Ufisadi wa kutisha Elimu Singida (v)

Ufisadi wa kutisha Elimu Singida (v)

Nyaflora

Member
Joined
Feb 4, 2015
Posts
14
Reaction score
0
Mkaguzi wa ndani wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida ameibua wizi wa fedha za Umma kama ifuatavyo. Tsh.170 milioni zina vielelezo vya mashaka, Tsh.130 milioni hazina vielelezo,na milioni 30 za mitihani zimeliwa na watu watatu wa Elimu msingi na sekondari kwa kufanya manunuzi hewa.

Hao maofisa Elimu Watatu majina yao niliyasikia wakiwa wanajadiliwa na watumishi wengine wa kada ya chini ambao hawafaidiki na ufisadi huo,bali wamekuwa wakiishia kuwaona mabosi wao wakibadili vyombo vya usafiri.Maeneo yanayotajwa ni mengi,niliyo yasikia ni hayo.

Source: ni mimi mwenyewe nimewasikia Baadhi ya wahudumu wa ofisi hiyo ya DED wakinong`ona nje ya ofisi wakisikitikia mabosi wao kwa waliyo ya fanya hadi kutishia utumishi wao pindi ikithibitika kufanya ufisadi huo.

Hata hivyo moja wa wahudumu hao alilalamika kuwa mabosi hao wote ni mabahili pindi wakipiga madili ya aina hiyo.Safari hii imetibuka.
 
Aisee,hiyo mbona kali?Hope takukuru na vyombo vingine vitapata taarifa na ku act mara moja.Halmashauri wamekuwa wadokozi sana kuelekea uchaguzi mkuu wakijua viongozi wakuu na madiwani akilizao zipo kwenye chaguzi
 
Ufisadi ktk halmashauri ni kawaida tu...

Shida wanapiga ela mbuz,
wangekuwa wanapiga kama wenzao wa serikali kuu.
 
Ufisadi ktk halmashauri ni kawaida tu...

Shida wanapiga ela mbuz,
wangekuwa wanapiga kama wenzao wa serikali kuu.

Umeonae,ila Walimu ndo wanakomaga,haki zao nyingi zinapokwa.Maafisa wanajichotea
 
Safi sanaa! mtanzania ukipata sehemu ya kupiga piga tu, pinda alisema wapigwe tu..!
 
Nyaflora,

Huku kutakuwa jimboni kwa tundu lisu. hana uchungu kabisa kwani wanae hawasomi huko.
 
Last edited by a moderator:
Utakula kwa urefu Wa kamba yako,wacha wazipige...nami nikipata chance napiga....
 
Nimeaona kuna dalili vyombo husika vimeanza kuchukua hatua stahiki,jamaa wanaitwa mmoja mmoja kujieleza.Tusubiri matokeo kama ndo wenyewe,au wamtembelewa na wadau wao.TUTAJUA BAADAYE
 
Back
Top Bottom