Uhakiki wa vyeti umejaa dosari

Mkulia

JF-Expert Member
Apr 26, 2012
375
95
Habari za majukumu wadau wa JF.

Uhakiki wa vyeti uliofanywa na serikali kwa watumishi wa umma miezi michache iliyopita umejaa sana dosari.

Licha ya uhakiki kutohusisha watunga sera/sheria wetu uhakiki huo haujawagusa kabisa waajiriwa katika sekta binafsi na wale waliojiajiri wenyewe. Hali hii inaleta maswali mengi yasiyo na majibu.

Hata hivyo kwa watumishi wa umma tuliohakikiwa wapo wengi walioingizwa katika makosa ambayo hawakustahili. Mathalani wapo walioorodheshwa kuwa wameghushi vyeti wakati wana vyeti halali. Wapo walioorodheshwa kuwa hawakukamilisha kupeleka vyeti (incomplete) wakati walikabidhi vyeti vyao vyote kwenye zoezi la uhakiki.

Cha kushangaza zaidi katika zoezi hilo kuna watumishi ambao wamehesabiwa zaidi ya mara moja kwasababu katika vyeti vyao kimoja kilianza na majina yao ya kwanza (first name) na vyeti vingine vilianza na majina ya pili(surname). Mathalani, sekondari alitumia PETER JOHN na cheti kinasomeka hivyo na alipokwenda chuo majina yake yakasomeka JOHN PETER na cheti kinasomeka hivyo,huyu amehesabiwa Kama ni watumishi wawili tofauti na Kila mahali ameandikiwa incomplete ila vyeti vyote ni halali na ni vyake.

Katika mazingira haya yamesabisha watumishi hao kupata taharuki na kupoteza muda mwingi kufuatilia namna ya kutatua matatizo hayo badala ya kufanya kazi. Tunaomba serikali ilione hili na kutatua changamoto hii bila kuwaathiri watumishi hao.
 
Mleta mada naona umevulugwa,kwa upande wa private sector hawalipwi na Umma labda kwa upande wa afya huko wanaweza kuhakikiwa,Huku wanaangalia utendaji, vyeti havina nafasi huku ni ujuzi tu.
 
Kwanza zoezi lilikuwa si la kufuatilia vyeti fake ila zoezi lilikuwa ni la uhakiki wa watumishi wa umma ndani ya Serikali ule uhalali wako.

Sasa likifanyika Kuna jambo linabainika then linarudiwa kwa kuongeza wigo wa uhakiki then wanagundua mengine mapya kabisa then wanaongeza wigo na requirements za uhakiki.

Na hatimaye kuyabaini yote yaliyojulikana hayakufuata taratibu na vyeti fake, kutokamilisha,kutokuwa raia,na mengine kadha wa kadha.

Na waliowengi wameshindwa kuthibitisha kwa kuwasilisha original certificate baada ya buibiwa,kupoteza,kuharibika,kuungua moto,kwenda na mafuriko au Hata kutochukua tu kutoka alikosoma secondary O au AA level.

Mimi Nakumbuka nimekwenda chuo baada ya kumalizia A level kwa kutumia Result slip ambazo zilikuwa zinatolewa sambamba na matokea ya mtihani.

Sasa wengi wamejikuta njiapanda original hana kuthibitisha kuwa alipoteza hana ambazo ni mrefu kiasi kikanuni na kisheria wameingia huko nao mpaka watakapoleta uthibitisho wa vilivyopo ktk mafaili yao na walivyotakiwa kuwanavyo mikononi ili ijulikane ndiyo kweli hao ndiyo wahusika halali wa failing no so and so ktk documents hizo.
 
Naweza kukuunga mkono maana nimegundua kwa wale waliobeba cheti cha mtu kizima kizima na uyo mtu hayuko kwenye ajira ya serikali wamepona.Kuna mmoja namfaham yeye zoezi lilivyoanza akapeleka vyeti badae akapata mashaka kua wanaweza kumshtukia akaamua kukimbia kazi majibu yalivyokuja cheti kinaonekana sahihi..Ata ivyo ili zoez limeibua mengi,kuna ndugu yangu ambaye alivyomaliza kidato cha nne zaid ya miaka 16 iliyopita alijiajiri mwenyewe sasa juzi jina lake linaonekana kwenye vyeti feki kama muajiriwa serikalini alipofwatilia akagundua kuna mtu katumia cheti chake zaidi ya miaka 12 kazini na kachukua mkopo bank mara mbili na leseni ya udereva kwa jina ilo ilo.
 
Habari za majukumu wadau wa JF.

Uhakiki wa vyeti uliofanywa na serikali kwa watumishi wa umma miezi michache iliyopita umejaa sana dosari.

Licha ya uhakiki kutohusisha watunga sera/sheria wetu uhakiki huo haujawagusa kabisa waajiriwa katika sekta binafsi na wale waliojiajiri wenyewe. Hali hii inaleta maswali mengi yasiyo na majibu.

Hata hivyo kwa watumishi wa umma tuliohakikiwa wapo wengi walioingizwa katika makosa ambayo hawakustahili. Mathalani wapo walioorodheshwa kuwa wameghushi vyeti wakati wana vyeti halali. Wapo walioorodheshwa kuwa hawakukamilisha kupeleka vyeti (incomplete) wakati walikabidhi vyeti vyao vyote kwenye zoezi la uhakiki.

Cha kushangaza zaidi katika zoezi hilo kuna watumishi ambao wamehesabiwa zaidi ya mara moja kwasababu katika vyeti vyao kimoja kilianza na majina yao ya kwanza (first name) na vyeti vingine vilianza na majina ya pili(surname). Mathalani, sekondari alitumia PETER JOHN na cheti kinasomeka hivyo na alipokwenda chuo majina yake yakasomeka JOHN PETER na cheti kinasomeka hivyo,huyu amehesabiwa Kama ni watumishi wawili tofauti na Kila mahali ameandikiwa incomplete ila vyeti vyote ni halali na ni vyake.

Katika mazingira haya yamesabisha watumishi hao kupata taharuki na kupoteza muda mwingi kufuatilia namna ya kutatua matatizo hayo badala ya kufanya kazi. Tunaomba serikali ilione hili na kutatua changamoto hii bila kuwaathiri watumishi hao.
Huo ni uongo Chuo kikuu peke ndo wanabadili majina hivyo ikiwa kwenye SARIS ila wanapotengeneza transcript lazimaa uulizwe majina ya kwenye cheti/4&6.... So you are and your point is senseless!!
 
Mtoa post imekukuta nini ila serikali si imetoa maelekezo ya utaratibu wa kufuata kama unaona umeonewa?
Kama mtumishi anavyeti halali hawezi kuonewa mradi aviwasilishe,
 
Ndugu yangu Gormahia una uhakiki na kauli yako? Licha ya vyuo vikuu, vipi vyuo ambavyo katika vyeti majina huandikwa kwa kuanza na surname,mfano vyuo vya Ualimu.
 
Back
Top Bottom