kwani nini bana
Member
- Oct 13, 2012
- 25
- 4
Mwanawani asthma ni ugonjwa mgumu kweli. Kwa kifupi ni allergy. Tiba asilia ni effective ukiwa mdogo. Asthma ya ukubwani bwana ishu. Ni nakhshauri pia uchunguze vitu gani vinaweza kusababisha ubanwe kifua. Kuna ndugu yangu mmoja ana hilo tatizo. Ni zaidi ya miaka 10 sasa. Anapona baada ya muda inarudi. Ana allergy na perfumes, jiko la mkaa linapokuwa linawashwa ile harufu, jiko la mchina ndo uziseme, sabuni,lotion zenye harufu kali. So pia check una allergy na nini ili uepuke hicho kitu. So far dawa asili hazijamsaidia. All the time anatembea na inhaler halafu pia ana mashine home. Kikibana sana inhaler ili fail anaweka dawa fulani aina 2 anazichanganya ni za maji anaweka mask kuzunguka pua anachomeka kwenye umeme iyo mashine dawa inakuwa inamuingia thru mvuke. Hivyo vyote vikidunda tunakimbiza hosp haraka. Naweza kusema pumu yake ni kali kwa kweli ila ameshakubaliana na maisha yanaenda. Yako inaweza kuwa ni mild asthma. kwani kwa mwezi unabanwa mara ngapi? Sikukatishi tamaa but endelea kutafuta tiba hiyo asilia
Kwa hakika nakushukuru sana kwa maelezo yako na mifano uliyoitoa. Katika kuhangaikia hili tatizo kuna daktari pia alishawahi kunishauri kuhusu kuepuka harufu kali kama perfumes nk
Nakushukuru sana.