Ugonjwa wa Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers Disease): Kinga, tiba na ushauri

Castle

Senior Member
Jul 25, 2008
116
20
Habari za saa hizi wakuu,

Niende kwenye mada husika. Nina mwaka wa tano naumwa sana tumbo na maumivu yakiwa yanahama sehemu mbalimbali za tumbo wakati mwingine kifuani, kwenye, mbavu na hata kiuno na nyonga. Nimetumia madawa mbalimbali sipati nafuu.

Nimeshapima magonjwa kama yote. Nimejaza mafile ya makaratasi ya hospital. Natibu vidonda visivyopona. Sina raha nimepoteza ufanisi katika uchakalikaji wa kusaka kipato. Sina raha napata riziki si haba ila siifurahi. Sili ninachokitamani.

Nimeshafanya Endoscope 3 (mpira wenye kamera tumboni) zote zinaonyesha nina vidonda lakini nakunywa dawa siponi. Hii ya tatu nimefanya majibu yametoka baada ya week 3.Dokta kaniandika madozi mengine ila anipi ufafanuzi vizuri kama niko kwenye hali gani.

Niko stage gani? Ananiambia ni michubuko ya kawaida tu nitapona. kweli? mwaka wa tano mnanipa moyo tu? Aisee hata sielewi, nataka ukweli. Picha zinanishangaza nazidi pata wasiwasi zaidi. Na nimechoka kunywa dawa za hospital zinaniongezea maumivu hata sijui nifanyaje.

Tafadhali mtaalam yeyote ama aliyepitia changamoto kama zangu naomba msaada wako wa mali. Nishauri nifanyaje maana nilisikia mpaka mkojo wa asubuhi inaponya. Nilikunywa na sikupona.

Naambatanisha na majibu ya hospital pamoja na picha (OGD). Pia naomba kufahamu kwanini hii picha hapa chini ina vidude vyeusi ni alama ya vidonda kupona au ndio nazidi kulika.

Asanteni.



UFAFANUZI WA KITAALAMU KUHUSU TATIZO LA VIDONDA VYA TUMBO
Vidonda vya tumbo ni nini?
Vidonda vya tumbo ni matokeo ya kuharibika kwa uteute wa ndani ya ukuta wa tumbo la Chakula au ndani ya utumbo mdogo wa Chakula na matokeo yake ni ukuta wa tumbo kugusana na tindikali iliyoko tumboni ambayo ni kali sana kama maji ya betri.

Vidonda vya tumbo husababishwa na maambukizi ya bacteria waitwao HELICOBACTER PYLORI, aidha matumizi ya baadhi ya dawa za kutuliza maumivu za jamii ya Non_steroids anti inflammatory drugs kama vile ASPIRIN /DICLOFENAC huweza kusababisha uwezekano wa kupata ugonjwa huu.

Vidonda vya tumbo vinaweza kujitokeza katika utumbo mdogo na katika tumbo la Chakula na pia ni Mara chache huweza kujitokeza katika koo la Chakula ambapo hapakukusudiwa kustahimili tindikali ya tumbo.


AINA ZA VIDONDA VYA TUMBO (PEPTIC ULCERS DISEASE)
Kuna aina nyingi za vidonda vya tumbo navyo ni
(a) vidonda vinavyotokea katika mfumo wa Chakula yani tumboni
b) vidonda vinavyotokea katika utumbo mdogo
(c) vidonda vinavyotokea katika koo /koromeo la Chakula

HATUA KUU ZA VIDONDA VYA TUMBO
ni vizuri kufaham kwamba huu ugonjwa una hatua nne ambazo ni muhimu

(1)HATUA YA KWANZA ~hatua ya kwanza ya huu ugonjwa ni ule uvimbe sugu unaotokea sehem ya ndan ya tumbo.

(2)HATUA YA PILI~hapa vijidonda hujitokeza sehemu zenye uvimbe na taratibu vidonda hvyo huongezeka na kua vikubwa katika hatua hii mgonjwa hupatwa na maumivu makali ya tumbo yanayodumu kwa muda mrefu yakiambatana na kiungulia, tumbo kujaa gesi wakati wote, kukosa hamu ya kula, choo kuwa kigumu au kukosa choo kwa muda mrefu.

Hata hivyo Hali hii ya kukosa choo kwa muda mrefu (CHRONIC DYSPEPSIA) yani kushindwa kufanya Kazi kwa mfumo wa mmeng'enyo wa Chakula kutokana na tindikali nyingi inayozalishwa tumboni huingia Kwenye mzunguko wa dam hivyo mgonjwa hujisikia uchovu na kizunguzungu cha Mara kwa Mara katika hatua hii tindikali husababisha magonjwa ya ini na Figo kwa kuwa tayar iko katika mfumo mzima wa damu.

(3) HATUA YA TATU ~hii ni hatua ambayo ni ya hatari kwasababu vidonda vikubwa hupasua mishipa yote midogomidogo ya damu na kusababisha damu kuvia tumbon na kubadilisha rangi ya choo kuwa cyo ya kawaida, pia damu nyingi ikivujia tumboni mgonjwa hutapika na kuharisha damu Hali hii husababisha mgonjwa kuishiwa damu Mara kwa Mara, maumivu makali ya tumbo,hupata Homa, maumivu ya viungo na kukosa hamu ya kula.

(4)HATUA YA NNE ~katika hatua saratani ya utumbo inahusika kwani katika hatua hii vidonda vya tumbo hutengeneza tundu katika tumbo au utumbo mdogo na kusababisha kuoza kwa viungo vya ndani na matokeo yake ni saratani ya utumbo.

VISABABISHI/ VIHATARISHI VYA VIDONDA VYA TUMBO
visababishi vya ugonjwa huu vipo vingi sana hivyo yatupasa kuviepuka ili kujiepusha na huu ugonjwa.zifuatazo ni visababishi vya ugonjwa huu
i. Utumiaji wa madawa ya kuondoa maumivu kwa muda mrefu
ii.mawazo na huzuni kwa muda mrefu
iii.kutokuwa na muda maalum wa kula
iv.Utumiaji wa pombe uliopitiliza
v. Utumiaji wa madawa ya kulevya nk

DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO
~Dalili za vidonda vya tumbo ni nyingi ila sio wote wanaopata Dalili hizi Wana vidonda vya tumbo
i. maumivu makali au kiungulia maeneo ya chembe moyo (EPIGASTIC PAINS)
ii. kuvimbiwa au tumbo kujaa gesi Hali hii huweza kuendana na kucheua na kujamba Mara kwa Mara
ii. kutapika damu
iii. mtu mwenye vidonda vya tumbo (gastric ULCERS) hupata maumivu makali pindi anapokula au amalizapo kula
iv. mtu mwenye vidonda vya tumbo katika utumbo mdogo (duodenal ulcers) hupata maumivu makali pindi anapokua na njaa.
v. kupoteza hamu ya kula
vi. kupata haja kubwa yenye rangi damu Tena chenye harufu mbaya
vii. kupungua uzito

MATIBABU NA JINSI YA KUJIKINGA NA UGONJWA HUU
~matibabu ya ugonjwa huu yanapatikana vizuri nchini mwetu ila tatzo ni tiba yenyew kutokua na wataalamu wa kutosha wa kutibu chanzo cha tatizo na kumaliza tatizo pasipo kuleta matatzo mengine kutokana na matibabu yenyewe kuhusisha mfumo wa dawa za kemikal ambazo zina madhara kwa mhusika na pia , hivyo tiba bora kwa vidonda vya tumbo ni mlo kamili na dawa zisizo na kemikal pia tunapaswa kuepuka baadhi ya vyakula na kuzingatia masharti.

MAMBO YA KUFANYA KWA MWENYE VIDONDA VYA TUMBO
i. epuka kula vyakula vyenye viungo vingi kama vile pilau
ii. epuka kutumia pombe
iii. epuka ulaji wa vyakula vyenye sukari nyingi
iv. kula Chakula kidogo kwa muda maalum
v. kula vyakula vyenye fiber yan vyakula vyenye nyuzunyuzi ambavyo ni jamii ya mbogamboga na matunda
vi. epuka unywaji wa kahawa au kinywaji chochote chenye caffeine kiepuke

BAADHI YA USHAURI NA MAONI YALIYOTOLEWA NA WADAU
---
---
---
---
---
---
---
---
---


Pia unashauriwa kusoma:
1. Ushauri kuhusu dalili hatarishi za vidonda vya tumbo - JamiiForums

2. naomba kujua dawa asili ya Vidonda vya tumbo - JamiiForums

3. Yajue haya majani ni Dawa ya vidonda vya tumbo - JamiiForums

4. Ugonjwa wa Vidonda vya Tumbo (Peptic Ulcers Disease): Kinga, tiba na ushauri

5. Angalizo: Baadhi ya dalili za vidonda vya tumbo hufanana na dalili za magonjwa ya moyo - JamiiForums

6. Vyakula Vinavyoliwa na Mgonjwa wa Vidonda Vya Tumbo
 
Mwambie apunguze mawazo na awe ana kunywa mazima.

Ajitahidi kukimbia vyakula vyenye tindikali?? (Acid) kama Limau, ndimu, binzari, maharage, pombe kali au pombe kwa ujumla nk ...

Kwa nyie nduguze mjitahidi kuwa naye kwa karibu na kumkeep busy ili asiwe na muda wa kukaa na kufikiri saana.
 
Vidonda vya tumbo havisababishwi na kile unachokula bali kile kinachokula wewe hivyo tafadhali msaidieni kufaham ni nini kinamla? anawaza nini na kwakua ni mda mrefu sasa atumie maziwa wengine wanasisitiza ya mbuzi na kupunguza vitu vya acid kwakua tayari kuna michubuko.

Asante.
 
Katika matibabu yake alishapewa antibiotics yoyote au ni antihistamines tu?mara nyingi normal flora helicobacter pylori ndiyo chanzo kikubwa cha vidonda vya tumbo.

Sasa, kimatibabu pamoja na hizo H2antihistamines lazima uwadhibiti hawa jamaa pia kwa antibiotics.

Sikonge kakushauri vizuri,vidonda vya tumbo kama hypertension matibabu yake yanaambatana na lifestyle change. Kama anavuta sigara aache. Aepuke vyakula vyenye mafuta mengi,spices na vyenye acid. Asitumie any non steroidal antiinflammatory drug kama aspirin, ibuprofen nk.

Dawa pekee hazitoshi bila kubadili style yake ya maisha kwani vidonda vitakuwa haviponi au vitajirudia. Jaribu kuzingatia matibabu na ushauri wa daktari wako kabla hujaenda kwa waganga wa kienyeji
 
Katika matibabu yake alishapewa antibiotics yoyote au ni antihistamines tu?mara nyingi normal flora helicobacter pylori ndiyo chanzo kikubwa cha vidonda vya tumbo...
HELIGO KIT in antibiotics ndani yake!

Ushauri!

Aende kwa vipimo zaidi, inawezekana sio vidonda vya tumbo ambavyo tunavihisi/fahamu (hivyo vya H. pylori, NSAIDs, ama vya mawazo); yaweza kuwa ugonjwa mwingine kama Crohn's disease, matatizo ya kifuko cha nyongo, na syndrome yenye my favourite name- Zollinger-Ellison syndrome!
 

hahaha mazee umenikumbusha mbali sana na Zollinger-Ellison syndrome, lakini hata h2 antihistamines like cimetidine zingeiondoa kama ingekuwepo.

Anyway ushauri wako mzuri lakini mimi bado nasisitiza kuhusu kupata matibabu bora na kufuata ushauri wa daktari wake kama ugonjwa wake utabaki kuwa vidonda vya tumbo.
 
Dawa ya vidonda vya tumbo Mfahamishe huyo jamaa anayeumwa na Vidonda vya Tumbo atumie Dawa ya Hii ya Kienyeji Akiamka Asubuhi kabla ya kula kitu akojowe mkojo wake mwenyewe kwa kipimo cha Glasi moja awe anakunywa mkojo wake kila siku Asubuhi kabla ya kula kitu kwa muda wa Siku Saba kisha Aende kupima hivyo Vidonda vya Tumbo Vitapona na kukauka kabisa Mwambie ajaribu kutumia hiyo Dawa itamsaidia Sana.

Tahadhari:
Kabla ya kunywa huo Mkojo wake aende kupima Hospitali huo mkojo wake je unayo maradhi ya Zinaa au hauna? Ahakikishe Mkojo hauna Maradhi yoyote yale ndio anaweza kuutumia kwa kunywa .
 
Ndio Akinge (Urine) wake awe anakunywa kila Asubuhi kabla ya kula kitu kwa muda wa wiki moja aende kupima hivyo Vidonda vyake vya Tumbo vitakuwa Vimekwisha kauka na Matatizo yake yatakuwa yamekwisha nasema kweli simtanii hiyo dawa imewasaidia wengi.Kabla ya kunyw a:Mkojo wake akaupime hospitali je mkojo wake hauna maradhi yoyote yale? ndipo anaweza kutumia kwa kunywa.
 
Ndio Akinge (Urine) wake awe anakunywa kila Asubuhi kabla ya kula kitu kwa muda wa wiki moja aende kupima hivyo Vidonda vyake vya Tumbo vitakuwa Vimekwisha kauka na Matatizo yake yatakuwa yamekwisha nasema kweli simtanii hiyo dawa imewasaidia wengi.
Tena akiuvundika huo mkojo ndio bora zaidi, hata mie nimeona watu wamepona kwa dawa hiyo.
 
Tena akiuvundika huo mkojo ndio bora zaidi, hata mie nimeona watu wamepona kwa dawa hiyo.

Hizi dawa zingine jamani zahitaji moyo,ninachojiuliza huyu aliyegundua dawa hii alikuwa anatafuta nini mpaka akafanikisha ugunduzi huu,any way kama pretty na mzizimkavu wako serious though I can't see it in their words,mgonjwa akashauriwe atumie dawa husika.DAWA HII NI ZAIDI YA DAWA YA KIENYEJI.
 

Mzee wewe ni msabato masalia nini?!
 
Dawa ya vidonda vya tumbo ni mchanganyiko wa asali mbichi na juice ya alovera katika ratio ya 1:1. Tumia vijiko vya chakula viwili asubuhi, viwili mchana na viwili usiku kwa muda wa mwezi mmoja itakusaidia! Pia mwambie apunguze mawazo na ajitahidi kula ili tumbo lake liwe na digestable food material kwa muda mrefu!

How it works:
Kwanza, layer nene ya mchanganyiko huu hufunika kabisa vidonda vya tumbo na kuzuia uwezekano wa intestinal acids (e.g week hydrochloric acid, HCL) kuendelea kuishambulia ile ngozi laini iliyoathilika (vidonda).

Pili, wakati alovera juice (chemical) inatibu vidonda vya tumbo, asali inafanya kazi ya ku-hold still hiyo alovera chemical ili iendelee kukaa palepale kwenye kidonda(Asali inatumika kama binding material). So the mixture will persistently coat the infected area, hence it completely removes any further possibility of the intestinal acids and any other corrosive chemicals to reach that area.
 
Last edited:
Hizi ndio tiba mbadala wandugu na siyo utani!
Mkojo wako lakini, siyo wa mtu mwingine na unatibu magonjwa mengi sana.
 

Castle,

Kwanza mpe pole sana. Mimi siyo Daktari ila ninajua dawa ya kienyeji ambayo niliwahi kuelekezwa kwa ajili ya my wife wangu, na alipoitumia akapona kabisa na ninatamani siku moja nimpate Daktari aliyebobea katika ugonjwa huu anielezee kwa undani.

Dawa yenyewe ni hivi, chukua kokwa la parachichi, likatekate vipande vidogovidogo kisha anika juani mpaka likauke. Baadae saga ili kupata unga laini. Chukua yai la kuku wa kienyeji, pasua utoe kile kiini chenye rangi ya njano, changanya na ule unga ambao umeandaa awali, koroga ili kupata mchanganyiko mzuri.

Kisha mpe mgonjwa wako anywe kijiko kimoja mara tatu, baada ya siku tatu atakuwa amepona.

Baada ya hapo akitaka kujua kama amepona au la, anaweza kufanya test ya kawaida kabisa kwa kula maharage, au chakula chenye pili*2 au akaenda kupima hospitali kabisa.

Ukifanikiwa ni PM.
 
Ndugu Che Kalizozele hiyo Dawa niliyosema Ya kutibu Mgonjwa Wa Vidonda Vya Tumbo nimeipata katika vitabu vya zamani sana vya Uganga wa Kienyeji vya Mwaka 1200 na Huo Utaalamu wa Kutumia Mkojo Kwenye Hospitali hawajuwi hata Ma Proffeser hawaoni ndani usione kuwa natani hiyo ni kweli na wengi waliojaribu wamepona.

Hakuna Dawa Ya kutibu Vidonda vya Tumbo yaani kwa lugha ya kigeni ni (Ulser) hakuna Hospitali ipo ya kutuliza tu sio kutibu Kunguru Mweupe kuna Maradhi ambayo hayawezi kutibika Hospitalini lakini kwa Wataalamu wa Kienyeji wanaweza kutibu kama Ugonjwa wa Pumu ugonjwa wa kisukari, Ugonjwa wa Kifafa, Ugonjwa wa Wendawazimu Kupooza na Ugonjwa wa Saratani (Cancer) na Ugonjwa Hepatitis B Virus.

Mpaka sasa hakuna Dawa za kutibu hayo maradhi ila zipo za kutuliza sio kuyamaliza Maradhi kinachotakiwa kwa Mgonjwa ni kujaribu kutumia Dawa ili kuona kama itaweza kumsaidia sio kupinga jamani Wenzangu tunajaribu kuelimishana sina kushindana asanteni sana.
 
mafuta ya Mamba sio Dawa ya kutibu Maradhi ya Vidonda vya Tumbo Jaribu kutumia Urine (Mkojo) wako mwenyewe kila siku ukinge Asubuhi Glasi moja unywe kabla ya kula kitu kwa muda wa siku 10 kisha uende kupima utakuta vidonda vyote vya Tumbo vimekauka na hiyo wamejaribu watu wengi imewasaidia ukiweza fanya hukuweza Achana nao itawasaidia wengine wenye huo ugonjwa wa Vidonda vya Tumbo asante sana.
 
Inawezekana ikawa kweli,maana mimi nakumbuka ilikuwa 1994,nilikuwa nasumbuliwa na jino halafu nilikuwa ugenini nikuwa hapo Livingstone Zambia,sikuwa nafedha ya kutosha kung"oa jino nikashauliwa na mtu, lakini mimi hakuwa kunywa,niliambiwa asubuhi mapema kabla ya kula chochote nichukue glasi moja la mkojo wangu wa kwanza baada ya kuamka nisukutue kwenye meno na niteme kwa siku 3,nikafanya hivyo,leo ni mwaka 2009 sijawahi kuumwa jino mpaka leo,inawezekana Mzizi mkavu ni mkweli kabisa,kwani si ni mkojo wako kwani kunashida gani.
 
Lusajo Kyejo Waeleze wewe ndio labda watamini wanafikiri mimi ninawadanganya kuwa Mkojo wako mwenyewe unatibu Maradhi ya Vidonda vya Tumbo? wanafikiri ninasema maneno ya uongo jaribu kuwaeleza wewe labda wataelewa vizuri asante sana ndugu Lusajo Kyejo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…