Walio fanya vizuri aje? Kukariri? Then baada ya hapo watuundie Ndege? Kukariri types of Rock, Coffee Farming in Brazili na kujua tarehe Vita kuu ya kwanza ya Dunia ilianza hizo sio akili ni mambo ya kukariri, Dunia isha hama huko kutambo sana Wakenya hawakuw wajinga kupiga stop mitihani ya Taifa, Bongo bado mnaabudu Div
Kenya wameacha mitihani ya kitaifa? Na hii KCSE na hawa best students wa mwaka jana ni ya wapi?
Kukariri kama sio sehemu ya kipimo cha akili ungekuwa hujui hata jina lako ambalo ulipewa, ulisikia wanakuita na ulifundishwa kuliandika. Hata kuvaa ungevaa sketi, maana umekariri umekuta wanaume wanavaa mavazi unayovaa sasa.
Hao waunda ndege huwa wanarudia kilekile kilichogunduliwa kwani. Si wanasoma kilichopo (kukariri na kuelewa) kisha wanafanya improvement. Yani unadhani Boeing kuna kichaa anayeenda pale anajikuta genius kisha aanze kuunda landing gear upya bila kuangalia na kukariri zilizopo na kuboresha, au unadhani pale Mercedes Benz unadhani kuna fala anaenda anaanza upya kuunda injini bila kusoma (kukariri na kuelewa) models na wapi kunahitaji improvement kama kudeal na torque, HP, carbon emission na fuel consumption, wakati kazi ya kuvumbua injini ilifanywa na Karl Benz late 1800s.
Kama huwezi kariri wewe moja kwa moja ni kilaza. Huo ni uwezo wa kawaida kabla hatujaja kwenye innovation, renovation na creation. Wewe unataka kidato cha pili wapewe mabati waunde helicopter bubu bila kujua basic laws of physics? Sasa nchi kama nchi yenye watu milioni 61 itajuaje kama wanafunzi milioni 2 wameelewa, wafuatwe mmoja mmoja nyumbani kwao wapewe mabati waunde ndege? Assessment ambayo ni convenient, possible, low cost, ya muda mfupi, standardized kuondoa lawama na inayopimika ni mitihani.
Hata kwenye kutoa hoja tu akili inapimwa. We unataka NECTA wawe na makenta yabebe vyuma wanafunzi wakaunde makabati sijui