ugonjwa wa kichaa cha mbwa nisaidieni

Magu

Senior Member
Jun 13, 2011
156
56
Mwenzenu nafuga mbwa wawili nyumbani kwangu ambao nawapenda sana na ninawahudumia kwa chakula na mahitaji mengine kama malazi na matibabu. Leo nimekuwa na kazi ya kuwaogesha kwa dawa mimi mwenyewe, ila bahati mbaya mmoja wao mdogo wakati namuogesha alinikang'ata jino ktk mkono wangu, je naweza kuwa ameniambukiza ugonjwa wa kichaa cha mbwa au ugojwa mwengine wowote unaoambukizwa na mbwa? Katika kusoma niliwahi ona wataalamu wakidai kuwa si kila kuumwa na mbwa unaweza ambukizwa (Not every dog bites can infect rabies), naombeni ushauri wenu wanaJF
 
Pole Magu, ikiwa unawapatia chanjo ya kuwakinga na kichaa cha mbwa walau mara 1 kwa kila mwaka, basi huo ni usalama wako wa kwanza, pili yakupasa kesho asubuhi uende hospitali yoyote ya serikali iliyo karibu nawe wakutibu kidonda pamoja na kupatiwa kinga.
 
jamani pia naomba msaada kujua kama ugojwa huo unaweza kuambukiza kutoka mtu mmoja hadi mwinine? maana nimekua nikihudumia mtu alieugua kichaa cha cha mbwa na hatimae akafariki?
 
Back
Top Bottom