Ufujaji wa pesa unavyojengeka tangu utotoni

Ufujaji wa pesa unavyojengeka tangu utotoni

kbm

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2012
Posts
5,224
Reaction score
1,686
KWANZA kabisa namshukuru Mungu, muumba wa mbingu na ardhi kwa kunijaalia uhai, afya njema pamoja na nguvu za kutosha kiasi cha kuniwezesha kutimiza majukumu yangu ya kila siku.

Wiki iliyopita nilielezea kuhusu namna unavyoweza kuishi ukiwa umeishiwa, ni matumainiyangu kwamba mlijifunza mengi.
Wiki hii nitazungumzia mada inayohusu ufujaji wa pesa, tabia ambayo imekithiri kwa baadhi ya watu katika jamii yetu.

Siku zote matumizi ya pesa hayawezi kuwa sawa baina ya mtu na mtu ama familia na familia. Si rahisi mtu anayepokea mshahara wa shilingi milioni moja akawa na matumizi sawa na mtu anayepokea laki moja. Lazima kutakuwa na tofauti.

Lakini je, mwenye kipato kikubwa anapokuwa na matumizi makubwa ni sahihi mwenye kipato kidogo kusema mtu huyo anafuja pesa? Kama sio, kufuja pesa ni kupi?

Kufuja pesa ni kutumia pesa bila mpangilio tena wakati mwingine katika mambo ambayo hayana maana.

Ifahamike kwamba ufujaji wa pesa hauko katika anasa tu kama vile ulevi, kuhonga na mambo mengine kama hayo, bali pia katika mambo ambayo kimsingi hata yakikosekana katika maisha ya binadamu hayawezi kuleta athari.

Tafiti mbalimbali zimedhihirisha kwamba wengi ambao hutumia pesa ovyo ni athari za malezi waliyoyapata kutoka kwa wazazi wao tangu utotoni. Mzazi ndiye anayeweza kumfundisha mtoto kuwa ama kutokuwa na nidhamu katika pesa.

Unaweza kukuta watu wawili wanafanya kazi moja na wanalipwa mshahara sawa, lakini mmoja akawa na matumizi ya ovyo na kujikuta akiumaliza ndani ya siku chache na kulazimika kuanza kukopa ili kuweza kusogeza siku.

Kama nilivyoeleza hapo awali kwamba matumizi baina ya mtu na mtu hata siku moja hayawezi kuwa sawa, lakini ni ukweli usiofichika kwamba wapo wanaosifika kwa utumiaji mbaya wa fedha, athari ambayo inatokana na malezi kutoka kwa wazazi wao.

Ndiyo maana linapozungumziwa suala la utumiaji mbovu wa fedha kwa mtu fulani lazima historia itahusishwa katika hilo. Upo uwezekano mkubwa kwamba enzi za utoto wake wazazi wake walikuwa wakimpa pesa nyingi bila kujali mahitaji yake na kulazimika kuzitumia ovyo huku wazazi wakionesha kutojali. Katika mazingira kama hayo ni wazi kwamba athari hii itakuja kuonekana ukubwani.

Kitendo cha baadhi ya wazazi kuwapatia watoto wao fedha nyingi kama sehemu ya matumizi yao ya kila siku ni kuwalazimisha wazitumie kwa fujo kwani watakuwa wanajua kesho watapewa nyingine.

Mtoto kuanzia utotoni anatakiwa ajue ugumu wa kupata pesa, ajue kwamba bila kusoma, kufanya kazi ama kujishughulisha kwa namna yoyote hawezi kupata pesa. Unapompatia fedha mwanao kila anapohitaji bila kuhoji juu ya matumizi yake ni kumfanya aone kwamba hakuna ugumu wowote kupata pesa mazingira ambayo kisaikolojia yanaweza kumuathiri.

Hata kama pesa ipo lakini si wakati wa kumzoesha mtoto utumiaji wa ovyo wa pesa. Mpatie mahitaji yake muhimu lakini usimpe pesa nyingi kiasi cha kumlazimisha atumie atakavyo kwa sababu zipo.

Ninachosisitiza ni utumiaji mzuri wa pesa na wala sisemi uwe bahili, mgumu wa kutoa, mgumu wa kusaidia, hapana! Tena kwa kuitumia pesa yako katika kuwasaidia ambao hawajiwezi hata Mungu anakujaalia urahisi katika kupata pesa tofauti kabisa na unapoitumia pesa unayoipata katika starehe zisizo na msingi.

Lazima nidhamu itumike katika kutumia kila shilingi unayoipata laa sivyo mwisho wa siku tunaweza kujutia pesa ambazo tumezitumia ovyo kwa kufurahisha nafsi zetu ama kujipatia umaarufu.

Kwa kuzingatia hilo ndio maana katika umri mdogo mtoto anatakiwa kufundishwa nidhamu ya pesa, utumiaji makini wa pesa.

Kushindwa kwa mzazi kufanya hivyo ni kumtengenezea mtoto mazingira ya kuja kushindwa kutumia vizuri pesa zake ambazo atakuwa akipata.

Kwa hiyo kama hutakuwa makini na kila shilingi unayoipata leo, fahamu kufanikiwa katika maisha yako ni kitendawili.


GPL
 
Umeandika maneno yenye maana sana.Na ni mafunzo muhimu sana.Bila shaka utakuwa ni mchumi uliyebobea,Ni jambo muhimu kweli kwenye matumizi ya pesa,unaweza kutumia pesa kwa mambo ya starehe,lilikutokea jambo la dharura,inakuwa huna pesa,unaanza kukopa.Somo lako zuri sana.Japo uzi kama huu huwezi pata wa kuchangia,kwa vile wa Tanzania tumezoea starehe sana.
 
Nakubaliana na hoja yako, mtoto hufunzwa angali mdogo akikua ni kupractise alichojifunza.
Watu wengi wanalalamika ni maskini na hawana hela ila ukiangalia pesa iliyopita mikononi mwao ni ya kutosha kujenga majumba na kuwa na biashara za maana.
Matumizi ndo tatizo, wengi wanamatumizi yasiyo ya lazima ambayo hayana faiuda kwao wala vizazi vyao. :A S thumbs_up::A S thumbs_up:
 
Kweli kabisa, somo hili ni zuri sana. Vijana inabidi tubadilike hata kama malezi ya kutojua ugumu wa pesa tuliyapitia. Nakuunga mkono sana kwani vijana wengi unakuta wanaingiza pesa hila kabla hata mwezi aujaisha wanakwenda kukopa na ndio imekuwa tabia ya kila siku.Nakumbuka wazazi wakinipa pesa kwenda kununua kitu au kufanyia matengenezo ya kitu, hata kama imebaki shilingi kumi walikuwa wanaidai na ndio hapo nilianza kujifunza namna nzuri ya kutumia pesa. Asante sana mwalimu kwa mada ya leo.
 
Nimekuelewa mdau, vipi sisi watoto wa mbwa ambao tulikuwa hatupewi hela nyingi lakini tumejikuta hatuna nidhamu ya matumizi kama wengine tu.
 
Umenena bro. Bravo kabisasi unajua ufahari nao ni ujinga mkubwa kwa wazazi kwenda watoto hao. Kikwajuni One hujakosea. Thread hii haitapata wachangiaji kwani ndo utamaduni wa Bongo-jema haliungwi mkono na la hovyo linashobokewa saaaana.
 
Kuna ukweli japokuwa si kwa wote. Kuna watoto waliokuwa wanapewa pesa nyingi kama matumizi kumbe hawatumii, wanahifadhi na kuja kuanzisha biashara àmbayo mzazi anashangaa katoa wapi hela. Watoto wengi wa kichaga wako hivyo, na kuna uzi unamzungumzia tajiri bilionea yuko arusha kwa kuuza solar alianzia huko. Mdogo wangu (muha) anayenifuata, kamaliza sua akiwa àmenunua pkpk na badaye akanunua bajaji, inasomba wanafunzi. Ukimwuliza pesa kapata wapi, ni mkusanyo wa pesa za matumizi alizokuwa anapewa na wazazi.
 
Umenena bro. Bravo kabisasi unajua ufahari nao ni ujinga mkubwa kwa wazazi kwenda watoto hao. Kikwajuni One hujakosea. Thread hii haitapata wachangiaji kwani ndo utamaduni wa Bongo-jema haliungwi mkono na la hovyo linashobokewa saaaana.
Nafikiri katika Dunia,wa Tanzania twaongoza kwa kutumia pesa ovyo,uko uzi niliuona humu jf.jinsi dada zetu wanavyomaliza pesa kwa viatu,nguo,vipodozi.
Na kwa wanaume kwa starehe za ma bara,madisco,kula lunch au diner kwenye mahoteli ya kifahari.Nakumbuka wakati fulani,siku za nyuma,yupo rafiki angu,alituchukuwa rafiki zake kama wanne,akatupeleka Hotel ya kitalii,juice glass ilikuwa ni 8000,kahawa kikombe 3000.Mmoja kati yetu alikuwa ni mtu mzima wa makamo,akamwambia yule rafiki yangu,Bora twende Kariakoo,juice kama ile ni shiling mia tano tu,na pesa itakayobakia katika zile elfu nane mara idadi yetu,apewe yeye.Yule rafiki yangu alikataa kumsikiza,yule mzee akasema nipe hiyo 8000 ya juice,itanisaidia mambo muhimu.Akampa,na hakunywa juice.Angemsikiza yule mzee,angekuwa anaokoa pesa ngapi,anazotumia kwa ufahari.Ufahari ni mama wa ujinga kweli.
 
Tunapenda vijisherehe vya hovyo hovyo, mara mwanangu leo birthday yake namfanyia sherehe, mwanangu kamaliza kidato cha nne namfanyia sherehe, leo miaka 10 ya ndoa yetu tunafanya sherehe na vitu vingi kama hivyo.
 
Tunapenda vijisherehe vya hovyo hovyo, mara mwanangu leo birthday yake namfanyia sherehe, mwanangu kamaliza kidato cha nne namfanyia sherehe, leo miaka 10 ya ndoa yetu tunafanya sherehe na vitu vingi kama hivyo.
 
Nimekuelewa mdau, vipi sisi watoto wa mbwa ambao tulikuwa hatupewi hela nyingi lakini tumejikuta hatuna nidhamu ya matumizi kama wengine tu.


yaani ndugu umenea,mi nkikumnbuka bi mkubwa alivokuwa mchungu,ajabu tangu nakua
i was very disciplined in money matters,but cku izi,yaani ukinipa elfu kumi saa 2 asubuhi,saa saba mchana kwishnei..mpaka najiuliza ivi nina matatizo gani..???
au kwa sababu hela natafuta mwenyewe siku izi...??
NaAMINI nahitaji some help,kisaikolojia au kwa maombi..maana!!
Mhhh...
 
yaani ndugu umenea,mi nkikumnbuka bi mkubwa alivokuwa mchungu,ajabu tangu nakua
i was very disciplined in money matters,but cku izi,yaani ukinipa elfu kumi saa 2 asubuhi,saa saba mchana kwishnei..mpaka najiuliza ivi nina matatizo gani..???
au kwa sababu hela natafuta mwenyewe siku izi...??
NaAMINI nahitaji some help,kisaikolojia au kwa maombi..maana!!
Mhhh...

hahahaaa unatisha mkuu hilo ni pepo njoo nikuombee
 
Naunga mkono hoja.

Hata mimi ninatatizo hilo,kutokana na hii mada I've to change.
 
Nimegundua kitu, kama sio mtumiaji wa kilevi basi ni kwamba tu hela hazitoshi. Maana ukijiangalia kama hujatumia kwa matumizi yoyote mabaya basi sio mfujaji. Tabu ni kuwa inakuja hele kidogo halafu inakuta mambo kama milioni inasubiri hiyo hiyo hela.
yaani ndugu umenea,mi nkikumnbuka bi mkubwa alivokuwa mchungu,ajabu tangu nakua
i was very disciplined in money matters,but cku izi,yaani ukinipa elfu kumi saa 2 asubuhi,saa saba mchana kwishnei..mpaka najiuliza ivi nina matatizo gani..???
au kwa sababu hela natafuta mwenyewe siku izi...??
NaAMINI nahitaji some help,kisaikolojia au kwa maombi..maana!!
Mhhh...
 
Back
Top Bottom