Ugonjwa wa Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers Disease): Kinga, tiba na ushauri

Mimi nimeteswa na vidonda vya tumbo kwa miaka 17 tangia 1990 hadi 2007,nilipona kabisa, sasa naweza kula chakula chochote,pilipili nakula maharage na yala pombe nakunywa aina zote hadi zile kali.
Ushauri wangu;
1 Fuata masharti kwa makini mkubwa (uliza hayo masharti uelekezwe)
2 Jitaidi sana uwe unapata maziwa fresh mara kwa mara (lakini isiwe wakati wa usiku)
3 Chukua Karanga mbichi safisha vizuri halafu saga mpaka iwe laini kabisa,chukua Mdalasini iliyosagwa vizuri,chukua Asali ya nyuki wakubwa (Asali ya maji isiyochemshwa)
(a) Karanga nusu kilo
(b) mdalasini kijiko cha chakula vinne
(c) Asali kiasi ambacho ukichanganya pamoja unapata mfano uji mzito
.
Unachanganya pomoja vya kutosha halafu unakula kidogo wastani wa kijiko kimoja mara kwa mara hata kama ni zaidi ya mara sita kwa siku,ikiisha unaandaa nyingine hivyo hivyo,hakika itakusaidia sana ila ujue matibabu hayo siyo ya kupona haraka kama malaria huwa ni taratibu kwa muda mrefu,kikubwa zaidi zingatia masharti ya mtu mwenye vidonda vya tumbo.
Najua utapona kabisa kama utazingatia.MUNGU akutangulie.
 
Vidonda vya tumbo vya sumbua kinoma, H.pylori Kit mara 2 hakuna matokeo, kikombe cha Babu Lolio kimepita hakuna matokeo chanya, kasi ni ile ile tu, vinatulia na kukamata tena, pengine vinasabisha kichwa kiwe na mawenge, mwili kuuma hovyo, kukosa stamina, moyo kwenda mbio, kuhisi hasira zisizo na msingi...... Maoni na Ushauri Tafadhali!!!

Uchukue maganda ya komamanga Uyatwange mpaka yatowe unga ujazo wa kikombe cha kahawa na uchukue asali ujazo wa kikombe cha kahawa uchanganye pamoja na unga wa maganda ya komamanga utengeneze hivyo kila siku unywe asubuhi kikombe kimoja na jioni kikombe kimoja muda wa mwezi mmoja Inshaallah kwa uwezo wa Allah utapona.

Au hii ingine U
kinge Mkojo (Urine) wako glasi moja uwe unakunywa kila Asubuhi kabla ya kula kitu kwa muda wa wiki moja uende kupima hivyo Vidonda vyake vya Tumbo vitakuwa Vimekwisha kauka na Matatizo yake yatakuwa yamekwisha nasema kweli simtanii hiyo dawa imewasaidia wengi.
 
Maradhi ya VIDONDA VYA TUMBO (ULCERS): Haya ni maradhi ambayo hufanya vidonda upande wa ndani ya ukuta wa tumbo. Kuna Duodenal ulcer na Gastric ulcer.

DALILI: (1) Kupata maumivu makali chini ya kifua kwa
upande wa ndani. (2) Kuchoka bila sababu. (3) Kuumwa kwa mgongo au kiuno. (4) Kupungua kwa nguvu za kiume. (5) Kuwa na kichefuchefu baadhi ya wakati. (6) Kuwa na kiungulia . (7) Tumbo kujaa gesi. (8) Tumbo kuwaka moto. (9) Kukosa choo na wakati mwingine kupata choo kigumu kama cha mbuzi. (10) Kukosa hamu ya kula. (11) Kutapika damu au wakati mwingine kutapika nyongo. (12) Maumivu makali baada ya kula vitu vikali au chakula cha moto.

TIBA: Kanuni ya kwanza: Chukua asali robo lita uchanganye na unga wa arki susi vijiko vinne vikubwa kisha ukoroge kwa kijiko. Chukua vijiko viwili vikubwa vya mchanganyiko huu ukoroge ndani ya kikombe cha maji ya moto. Yakishapoa unywe kikombe kimoja kutwa mara tatu.

Kanuni ya pili: Chukua viazi vya mviringo (vya chipsi) kama vitatu halafu uvikoshe na kuvimenya. Baada ya kuvimenya upate juisi yake kwa kuvisaga kwenye blenda. Kunywa vijiko vitatu vikubwa vya chakula kutwa mara mbili. Kanuni ya tatu: Chukua lozi gramu 30 halafu usage iwe unga. Changanya lozi hii yote ndani ya kikombe kidogo cha maziwa ya moto kisha uongeze asali vijiko viwili vikubwa. Kunywa kikombe kimoja robo saa kabla ya kula chakula cha asubuhi. Fanya hivyo kwa muda wa mwezi na utapata shifaa.
 
Mkuu meza plasta utapona kabisa(joking)Kwa Rehabu usiende hana jipya,jitahidi kutosikia njaa yaani kukaa muda mrefu bila kula,nenda hospitali.
 
Naomba jaribu kuitafuta Aloe Vera Gel ni aina ya kinywaji ipo kama juice inasaidia kuponya vidonda vya tumbo, kuondoa sumu mwilini,kusaidia mmen'genyo wa chakula, pressure,kisukari haina ladha ukiinywa ipo kwenye chupa ya plastic ya njano ina lita1 unatakiwa unywe lita nzima mara moja baada ya hapo utakuwa unakunywa kidogo kidogo kwa siku at least mara mbili.Inauzwa chupa moja sh 41,011/= ukinywa ile ya mara moja utaarisha sana usije kushangaa ni sumu zilizokuwa mwilini zinatoka.Nakwambia hivi kwa kuwa nilikuwa na tatizo kama lako now I am ok.
 
Wasiliana na mimi dawa ipo utapona kabisa! Nilikuwa na vidonda serious hujapata kuona! Siku hizi natwanga maharage kama kawa! Tafadhali niandikie private email nitakupa contact zangu
 
i. Matango
Tengeneza juisi ya matango na kunywa kila kwenye mlo wako.
ii. Karela na mtindi
Majani ya karela 15 g
Mtindi glasi 1
Pondaponda majani ya karela, changanya na mtindi.
Matumizi:
Glasi 1 kila siku kwa muda wa mwezi 1.
iii. Bilinganya.
Katakata bilinganya vipande vidogo vidogo, chemsha na tia chumvi kidogo.
Matumizi:
Kula mara 2 kila siku kwa muda wa mwezi 1.
iv. Kabichi.
Kabichi ½ kilo
Maji ½ lita
Katakata kabichi vipande vidogovidogo, tia maji na chemsha hadi maji yawe ¼ lita tu.
Matumizi:
Kunywa maji yote baada ya kupoa, mara 2 kila siku kwa mwezi 1.
v. Ndizi.
Ndizi 2 za kupika na maziwa glasi 1 mara 4 kama chakula pekee kwa muda wa siku 14.

KUMBUKA:
Kabichi lina kemikali inayosaidia kuondoa vidonda vya tumbo
​ Asali na mdalasini inatibu maumivu ya tumbo pia hutibu vidonda vya tumbo kwenye shina la vidonda
 
umeelekeza dawa nyingi,unatumia zote kwa pamoja au ukipata mojawapo inatosha?
 
hii ni kitu muhimu sana kamanda, nilikuwa nimeshtuka kidogo baada ya kuona ni dawa nyingi, nikawaq najiuliza sasa kama natakiwa nitumie dawa zote hizi si itakuwa balaa? hivi hiyo kalela ndiyo nini? mi siijui kabisa, ikojeikoje?
 
hayo ni majani yamekaa yana rangi nyekundu masokoni yanauzwa kwa kilo yanafida sana hasa kwa wenye presha na upungufu wa damu mwilini
 
Hii ya mkojo naweza kujaribu. Nakumbuka kuna kipindi nilikuwa nikiumwa macho nilikuwa natumia mkojo kunawa, mara moja tu napona. Yaani mimi vidonda vya tumbo vimeweka kambi. Dawa ya feterawa nimetumia lakini wapi. Kuna kipindi nilitumia cimetidine nikapona na nikawa nagonga bia, harage n.k. Vilikuja kurudi kwa kasi, nikatumia cimetidine but wapi, dawa za kienyeji nimebadilisha kama tano hivi. Maumivu makali kweli tumboni na kifuani kama vinawaka moto. Kuna daktari kaniambia nikapime next week ila nisile nyama siku tatu kabla. Nikikuta bado ni ulcers nitatumia mkojo na hope nitapona.

Umetumia Mkojo? Umepona? Mimi vidonda vimepata nishani, havinitoki kabisa...
 
Kuna dawa nilitumia mimi na nikapona!
Kwa kikurya inaitwa "matotonia maiso",...ni kama majani flan hivi,waswahili wanaita vinasa nguo,..ukitembea kwenye nyasi kama yapo basi yanatoa vidude flani hivi vina nasa nguo kwa wingi!

Sasa basi,unachuma najani yake,unayatwanga kisha una loweka kwa masaa kama ma2 hivi!
Kunywa kama unakunywa maji,hata ukihisi kiu tumia kama maji ya kunywa tu!
Kila dawa unayo andaa itumike ndani ya siku hiyo pekee,ndani ya week1 kama vidonda sio vikali sana vitaisha,au kama ni vikali ongeza hata week2 au tatu!

Onyo:
1.ni majani na sio mizizi,mizizi yake ni tiba ya kitu kingine na sio vidonda vya tumbo!
2.usi chemshe,(ukichemsha ni dawa ya kitu kingine),..loweka tu

Ni yale majani ya kijani yanatoa viua vyeusi mfano wa maua ya alizeti na vichunga vinavyonasa kwenye nguo au nywele ukigusa? (zamani tuliita Manyolinyoli??)..
 
Pole sana ndugu unayeumwa! Pole sana

Kwanza kwa kuanzia ndugu vidonda vya tumbo vinasumbua sana na kupunguza quality of life. Hata hivyo zinatibika, tena kwa ufanisi mkubwa according to the very latest medical advances

Kwanza ni muhimu umuone daktari. Hilio ni muhimu. Pili ninachoweza kukushauri ni kwamba kama una matatizo ya tumbo ni ngumu sana kujua specifically ni ugonjwa gani mathalani inaweza kuwa unatoa 'acid' nyingi na inarudi kwenye koo kwa kitaalamu inaitwa gastro-oesophageal reflux disease (GERD) au pengine una kidonda kwenye utumbo i.e. peptic ulcer disease (PUD).

Matatizo haya yote yanaweza kukuletea matatizo ya tumbo na dalili zisipishane sana ikawa tabu kujua utibu vipi unless ufanyiwe kipimo. Kipimo hicho kinaweza kuwa kumezeshwa mpira wenye kamera i.e oesophago-gastroscopy (OGD). Kama vifaa vipo kinyama cha kupimwa hunyofolewa na pia urease breath test hufanywa au test yeyote na aina hii.

Ni muhimu kutofautisha hayo magonjwa mawili kwani japo dalili zake zinafanana lakini pia matibabu yake ni tofauti sana, tena sana.

Pamoja na kumsaidia muuliza swali lakini pia nimeamua kutoa maelezo haya marefu kwani kwa kiasi kikubwa vimelea vinavyosababisha vidoda vya tumbo vimehusishwa pia kuweza kusababisha aina mbalimbali za kansa. Matibabu ya vimelea hivi ni rahisi kama mgonjwa atazingatia kumaliza dawa.

Matibabu ya vidonda vya tumbo kwa kutumia dawa za kienyeji kama vile mkojo et al kwa kweli sifahamu hata kidogo lakini napata shida sana kuamini kama kweli vinatibu. The only thing I agree ni kwamba mkojo unakuwa na urea ambayo ni alkaline which might actually help katika ku-neutralize acid tumboni, lakini kamwe siyo kuua vimelea (H. pylori) vinavyosababisha tatizo lenyewe.

Life style change is another key component katika package nzima ya kudeal na vidonda vya tumbo.

I hope maeleza haya yatakusaidia katika mchakato wako wa kutafuta tiba ya tatizo lako. Hata hivyo naomba utambue kuwa maelezao niliyoyatoa ni general sana, na kwamba kila mgonjwa ana matibabu very individualized and tailored to his/her problem(s). And ethically, siyo rahisi ku-individualize matibabu kwenye social media au publicly, ndio maana nikukushauri ukamuone daktari ili muweze kuelezana kwa mapana na marefu yake

Otherwise pole sana mkuu
 
Back
Top Bottom