Ufisadi ttcl

Kyenju

JF-Expert Member
Joined
Jun 16, 2012
Posts
5,143
Reaction score
2,547
Wakati Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, January Makamba, alitarajiwa kukutana na wafanyakazi wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) jana, viongozi wakuu wake wanatuhumiwa kufanya ufisadi unaoiangamiza kampuni hiyo ya umma.

Kila mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi analipwa Sh. milioni moja kwa siku; hizo zikiwa nje ya marupurupu mengine.

Pia imebainika kuwa mamilioni ya shilingi hupotea kutoka kwenye makusanyo ya kanda, huku Dar es Salaam ikiwa kama kitovu cha ufisa huo.
 
Kwa hiyo kuna mtanzania kwa mwezi anavuta mill 30
Ngoja niwahi panadol... kichwa kimeshaanza kuniuma
 
Kwa hiyo kuna mtanzania kwa mwezi anavuta mill 30
Ngoja niwahi panadol... kichwa kimeshaanza kuniuma

Mil 30 ukiongeza na marupurupu ni = na mil?
 
wanamalizia kugawana fito TTCL imeshauzwa, kauziwa mdogo wake SAS
 
kuna uzi ulianzishwa asubui jukwaa la siasa naona umeondolewa kuhusu makamba kuzungumza na wafanyakazi TTCL naona haupo kunani sjui
 

Duuu....hao watu hawafikirii watanzania wenzao wenye uhaba wa chakula???
 

Hapa kwetu songea, ofisi nyingi TTCL ndio net. provider. Imenichefua hii taarifa kwani toka ijumaa ofisi nyingi zimeshindwa kutoa huduma kwa tatizo dogo lenye hadithi kibao.

Tumeshindwa fanya kazi system zote chali hadi aibu kwa wateja na usumbufu mkubwa achilia mbali upotevu wa mapato kwa serikali. Inauma sana. Kama ni kweli ufisadi huo wafanyika hapo, nadhani ni byema ipitishwe sheria ya dharura kuwafilisi na wanyongwe hadharani.
 

Wataweza kuusimamia mkongo wa taifa?
 
Nilipomuona tu Mkurugenzi Mkuu wa TTCL kwenye kikao cha wafanyakazi nikapata jibu moja tu,kumbe ndio maana TTCL haiwezi kupiga hatua katika ulimwengu huu wa dijitali pamoja na kuwa ina nyenzo kubwa kuliko kampuni yoyote ya simu,sijui mtendaji mkuu huyo kama anajua hata kufungua tu kompyuta .Nilitegemea kampuni kama TTCL iongozwe na dotcom wa ukwee na si wa kuchongwa,teknilojia inabidilika kila kukichwa sasa yule ndugu naona yeye anawaza mingo tu,na sijui kwanini bwana Utoah & Co hajapitia huko hadi Waziri aseme !!
 

katika ma ceo wote tanzania naona huyu ndiye ceo wa kwanza kushindwa usaili lakini bado anaongoza ttcl. Yeye mwenyewe kamwambia january afanye haraka kuipatia ttcl uongozi mpya sijui kwanini bado wizara inamng'ang'ania wanataka ttcl ife!!!!!!!
 
katika ma ceo wote tanzania naona huyu ndiye ceo wa kwanza kushindwa usaili lakini bado anaongoza ttcl. Yeye mwenyewe kamwambia january afanye haraka kuipatia ttcl uongozi mpya sijui kwanini bado wizara inamng'ang'ania wanataka ttcl ife!!!!!!!

Mbona TZ tunao vijana wengi na wasomi wazuri ktk ICT na TEHAMA kwa ujumla na wako very active, kwanini tunag'angania kampuni kubwa kama hii iongozwe na watu wasio na vision?
 
Kwa hiyo kuna mtanzania kwa mwezi anavuta mill 30
Ngoja niwahi panadol... kichwa kimeshaanza kuniuma

Yaani milioni 30 kwa mwezi inakutisha,mbona ni vijisenti tu!

Nothing comes to a sleeping man but dreams-Tupac Shakur
 
Wasubiri nguvu ya umma itakachowafanya

Nguvu ya umma is just a fairytale,jiangalie wewe na familia yako,that's what I'm doing.

Nothing comes to a sleeping man but dreams-Tupac Shakur
 
Kuna tetesi kuwa waliotuhumiwa wote,CEO anastaafu kuanzia kesho na wengine wamewekwa nje ili uchunguzi ufanyike kama alivyosema makamba.


Makamba oyeeeeeeeee

Mbarawa ziiiiiiiiiiiiiiiii
 
Kuna tetesi kuwa waliotuhumiwa wote,CEO anastaafu kuanzia kesho na wengine wamewekwa nje ili uchunguzi ufanyike kama alivyosema makamba.


Makamba oyeeeeeeeee

Mbarawa ziiiiiiiiiiiiiiiii

Mkuu si tetesi ni wamewekwa pembeni imekuja safu mpya kabisa ikiongozwa na Kamugisha Kazaura uyu jamaa nna imani naye hasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…