by-laws za sura ya 269 za sheria za Tanzania (The Archtects and Quantity Surveryors (Registration) Act By-Laws). Hii inajitokeza katika kanuni ya 113 na haihusiani na masuala ya bomoabomoa au amri za mahakama.

Msamiati huu pia upo katika sura ya 322 ya sheria za Tanzania (The Police Force and Auxiliary Serivices Act) katika kifungu namba 43. Zaidi msamiati huu unapatikana katika sura ya 258 ya sheria za Tanzania (The Political Parties Act) kifungu cha 11. Sura Na 394 ya sheria za Tanzania (the Insurance Act) pia ina msamiati Stop Order, katiaka kifungu na. 101.

Zaidi ya hapo msamiati huu hauonekani katika sheria zingine Tanzania ikiwemo ile inayotoa msingi wa Kuzia tendo fulani lisifanyike au kushinikiza kufanyika kwa jambo fulani (injunction) ambayo ni sura ya 33 ya sheria za Tanzania. Sheria hii ndiyo inayotoa Amri ya zuio ambayo ndio ingefaa kuzuia bomoabomoa inayolalamikiwa.

Stop Order inaweza tolewa kwa mtu binafsi au taasisi binafsi kama vile kampuni pale tu itakabodhihirika kuwa mtu huyo au taasisi hiyo haina mamlaka kisheria kufanya shugghuli pale au kuhodhi eneo lile. (The Town Director v Daniel Sekao 1988 TLR 22 (HC))

Amri ya Zuio (Temporary Injunction)

Amri ya zuio ama injuction ni zao la litokanalo na taratibu zilizoanzia uingereza, na Kesi iliyoweka misingi wa zuio hili ni kesi ya American Cyanamid Co. v Ethicon Ltd ([1975] AC 396; [1975] 1 ALL ER 504). Katika kutoa zuio hili, mahakama huangalia vigezo vitatu muhimu (baadhi ya kesi huongeza kingine na kuwa vinne). Kwa Tanzania amri hii hutolewa chini ya kifungu cha 68 na O. XXXVII ya sura ya 33 ya sheria za Tanzania (the Civil Procedure Code).

Hili ni zuio ambalo hutolewa na mahakama kuzuia upande wa pili wa wadaawa kufanya jambo au kulazimisha kufanya jambo kwa kipindi kesi ya msingi ikiendelea au hadi pale mahakama itakavyoamua vinginevyo. Amri hii ya zuio ni nusu ya hukumu na inafanya kazi kama vile hukumu ya kesi ya msingi ilishatolewa, hadi pale mahakama itakapotoa amri nyingine tofauti. Mwandishi msomi Sohoni katika kitabu chake SOHONI'S LAW OF INJUNTIONS, 2nd Edition ukurasa 67 anaandika:

“As such, an injunction is in its operation, somewhat like judgment and execution before trial, it is only to be resorted to from a pressing necessity, to avoid injurious consequences which cannot be repaired under any standard of compensation…. an application for an Injunction is an appeal to the Court, and the plaintiff is bound to make out a case showing a clear necessary for its exercise, it being the duty of the courts rather to protect acknowledged rights than to establish new and doubtful cases. Moreover, a temporary injunction is a restrictive or prohibitory process designed to compel the party against whom it is granted to maintain his Status merely, until the matter in dispute shall by due process of the courts be determined.”

Amri ya Zuio haitolewi na haifanyi kazi kwa mtu au taasisi isiyokuwa moja ya wadaawa katika kesi ya msingi (National Bank of Commerce v Dar es Salaam Education and Office Stationery 1995 TLR 272 (CA)).

Tofauti kati ya Stop Order na Injunction (Amri ya Zuio)

Kwa hiyo basi, Stop order na Amri ya Zuio ni vitu viwili tofauti vitokanavyo na misingi tofauti ya kisheria. Wakati stop order ni zao la sheria Huru (substantive law) Amri ya zuio ni zao la sheria za kiutaratibu (Procedural Law). Stop Order inaweza kutolewa na mtu yeyote au mamlaka yeyote lakini amri ya Zuio inatolewa na Mahakama Pekee. Wakati Stop order ina asili ya kushinikiza utii wa kanuni zilizopo kwa mujibu wa sheria, Amri ya zuio in asili ya hukumu itokayo kabla ya kesi ya msingi haijasikilizwa, huku ikizingatia usumbufu na haki kufurahia mali baina ya wadaawa. Stop order haizingatii uwiano wa manufaa (balance of convenience) lakini Amri ya Zuio siku zote huzingatia uwiano wa manufaa baina ya wadaawa. Pia Stop Order inaweza tolewa baina ya watu au taasisi zisizo na mahusiano ya kimkataba au kiutendaji, wakati Amri ya zuio hutolewa baina ya pande zilizo katika mgogoro pekee. Stop orders hutolewa pasopo taratibu za kusikilizwa katika misingi ya kesi za madai (on preponderance of evidence) wakati Amri ya zuio usikilizwaji lazima ufanyike. Vilevile Stop Order inatoa wasaa kwa mhusika kukata rufaa dhidi ya order hiyo, wakati Amri ya Zuio haitoi wasaa wa kukatiwa rufaa (Hardmore Productions Ltd. and Others v. Hammilton And Another, [1983] 1 A.C 191, - Diplock, L.J., angalia pia Gazelle Tracker Limited v Tanzania Petroleum Development Corporation Civil Application no. 15 of 2006 (CAT, unreported)).

Hatua za kufuatwa katika Amri ya Zuio

Baada mmoja wa wadawa kuomba amri ya Zuio katika mahakama yenye mamlaka, ombi hilo husikilizwa (ikumbukwe kuwa maombi haya huwekwa mbele ya mahakama pale ambapo kesi ya msingi ilishafunguliwa). Mahakama ikishajiridisha kwa kuzingatia vigezo vinne vikuu, hutoa amri ya kuzui kutendeka kwa jambo fulani (prohibitive/restrictive injuction) au kulazimisha kufanya jambo fulani (mandatory injunction). Amri hii ikishatolewa (interim decree) hutolewa kwa mfumo wa drawn orders na wadaawa wote hupewa service ya hizi orders.

Amri za Zuio hazitakiwi kuwekwa kwenye mbao za matangazo au eneo husika ili kuzuia kitendo fulani kisifanyike. Hii si dhamira ya Amri hizi. Dhamira ya amri hizi ni kushinikiza ukaziaji wa “hukumu” iliyotolewa kabla ya uamuzi wa mwisho wa kesi ya msingi (ndio maana ya kuitwa temporary injunction). Kwa hiyo kama mmoja wa wadaawa hakuwepo siku amri hizi zinatolewa na mahakama upande ulioomba amri hizi unalazimika kumtafuta mdaawa aliyelengwa na amri hizi na kumpatia (serve).

Ukweli kuhusu kitu kinachotolewa kwa jina la Stop Order

Mahakama ina maafisa wa ngazi mbalimbali, ukianzia na makarani, mahakimu, mawakili, wasajili na majaji. Mahakama inapota amri (katika hukumu yake) hutoa kitu kinachoitwa decree (extracted decree or drawn orders). Hakimu au jaji mara nyingi hajihusishi na kuandika (extract) decree hizi. Makarani na wasajili hufanya hii kazi na hakimu au jaji ataweka saini yake baada ya kuandikwa kwa decree.

Iwapo mahakama imetoa amri yake ya zuio kutokana na sura ya 33 ya sheria za nchi (O. XXXVII) hakuna kitu kinachotakiwa kutolewa kinaitwa Stop order, hata kama chini yake itajitokeza saini ya jaji au hakimu. Watumishi wa Mahakama hasa makarani wamekuwa si wajuzi wa taratibu za kisheria kwa hiyo kwa namna moja au nyingine wanaweza kuandaa kitu kimeandikwa stop order na mamlaka husika ikaweka saini yake kwa kupitiwa. Kama kitu hiki kinajitokeza basi nyaraka hii inakuwa ni batili katika misingi ya sheria.

Baadhi ya mawakili, ama kwa kutojua au kwa kuhadaa wateja wao mamekuwa na mtindo wa kuandika vitu kama hivi pia wakinuia kutoa zuio linalotolewa na kisheria kwa mujibu wa sura ya 33 ya sheria za nchi. Kitu kama hiki ni batili pia.

Amri ya zuio na inayotumika kuzuia mtu, taasisi au serikali ni ile ambayo msingi wake unaanzia kwenye kesi yenyewe iliyoko mahakamani. Waathirika au wadaawa walalamikaji wanaweka maombi ya zuio mbele ya mahakama kwa kutumia fomu maalumu (chamber summons) na mahakama hupanga siku ya kusikiliza maombi hayo. Maombi lazima yasikilizwe na mahakama itoe uamuzi juu ya maombi hayo.

UHURU WA MAHAKAMA HAUJAINGILIWA

Kufuatana na hali hii ni wazi kuwa mahakama haijatoa Amri yoyote kuzuia bomoabomoa. Pia serikali au mamlaka yeyote ya serikali haikuvunja amri halali ya mahakama. Kwa hali hiyo basi uhuru wa mahakama umebaki imara kwa mujibu wa Ibara ya 107B ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

NINI KIFANYIKE

Elimu mahsusi itolewe kwa umma kuhusiana na uhuru wa mahakama na namna unavyokuwa. Wananchi waelimishwe ni kwa jinsi gani na misingi ipi mahakama inatoa Amri ya Zuio. Mawakili wawe wakweli kwa wateja wao na wasaidiane na serikali kutoa elimu husiaka. Maofisa wa mahakama hasa makarani wapewe elimu juu ya amri hizi, ikiwemo namna ya kuziandaa na mipaka iwekwe katika mamlaka inayotakiwa kutoa amri hizi. Pia umma ueleweshwe kubainisha order zinazotolewa na mahakama ikiwa katika muendelezo wa usikilizwaji kesi (mfano maintenance of status quo) na amri za stop/stay of execution.
 
UHALISIA WA ZUIO LA BOMOABOMOA DHIDI YA SERIKALI

Hivi karibuni baadhi ya maeneo katika jiji la Dar es Salaam (hasa maeneo ya Kimara) kumekuwa na ubomoaji unaofanywa na serikali kupitia wakala wa barabara TANROADS dhidi ya makazi ya wananchi na kuibua manung’uniko na lawama za hapa na pale, wengine wakidai kuwa kuna kesi mahakamani na mahakama ilikwishatoa amri ya kuzuia ubomoaji huo. Kumeibuka kauli mbalimbali, wengine wakisema kuwa serikali imeingilia uhuru wa mahakama na kukiuka amri iliyotolewa na mahakama. Ifuatayo ni makala fupi kuhusiana na ni nini hasa inapaswa kutambulika kuwa amri yamahakama kuzui bomoabomoa mahali popote pale.

Wapo wanaodai kuna zuio na walioonesha karatazi zilizoandikwa Stop Order wakisema kuwa ndio amri halali ya Mahakama. Nitatoa ufafanuzi wa hivi vitu viweli, Stop Order na Amri ya Zuio.

Stop Order

Mwandishi Bryan A. Garner Katika kamusi ya misamiati ya kisheria Black’ law Dictionary, 8th edition anatoa maana ya neno Stop order:

“Order that suspends a registration statement containing false, incomplete, or misleading information…. A bank customer’s order instructing the bank not to honor one of the customers’ checks – also termed stop payment order. …An order to buy or sell when the security’s price reaches a specified level (the stop price) on the market…”

Msamiati Stop order umetajwa katika baadhi ya sheria za Tanzania. Msamiati huu unajitokeza katika sura na. 323 ya sheria za Tanzania (The Forest Act) na hauhusiani vyovyote na kesi za madai na ubomoaji kupisha miradi ya serikali. Pia msamiati Stop Order unajitokeza katika by-laws za sura ya 269 za sheria za Tanzania (The Archtects and Quantity Surveryors (Registration) Act By-Laws). Hii inajitokeza katika kanuni ya 113 na haihusiani na masuala ya bomoabomoa au amri za mahakama.

Msamiati huu pia upo katika sura ya 322 ya sheria za Tanzania (The Police Force and Auxiliary Serivices Act) katika kifungu namba 43. Zaidi msamiati huu unapatikana katika sura ya 258 ya sheria za Tanzania (The Political Parties Act) kifungu cha 11. Sura Na 394 ya sheria za Tanzania (the Insurance Act) pia ina msamiati Stop Order, katiaka kifungu na. 101.

Zaidi ya hapo msamiati huu hauonekani katika sheria zingine Tanzania ikiwemo ile inayotoa msingi wa Kuzia tendo fulani lisifanyike au kushinikiza kufanyika kwa jambo fulani (injunction) ambayo ni sura ya 33 ya sheria za Tanzania. Sheria hii ndiyo inayotoa Amri ya zuio ambayo ndio ingefaa kuzuia bomoabomoa inayolalamikiwa.

Stop Order inaweza tolewa kwa mtu binafsi au taasisi binafsi kama vile kampuni pale tu itakabodhihirika kuwa mtu huyo au taasisi hiyo haina mamlaka kisheria kufanya shugghuli pale au kuhodhi eneo lile. (The Town Director v Daniel Sekao 1988 TLR 22 (HC))

Amri ya Zuio (Temporary Injunction)

Amri ya zuio ama injuction ni zao la litokanalo na taratibu zilizoanzia uingereza, na Kesi iliyoweka misingi wa zuio hili ni kesi ya American Cyanamid Co. v Ethicon Ltd ([1975] AC 396; [1975] 1 ALL ER 504). Katika kutoa zuio hili, mahakama huangalia vigezo vitatu muhimu (baadhi ya kesi huongeza kingine na kuwa vinne). Kwa Tanzania amri hii hutolewa chini ya kifungu cha 68 na O. XXXVII ya sura ya 33 ya sheria za Tanzania (the Civil Procedure Code).

Hili ni zuio ambalo hutolewa na mahakama kuzuia upande wa pili wa wadaawa kufanya jambo au kulazimisha kufanya jambo kwa kipindi kesi ya msingi ikiendelea au hadi pale mahakama itakavyoamua vinginevyo. Amri hii ya zuio ni nusu ya hukumu na inafanya kazi kama vile hukumu ya kesi ya msingi ilishatolewa, hadi pale mahakama itakapotoa amri nyingine tofauti. Mwandishi msomi Sohoni katika kitabu chake SOHONI'S LAW OF INJUNTIONS, 2nd Edition ukurasa 67 anaandika:

“As such, an injunction is in its operation, somewhat like judgment and execution before trial, it is only to be resorted to from a pressing necessity, to avoid injurious consequences which cannot be repaired under any standard of compensation…. an application for an Injunction is an appeal to the Court, and the plaintiff is bound to make out a case showing a clear necessary for its exercise, it being the duty of the courts rather to protect acknowledged rights than to establish new and doubtful cases. Moreover, a temporary injunction is a restrictive or prohibitory process designed to compel the party against whom it is granted to maintain his Status merely, until the matter in dispute shall by due process of the courts be determined.”

Amri ya Zuio haitolewi na haifanyi kazi kwa mtu au taasisi isiyokuwa moja ya wadaawa katika kesi ya msingi (National Bank of Commerce v Dar es Salaam Education and Office Stationery 1995 TLR 272 (CA)).

Tofauti kati ya Stop Order na Injunction (Amri ya Zuio)

Kwa hiyo basi, Stop order na Amri ya Zuio ni vitu viwili tofauti vitokanavyo na misingi tofauti ya kisheria. Wakati stop order ni zao la sheria Huru (substantive law) Amri ya zuio ni zao la sheria za kiutaratibu (Procedural Law). Stop Order inaweza kutolewa na mtu yeyote au mamlaka yeyote lakini amri ya Zuio inatolewa na Mahakama Pekee. Wakati Stop order ina asili ya kushinikiza utii wa kanuni zilizopo kwa mujibu wa sheria, Amri ya zuio in asili ya hukumu itokayo kabla ya kesi ya msingi haijasikilizwa, huku ikizingatia usumbufu na haki kufurahia mali baina ya wadaawa. Stop order haizingatii uwiano wa manufaa (balance of convenience) lakini Amri ya Zuio siku zote huzingatia uwiano wa manufaa baina ya wadaawa. Pia Stop Order inaweza tolewa baina ya watu au taasisi zisizo na mahusiano ya kimkataba au kiutendaji, wakati Amri ya zuio hutolewa baina ya pande zilizo katika mgogoro pekee. Stop orders hutolewa pasopo taratibu za kusikilizwa katika misingi ya kesi za madai (on preponderance of evidence) wakati Amri ya zuio usikilizwaji lazima ufanyike. Vilevile Stop Order inatoa wasaa kwa mhusika kukata rufaa dhidi ya order hiyo, wakati Amri ya Zuio haitoi wasaa wa kukatiwa rufaa (Hardmore Productions Ltd. and Others v. Hammilton And Another, [1983] 1 A.C 191, - Diplock, L.J., angalia pia Gazelle Tracker Limited v Tanzania Petroleum Development Corporation Civil Application no. 15 of 2006 (CAT, unreported)).

Hatua za kufuatwa katika Amri ya Zuio

Baada mmoja wa wadawa kuomba amri ya Zuio katika mahakama yenye mamlaka, ombi hilo husikilizwa (ikumbukwe kuwa maombi haya huwekwa mbele ya mahakama pale ambapo kesi ya msingi ilishafunguliwa). Mahakama ikishajiridisha kwa kuzingatia vigezo vinne vikuu, hutoa amri ya kuzui kutendeka kwa jambo fulani (prohibitive/restrictive injuction) au kulazimisha kufanya jambo fulani (mandatory injunction). Amri hii ikishatolewa (interim decree) hutolewa kwa mfumo wa drawn orders na wadaawa wote hupewa service ya hizi orders.

Amri za Zuio hazitakiwi kuwekwa kwenye mbao za matangazo au eneo husika ili kuzuia kitendo fulani kisifanyike. Hii si dhamira ya Amri hizi. Dhamira ya amri hizi ni kushinikiza ukaziaji wa “hukumu” iliyotolewa kabla ya uamuzi wa mwisho wa kesi ya msingi (ndio maana ya kuitwa temporary injunction). Kwa hiyo kama mmoja wa wadaawa hakuwepo siku amri hizi zinatolewa na mahakama upande ulioomba amri hizi unalazimika kumtafuta mdaawa aliyelengwa na amri hizi na kumpatia (serve).

Ukweli kuhusu kitu kinachotolewa kwa jina la Stop Order

Mahakama ina maafisa wa ngazi mbalimbali, ukianzia na makarani, mahakimu, mawakili, wasajili na majaji. Mahakama inapota amri (katika hukumu yake) hutoa kitu kinachoitwa decree (extracted decree or drawn orders). Hakimu au jaji mara nyingi hajihusishi na kuandika (extract) decree hizi. Makarani na wasajili hufanya hii kazi na hakimu au jaji ataweka saini yake baada ya kuandikwa kwa decree.

Iwapo mahakama imetoa amri yake ya zuio kutokana na sura ya 33 ya sheria za nchi (O. XXXVII) hakuna kitu kinachotakiwa kutolewa kinaitwa Stop order, hata kama chini yake itajitokeza saini ya jaji au hakimu. Watumishi wa Mahakama hasa makarani wamekuwa si wajuzi wa taratibu za kisheria kwa hiyo kwa namna moja au nyingine wanaweza kuandaa kitu kimeandikwa stop order na mamlaka husika ikaweka saini yake kwa kupitiwa. Kama kitu hiki kinajitokeza basi nyaraka hii inakuwa ni batili katika misingi ya sheria.

Baadhi ya mawakili, ama kwa kutojua au kwa kuhadaa wateja wao mamekuwa na mtindo wa kuandika vitu kama hivi pia wakinuia kutoa zuio linalotolewa na kisheria kwa mujibu wa sura ya 33 ya sheria za nchi. Kitu kama hiki ni batili pia.

Amri ya zuio na inayotumika kuzuia mtu, taasisi au serikali ni ile ambayo msingi wake unaanzia kwenye kesi yenyewe iliyoko mahakamani. Waathirika au wadaawa walalamikaji wanaweka maombi ya zuio mbele ya mahakama kwa kutumia fomu maalumu (chamber summons) na mahakama hupanga siku ya kusikiliza maombi hayo. Maombi lazima yasikilizwe na mahakama itoe uamuzi juu ya maombi hayo.

UHURU WA MAHAKAMA HAUJAINGILIWA

Kufuatana na hali hii ni wazi kuwa mahakama haijatoa Amri yoyote kuzuia bomoabomoa. Pia serikali au mamlaka yeyote ya serikali haikuvunja amri halali ya mahakama. Kwa hali hiyo basi uhuru wa mahakama umebaki imara kwa mujibu wa Ibara ya 107B ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

NINI KIFANYIKE

Elimu mahsusi itolewe kwa umma kuhusiana na uhuru wa mahakama na namna unavyokuwa. Wananchi waelimishwe ni kwa jinsi gani na misingi ipi mahakama inatoa Amri ya Zuio. Mawakili wawe wakweli kwa wateja wao na wasaidiane na serikali kutoa elimu husiaka. Maofisa wa mahakama hasa makarani wapewe elimu juu ya amri hizi, ikiwemo namna ya kuziandaa na mipaka iwekwe katika mamlaka inayotakiwa kutoa amri hizi. Pia umma ueleweshwe kubainisha order zinazotolewa na mahakama ikiwa katika muendelezo wa usikilizwaji kesi (mfano maintenance of status quo) na amri za stop/stay of execution.



Kenge
 
Umeandika mavi kabisa wewe mbumbumbu wa sheria. Hukumu ya mahakama ipo halafu wewe kenge unaleta kitita cha notes kuelezea stop order badala ya kurejea hukumu ya mahakama kuhusu uhalali wa zile nyumba. Wewe kama Una degree ya sheria basi Ni degree ya chupi
Kesi za uhalali wa nyumba ni kesi tofauti kabisa na kinachozungumziwa hapa, na bado kesi nyingi ziko mahakamani zinasikilizwa. Cha mhumu uliza kwa nini wanabomolewa.
Vilevile hiyo hukumu ya uhalali wa nyumba ilete hapa. Ni nani aliyesema kuwa wanaobomolewa si wamiliki halali wa maeneo yale?
 
UHALISIA WA ZUIO LA BOMOABOMOA DHIDI YA SERIKALI

Hivi karibuni baadhi ya maeneo katika jiji la Dar es Salaam (hasa maeneo ya Kimara) kumekuwa na ubomoaji unaofanywa na serikali kupitia wakala wa barabara TANROADS dhidi ya makazi ya wananchi na kuibua manung’uniko na lawama za hapa na pale, wengine wakidai kuwa kuna kesi mahakamani na mahakama ilikwishatoa amri ya kuzuia ubomoaji huo. Kumeibuka kauli mbalimbali, wengine wakisema kuwa serikali imeingilia uhuru wa mahakama na kukiuka amri iliyotolewa na mahakama. Ifuatayo ni makala fupi kuhusiana na ni nini hasa inapaswa kutambulika kuwa amri yamahakama kuzui bomoabomoa mahali popote pale.

Wapo wanaodai kuna zuio na walioonesha karatazi zilizoandikwa Stop Order wakisema kuwa ndio amri halali ya Mahakama. Nitatoa ufafanuzi wa hivi vitu viweli, Stop Order na Amri ya Zuio.

Stop Order

Mwandishi Bryan A. Garner Katika kamusi ya misamiati ya kisheria Black’ law Dictionary, 8th edition anatoa maana ya neno Stop order:

“Order that suspends a registration statement containing false, incomplete, or misleading information…. A bank customer’s order instructing the bank not to honor one of the customers’ checks – also termed stop payment order. …An order to buy or sell when the security’s price reaches a specified level (the stop price) on the market…”

Msamiati Stop order umetajwa katika baadhi ya sheria za Tanzania. Msamiati huu unajitokeza katika sura na. 323 ya sheria za Tanzania (The Forest Act) na hauhusiani vyovyote na kesi za madai na ubomoaji kupisha miradi ya serikali. Pia msamiati Stop Order unajitokeza katika by-laws za sura ya 269 za sheria za Tanzania (The Archtects and Quantity Surveryors (Registration) Act By-Laws). Hii inajitokeza katika kanuni ya 113 na haihusiani na masuala ya bomoabomoa au amri za mahakama.

Msamiati huu pia upo katika sura ya 322 ya sheria za Tanzania (The Police Force and Auxiliary Serivices Act) katika kifungu namba 43. Zaidi msamiati huu unapatikana katika sura ya 258 ya sheria za Tanzania (The Political Parties Act) kifungu cha 11. Sura Na 394 ya sheria za Tanzania (the Insurance Act) pia ina msamiati Stop Order, katiaka kifungu na. 101.

Zaidi ya hapo msamiati huu hauonekani katika sheria zingine Tanzania ikiwemo ile inayotoa msingi wa Kuzia tendo fulani lisifanyike au kushinikiza kufanyika kwa jambo fulani (injunction) ambayo ni sura ya 33 ya sheria za Tanzania. Sheria hii ndiyo inayotoa Amri ya zuio ambayo ndio ingefaa kuzuia bomoabomoa inayolalamikiwa.

Stop Order inaweza tolewa kwa mtu binafsi au taasisi binafsi kama vile kampuni pale tu itakabodhihirika kuwa mtu huyo au taasisi hiyo haina mamlaka kisheria kufanya shugghuli pale au kuhodhi eneo lile. (The Town Director v Daniel Sekao 1988 TLR 22 (HC))

Amri ya Zuio (Temporary Injunction)

Amri ya zuio ama injuction ni zao la litokanalo na taratibu zilizoanzia uingereza, na Kesi iliyoweka misingi wa zuio hili ni kesi ya American Cyanamid Co. v Ethicon Ltd ([1975] AC 396; [1975] 1 ALL ER 504). Katika kutoa zuio hili, mahakama huangalia vigezo vitatu muhimu (baadhi ya kesi huongeza kingine na kuwa vinne). Kwa Tanzania amri hii hutolewa chini ya kifungu cha 68 na O. XXXVII ya sura ya 33 ya sheria za Tanzania (the Civil Procedure Code).

Hili ni zuio ambalo hutolewa na mahakama kuzuia upande wa pili wa wadaawa kufanya jambo au kulazimisha kufanya jambo kwa kipindi kesi ya msingi ikiendelea au hadi pale mahakama itakavyoamua vinginevyo. Amri hii ya zuio ni nusu ya hukumu na inafanya kazi kama vile hukumu ya kesi ya msingi ilishatolewa, hadi pale mahakama itakapotoa amri nyingine tofauti. Mwandishi msomi Sohoni katika kitabu chake SOHONI'S LAW OF INJUNTIONS, 2nd Edition ukurasa 67 anaandika:

“As such, an injunction is in its operation, somewhat like judgment and execution before trial, it is only to be resorted to from a pressing necessity, to avoid injurious consequences which cannot be repaired under any standard of compensation…. an application for an Injunction is an appeal to the Court, and the plaintiff is bound to make out a case showing a clear necessary for its exercise, it being the duty of the courts rather to protect acknowledged rights than to establish new and doubtful cases. Moreover, a temporary injunction is a restrictive or prohibitory process designed to compel the party against whom it is granted to maintain his Status merely, until the matter in dispute shall by due process of the courts be determined.”

Amri ya Zuio haitolewi na haifanyi kazi kwa mtu au taasisi isiyokuwa moja ya wadaawa katika kesi ya msingi (National Bank of Commerce v Dar es Salaam Education and Office Stationery 1995 TLR 272 (CA)).

Tofauti kati ya Stop Order na Injunction (Amri ya Zuio)

Kwa hiyo basi, Stop order na Amri ya Zuio ni vitu viwili tofauti vitokanavyo na misingi tofauti ya kisheria. Wakati stop order ni zao la sheria Huru (substantive law) Amri ya zuio ni zao la sheria za kiutaratibu (Procedural Law). Stop Order inaweza kutolewa na mtu yeyote au mamlaka yeyote lakini amri ya Zuio inatolewa na Mahakama Pekee. Wakati Stop order ina asili ya kushinikiza utii wa kanuni zilizopo kwa mujibu wa sheria, Amri ya zuio in asili ya hukumu itokayo kabla ya kesi ya msingi haijasikilizwa, huku ikizingatia usumbufu na haki kufurahia mali baina ya wadaawa. Stop order haizingatii uwiano wa manufaa (balance of convenience) lakini Amri ya Zuio siku zote huzingatia uwiano wa manufaa baina ya wadaawa. Pia Stop Order inaweza tolewa baina ya watu au taasisi zisizo na mahusiano ya kimkataba au kiutendaji, wakati Amri ya zuio hutolewa baina ya pande zilizo katika mgogoro pekee. Stop orders hutolewa pasopo taratibu za kusikilizwa katika misingi ya kesi za madai (on preponderance of evidence) wakati Amri ya zuio usikilizwaji lazima ufanyike. Vilevile Stop Order inatoa wasaa kwa mhusika kukata rufaa dhidi ya order hiyo, wakati Amri ya Zuio haitoi wasaa wa kukatiwa rufaa (Hardmore Productions Ltd. and Others v. Hammilton And Another, [1983] 1 A.C 191, - Diplock, L.J., angalia pia Gazelle Tracker Limited v Tanzania Petroleum Development Corporation Civil Application no. 15 of 2006 (CAT, unreported)).

Hatua za kufuatwa katika Amri ya Zuio

Baada mmoja wa wadawa kuomba amri ya Zuio katika mahakama yenye mamlaka, ombi hilo husikilizwa (ikumbukwe kuwa maombi haya huwekwa mbele ya mahakama pale ambapo kesi ya msingi ilishafunguliwa). Mahakama ikishajiridisha kwa kuzingatia vigezo vinne vikuu, hutoa amri ya kuzui kutendeka kwa jambo fulani (prohibitive/restrictive injuction) au kulazimisha kufanya jambo fulani (mandatory injunction). Amri hii ikishatolewa (interim decree) hutolewa kwa mfumo wa drawn orders na wadaawa wote hupewa service ya hizi orders.

Amri za Zuio hazitakiwi kuwekwa kwenye mbao za matangazo au eneo husika ili kuzuia kitendo fulani kisifanyike. Hii si dhamira ya Amri hizi. Dhamira ya amri hizi ni kushinikiza ukaziaji wa “hukumu” iliyotolewa kabla ya uamuzi wa mwisho wa kesi ya msingi (ndio maana ya kuitwa temporary injunction). Kwa hiyo kama mmoja wa wadaawa hakuwepo siku amri hizi zinatolewa na mahakama upande ulioomba amri hizi unalazimika kumtafuta mdaawa aliyelengwa na amri hizi na kumpatia (serve).

Ukweli kuhusu kitu kinachotolewa kwa jina la Stop Order

Mahakama ina maafisa wa ngazi mbalimbali, ukianzia na makarani, mahakimu, mawakili, wasajili na majaji. Mahakama inapota amri (katika hukumu yake) hutoa kitu kinachoitwa decree (extracted decree or drawn orders). Hakimu au jaji mara nyingi hajihusishi na kuandika (extract) decree hizi. Makarani na wasajili hufanya hii kazi na hakimu au jaji ataweka saini yake baada ya kuandikwa kwa decree.

Iwapo mahakama imetoa amri yake ya zuio kutokana na sura ya 33 ya sheria za nchi (O. XXXVII) hakuna kitu kinachotakiwa kutolewa kinaitwa Stop order, hata kama chini yake itajitokeza saini ya jaji au hakimu. Watumishi wa Mahakama hasa makarani wamekuwa si wajuzi wa taratibu za kisheria kwa hiyo kwa namna moja au nyingine wanaweza kuandaa kitu kimeandikwa stop order na mamlaka husika ikaweka saini yake kwa kupitiwa. Kama kitu hiki kinajitokeza basi nyaraka hii inakuwa ni batili katika misingi ya sheria.

Baadhi ya mawakili, ama kwa kutojua au kwa kuhadaa wateja wao mamekuwa na mtindo wa kuandika vitu kama hivi pia wakinuia kutoa zuio linalotolewa na kisheria kwa mujibu wa sura ya 33 ya sheria za nchi. Kitu kama hiki ni batili pia.

Amri ya zuio na inayotumika kuzuia mtu, taasisi au serikali ni ile ambayo msingi wake unaanzia kwenye kesi yenyewe iliyoko mahakamani. Waathirika au wadaawa walalamikaji wanaweka maombi ya zuio mbele ya mahakama kwa kutumia fomu maalumu (chamber summons) na mahakama hupanga siku ya kusikiliza maombi hayo. Maombi lazima yasikilizwe na mahakama itoe uamuzi juu ya maombi hayo.

UHURU WA MAHAKAMA HAUJAINGILIWA

Kufuatana na hali hii ni wazi kuwa mahakama haijatoa Amri yoyote kuzuia bomoabomoa. Pia serikali au mamlaka yeyote ya serikali haikuvunja amri halali ya mahakama. Kwa hali hiyo basi uhuru wa mahakama umebaki imara kwa mujibu wa Ibara ya 107B ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

NINI KIFANYIKE

Elimu mahsusi itolewe kwa umma kuhusiana na uhuru wa mahakama na namna unavyokuwa. Wananchi waelimishwe ni kwa jinsi gani na misingi ipi mahakama inatoa Amri ya Zuio. Mawakili wawe wakweli kwa wateja wao na wasaidiane na serikali kutoa elimu husiaka. Maofisa wa mahakama hasa makarani wapewe elimu juu ya amri hizi, ikiwemo namna ya kuziandaa na mipaka iwekwe katika mamlaka inayotakiwa kutoa amri hizi. Pia umma ueleweshwe kubainisha order zinazotolewa na mahakama ikiwa katika muendelezo wa usikilizwaji kesi (mfano maintenance of status quo) na amri za stop/stay of execution.
Kamhadithie hizi ngonjera mtu uliyembomolea, halafu mwombe kura 2020.
 
Kesi za uhalali wa nyumba ni kesi tofauti kabisa na kinachozungumziwa hapa, na bado kesi nyingi ziko mahakamani zinasikilizwa. Cha mhumu uliza kwa nini wanabomolewa.
Vilevile hiyo hukumu ya uhalali wa nyumba ilete hapa. Ni nani aliyesema kuwa wanaobomolewa si wamiliki halali wa maeneo yale?
Pambafu!!!! Tunakujua wewe ni mnufaika wa hii serikali ya kidikteta ndio maana upo humu kutwa kumtetea dikteta
 
Pambafu!!!! Tunakujua wewe ni mnufaika wa hii serikali ya kidikteta ndio maana upo humu kutwa kumtetea dikteta
Ndugu kwenye andiko hilo kuna neno dikteta? Ok, mimi ni mnufaika wa serikali, je, inabadili ukweli uliopo?
 
  • Thanks
Reactions: UCD
Mbona unakuwa na akili ndogi, wewe unafikiri baada ya kumbomolea hajakusikia?
Tumia akili hiyonhiyo kubomoa zile nyumba 17,000 mabondeni!
Awamu kwa awamu. Bomoabomoa haijanza leo. Hata enizi za mzee ruksa ilikuwepo.
 
Je Humanitarian ground haipo kwenye bomoabomoa hiyo ?
 
Back
Top Bottom